< תהילים 51 >

למנצח מזמור לדוד ב בבוא-אליו נתן הנביא-- כאשר-בא אל-בת-שבע ג חנני אלהים כחסדך כרב רחמיך מחה פשעי 1
Unirehemu, Mungu, kwa sababu ya uaminifu wa agano lako; kwa ajili ya wingi wa matendo yako ya rehema, uyafute makosa yangu.
הרבה (הרב) כבסני מעוני ומחטאתי טהרני 2
Unioshe kabisa uovu wangu na unisafishe dhambi zangu.
כי-פשעי אני אדע וחטאתי נגדי תמיד 3
Kwa maana ninayajua makosa yangu, na dhambi yangu iko mbele yako siku zote.
לך לבדך חטאתי והרע בעיניך עשיתי למען תצדק בדברך-- תזכה בשפטך 4
Dhidi yako, wewe pekee, nimetenda dhambi na kufanya uovu mbele ya macho yako; uko sawa usemapo; wewe uko sahahi utoapo hukumu.
הן-בעוון חוללתי ובחטא יחמתני אמי 5
Tazama, nilizaliwa katika uovu; pindi tu mama yangu aliponibeba mimba, nilikuwa katika dhambi. Tazama, wewe unahitaji uaminifu ndani ya moyo wangu;
הן-אמת חפצת בטחות ובסתם חכמה תודיעני 6
katika moyo wangu wewe utanifanya niijue hekima.
תחטאני באזוב ואטהר תכבסני ומשלג אלבין 7
Unisafishe kwa hisopo, nami nitakuwa safi; unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
תשמיעני ששון ושמחה תגלנה עצמות דכית 8
Unifanye kusikia furaha na shangwe ili kwamba mifupa ulioivunja ifurahi.
הסתר פניך מחטאי וכל-עונתי מחה 9
Uufiche uso wako mbali na dhambi zangu na uyafute maovu yangu yote.
לב טהור ברא-לי אלהים ורוח נכון חדש בקרבי 10
Uniumbie moyo safi, Mungu, na uifanye upya roho ya haki ndani yangu.
אל-תשליכני מלפניך ורוח קדשך אל-תקח ממני 11
Usiniondoe uweponi mwako, na usimuondoe roho Mtakatifu ndani yangu.
השיבה לי ששון ישעך ורוח נדיבה תסמכני 12
Unirudishie furaha ya wokovu wako, na unihifadhi mimi kwa roho ya utayari.
אלמדה פשעים דרכיך וחטאים אליך ישובו 13
Ndipo nitawafundisha wakosaji jia zako, na wenye dhambi watakugeukia wewe.
הצילני מדמים אלהים-- אלהי תשועתי תרנן לשוני צדקתך 14
Unisamehe kwa ajili ya umwagaji damu, Mungu wa wokovu wangu, nami nitapiga kelele za shangwe ya haki yako.
אדני שפתי תפתח ופי יגיד תהלתך 15
Ee Bwana, uifungue midomo yangu, na mdomo wangu itazieleza sifa zako.
כי לא-תחפץ זבח ואתנה עולה לא תרצה 16
Kwa maana wewe haufurahishwi katika sadaka, vinginevyo ningekutolea sadaka; wewe hauwi radhi katika sadaka ya kuteketezwa.
זבחי אלהים רוח נשברה לב-נשבר ונדכה-- אלהים לא תבזה 17
Sadaka ya Mungu ni roho iliyovunjika. Wewe, Mungu hautadharau moyo uliopondeka na kujutia.
היטיבה ברצונך את-ציון תבנה חומות ירושלם 18
Uitendee mema Sayuni katika nia yako nzuri; uzijenge tena kuta za Yerusalem.
אז תחפץ זבחי-צדק עולה וכליל אז יעלו על-מזבחך פרים 19
Kisha wewe utafurahia sadaka yenye haki, katika sadaka za kuteketeza; ndipo watu wetu watatoa ng'ombe kwenye madhabahu yako.

< תהילים 51 >