< תהילים 55 >
למנצח בנגינת משכיל לדוד ב האזינה אלהים תפלתי ואל-תתעלם מתחנתי | 1 |
Kwa mwimbishaji. Na ala za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, sikiliza maombi yangu, wala usidharau hoja yangu.
הקשיבה לי וענני אריד בשיחי ואהימה | 2 |
Nisikie na unijibu. Mawazo yangu yananisumbua na nimehangaishwa
מקול אויב--מפני עקת רשע כי-ימיטו עלי און ובאף ישטמוני | 3 |
kwa sauti ya adui, kwa kukaziwa macho na waovu, kwa sababu wananiletea mateso juu yangu na kunitukana kwa hasira zao.
לבי יחיל בקרבי ואימות מות נפלו עלי | 4 |
Moyo wangu umejaa uchungu, hofu ya kifo imenishambulia.
יראה ורעד יבא בי ותכסני פלצות | 5 |
Woga na kutetemeka vimenizunguka, hofu kuu imenigharikisha.
ואמר--מי-יתן-לי אבר כיונה אעופה ואשכנה | 6 |
Nilisema, “Laiti ningekuwa na mbawa za njiwa! Ningeruka niende mbali kupumzika.
הנה ארחיק נדד אלין במדבר סלה | 7 |
Ningalitorokea mbali sana na kukaa jangwani,
אחישה מפלט לי-- מרוח סעה מסער | 8 |
ningaliharakisha kwenda mahali pa salama, mbali na tufani kali na dhoruba.”
בלע אדני פלג לשונם כי-ראיתי חמס וריב בעיר | 9 |
Ee Bwana, uwatahayarishe waovu na uwachanganyishie semi zao, maana nimeona jeuri na ugomvi mjini.
יומם ולילה--יסובבה על-חומתיה ואון ועמל בקרבה | 10 |
Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake, uovu na dhuluma vimo ndani yake.
הוות בקרבה ולא-ימיש מרחבה תך ומרמה | 11 |
Nguvu za uharibifu zinatenda kazi mjini, vitisho na uongo haviondoki mitaani mwake.
כי לא-אויב יחרפני ואשא לא-משנאי עלי הגדיל ואסתר ממנו | 12 |
Kama aliyenitukana ni adui yangu, ningevumilia, kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu, ningejificha asinione.
ואתה אנוש כערכי אלופי ומידעי | 13 |
Kumbe ni wewe, mwenzangu, mshiriki na rafiki yangu wa karibu,
אשר יחדו נמתיק סוד בבית אלהים נהלך ברגש | 14 |
ambaye awali tulifurahia ushirika mzuri, tulipokuwa tukienda na umati hekaluni mwa Mungu.
ישימות (ישי מות) עלימו--ירדו שאול חיים כי-רעות במגורם בקרבם (Sheol ) | 15 |
Kifo na kiwajie adui zangu ghafula, na washuke kuzimu wangali hai, kwa maana uovu upo ndani yao. (Sheol )
אני אל-אלהים אקרא ויהוה יושיעני | 16 |
Lakini ninamwita Mungu, naye Bwana huniokoa.
ערב ובקר וצהרים אשיחה ואהמה וישמע קולי | 17 |
Jioni, asubuhi na adhuhuri ninalia kwa huzuni, naye husikia sauti yangu.
פדה בשלום נפשי מקרב-לי כי-ברבים היו עמדי | 18 |
Huniokoa nikawa salama katika vita vilivyopangwa dhidi yangu, ingawa watu wengi hunipinga.
ישמע אל ויענם-- וישב קדם סלה אשר אין חליפות למו ולא יראו אלהים | 19 |
Mungu anayemiliki milele, atawasikia na kuwaadhibu, watu ambao hawabadilishi njia zao, wala hawana hofu ya Mungu.
שלח ידיו בשלמיו חלל בריתו | 20 |
Mwenzangu hushambulia rafiki zake, naye huvunja agano lake.
חלקו מחמאת פיו-- וקרב-לבו רכו דבריו משמן והמה פתחות | 21 |
Mazungumzo yake ni laini kama siagi, hata hivyo vita vimo moyoni mwake. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, hata hivyo ni upanga mkali uliofutwa.
השלך על-יהוה יהבך-- והוא יכלכלך לא-יתן לעולם מוט-- לצדיק | 22 |
Mtwike Bwana fadhaa zako, naye atakutegemeza, hatamwacha kamwe mwenye haki wake aanguke.
ואתה אלהים תורדם לבאר שחת-- אנשי דמים ומרמה לא-יחצו ימיהם ואני אבטח-בך | 23 |
Lakini wewe, Ee Mungu, utawashusha waovu katika shimo la uharibifu. Wenye kiu ya kumwaga damu na wenye hila, hawataishi nusu ya siku zao. Lakini mimi ninakutumaini wewe.