< תהילים 55 >

למנצח בנגינת משכיל לדוד ב האזינה אלהים תפלתי ואל-תתעלם מתחנתי 1
Kwa mwimbishaji. Na ala za uimbaji. Utenzi wa Daudi. Ee Mungu, sikiliza maombi yangu, wala usidharau hoja yangu.
הקשיבה לי וענני אריד בשיחי ואהימה 2
Nisikie na unijibu. Mawazo yangu yananisumbua na nimehangaishwa
מקול אויב--מפני עקת רשע כי-ימיטו עלי און ובאף ישטמוני 3
kwa sauti ya adui, kwa kukaziwa macho na waovu, kwa sababu wananiletea mateso juu yangu na kunitukana kwa hasira zao.
לבי יחיל בקרבי ואימות מות נפלו עלי 4
Moyo wangu umejaa uchungu, hofu ya kifo imenishambulia.
יראה ורעד יבא בי ותכסני פלצות 5
Woga na kutetemeka vimenizunguka, hofu kuu imenigharikisha.
ואמר--מי-יתן-לי אבר כיונה אעופה ואשכנה 6
Nilisema, “Laiti ningekuwa na mbawa za njiwa! Ningeruka niende mbali kupumzika.
הנה ארחיק נדד אלין במדבר סלה 7
Ningalitorokea mbali sana na kukaa jangwani,
אחישה מפלט לי-- מרוח סעה מסער 8
ningaliharakisha kwenda mahali pa salama, mbali na tufani kali na dhoruba.”
בלע אדני פלג לשונם כי-ראיתי חמס וריב בעיר 9
Ee Bwana, uwatahayarishe waovu na uwachanganyishie semi zao, maana nimeona jeuri na ugomvi mjini.
יומם ולילה--יסובבה על-חומתיה ואון ועמל בקרבה 10
Usiku na mchana wanazunguka juu ya kuta zake, uovu na dhuluma vimo ndani yake.
הוות בקרבה ולא-ימיש מרחבה תך ומרמה 11
Nguvu za uharibifu zinatenda kazi mjini, vitisho na uongo haviondoki mitaani mwake.
כי לא-אויב יחרפני ואשא לא-משנאי עלי הגדיל ואסתר ממנו 12
Kama aliyenitukana ni adui yangu, ningevumilia, kama mtu mwovu angejiinua dhidi yangu, ningejificha asinione.
ואתה אנוש כערכי אלופי ומידעי 13
Kumbe ni wewe, mwenzangu, mshiriki na rafiki yangu wa karibu,
אשר יחדו נמתיק סוד בבית אלהים נהלך ברגש 14
ambaye awali tulifurahia ushirika mzuri, tulipokuwa tukienda na umati hekaluni mwa Mungu.
ישימות (ישי מות) עלימו--ירדו שאול חיים כי-רעות במגורם בקרבם (Sheol h7585) 15
Kifo na kiwajie adui zangu ghafula, na washuke kuzimu wangali hai, kwa maana uovu upo ndani yao. (Sheol h7585)
אני אל-אלהים אקרא ויהוה יושיעני 16
Lakini ninamwita Mungu, naye Bwana huniokoa.
ערב ובקר וצהרים אשיחה ואהמה וישמע קולי 17
Jioni, asubuhi na adhuhuri ninalia kwa huzuni, naye husikia sauti yangu.
פדה בשלום נפשי מקרב-לי כי-ברבים היו עמדי 18
Huniokoa nikawa salama katika vita vilivyopangwa dhidi yangu, ingawa watu wengi hunipinga.
ישמע אל ויענם-- וישב קדם סלה אשר אין חליפות למו ולא יראו אלהים 19
Mungu anayemiliki milele, atawasikia na kuwaadhibu, watu ambao hawabadilishi njia zao, wala hawana hofu ya Mungu.
שלח ידיו בשלמיו חלל בריתו 20
Mwenzangu hushambulia rafiki zake, naye huvunja agano lake.
חלקו מחמאת פיו-- וקרב-לבו רכו דבריו משמן והמה פתחות 21
Mazungumzo yake ni laini kama siagi, hata hivyo vita vimo moyoni mwake. Maneno yake ni mororo kuliko mafuta, hata hivyo ni upanga mkali uliofutwa.
השלך על-יהוה יהבך-- והוא יכלכלך לא-יתן לעולם מוט-- לצדיק 22
Mtwike Bwana fadhaa zako, naye atakutegemeza, hatamwacha kamwe mwenye haki wake aanguke.
ואתה אלהים תורדם לבאר שחת-- אנשי דמים ומרמה לא-יחצו ימיהם ואני אבטח-בך 23
Lakini wewe, Ee Mungu, utawashusha waovu katika shimo la uharibifu. Wenye kiu ya kumwaga damu na wenye hila, hawataishi nusu ya siku zao. Lakini mimi ninakutumaini wewe.

< תהילים 55 >