< תהילים 51 >
למנצח מזמור לדוד ב בבוא-אליו נתן הנביא-- כאשר-בא אל-בת-שבע ג חנני אלהים כחסדך כרב רחמיך מחה פשעי | 1 |
Unirehemu, Mungu, kwa sababu ya uaminifu wa agano lako; kwa ajili ya wingi wa matendo yako ya rehema, uyafute makosa yangu.
הרבה (הרב) כבסני מעוני ומחטאתי טהרני | 2 |
Unioshe kabisa uovu wangu na unisafishe dhambi zangu.
כי-פשעי אני אדע וחטאתי נגדי תמיד | 3 |
Kwa maana ninayajua makosa yangu, na dhambi yangu iko mbele yako siku zote.
לך לבדך חטאתי והרע בעיניך עשיתי למען תצדק בדברך-- תזכה בשפטך | 4 |
Dhidi yako, wewe pekee, nimetenda dhambi na kufanya uovu mbele ya macho yako; uko sawa usemapo; wewe uko sahahi utoapo hukumu.
הן-בעוון חוללתי ובחטא יחמתני אמי | 5 |
Tazama, nilizaliwa katika uovu; pindi tu mama yangu aliponibeba mimba, nilikuwa katika dhambi. Tazama, wewe unahitaji uaminifu ndani ya moyo wangu;
הן-אמת חפצת בטחות ובסתם חכמה תודיעני | 6 |
katika moyo wangu wewe utanifanya niijue hekima.
תחטאני באזוב ואטהר תכבסני ומשלג אלבין | 7 |
Unisafishe kwa hisopo, nami nitakuwa safi; unioshe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.
תשמיעני ששון ושמחה תגלנה עצמות דכית | 8 |
Unifanye kusikia furaha na shangwe ili kwamba mifupa ulioivunja ifurahi.
הסתר פניך מחטאי וכל-עונתי מחה | 9 |
Uufiche uso wako mbali na dhambi zangu na uyafute maovu yangu yote.
לב טהור ברא-לי אלהים ורוח נכון חדש בקרבי | 10 |
Uniumbie moyo safi, Mungu, na uifanye upya roho ya haki ndani yangu.
אל-תשליכני מלפניך ורוח קדשך אל-תקח ממני | 11 |
Usiniondoe uweponi mwako, na usimuondoe roho Mtakatifu ndani yangu.
השיבה לי ששון ישעך ורוח נדיבה תסמכני | 12 |
Unirudishie furaha ya wokovu wako, na unihifadhi mimi kwa roho ya utayari.
אלמדה פשעים דרכיך וחטאים אליך ישובו | 13 |
Ndipo nitawafundisha wakosaji jia zako, na wenye dhambi watakugeukia wewe.
הצילני מדמים אלהים-- אלהי תשועתי תרנן לשוני צדקתך | 14 |
Unisamehe kwa ajili ya umwagaji damu, Mungu wa wokovu wangu, nami nitapiga kelele za shangwe ya haki yako.
אדני שפתי תפתח ופי יגיד תהלתך | 15 |
Ee Bwana, uifungue midomo yangu, na mdomo wangu itazieleza sifa zako.
כי לא-תחפץ זבח ואתנה עולה לא תרצה | 16 |
Kwa maana wewe haufurahishwi katika sadaka, vinginevyo ningekutolea sadaka; wewe hauwi radhi katika sadaka ya kuteketezwa.
זבחי אלהים רוח נשברה לב-נשבר ונדכה-- אלהים לא תבזה | 17 |
Sadaka ya Mungu ni roho iliyovunjika. Wewe, Mungu hautadharau moyo uliopondeka na kujutia.
היטיבה ברצונך את-ציון תבנה חומות ירושלם | 18 |
Uitendee mema Sayuni katika nia yako nzuri; uzijenge tena kuta za Yerusalem.
אז תחפץ זבחי-צדק עולה וכליל אז יעלו על-מזבחך פרים | 19 |
Kisha wewe utafurahia sadaka yenye haki, katika sadaka za kuteketeza; ndipo watu wetu watatoa ng'ombe kwenye madhabahu yako.