< תהילים 49 >

למנצח לבני-קרח מזמור ב שמעו-זאת כל-העמים האזינו כל-ישבי חלד 1
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Sikieni haya, enyi mataifa yote, sikilizeni, ninyi wote mkaao dunia hii.
גם-בני אדם גם-בני-איש-- יחד עשיר ואביון 2
Wakubwa kwa wadogo, matajiri na maskini pamoja:
פי ידבר חכמות והגות לבי תבונות 3
Kinywa changu kitasema maneno ya hekima, usemi wa moyo wangu utatoa ufahamu.
אטה למשל אזני אפתח בכנור חידתי 4
Nitatega sikio langu nisikilize mithali, nitafafanua kitendawili kwa zeze:
למה אירא בימי רע-- עון עקבי יסובני 5
Kwa nini niogope siku mbaya zinapokuja, wakati wadanganyifu waovu wanaponizunguka,
הבטחים על-חילם וברב עשרם יתהללו 6
wale wanaotegemea mali zao na kujivunia utajiri wao mwingi?
אח--לא פדה יפדה איש לא-יתן לאלהים כפרו 7
Hakuna mwanadamu awaye yote awezaye kuukomboa uhai wa mwingine, au kumpa Mungu fidia kwa ajili yake.
ויקר פדיון נפשם וחדל לעולם 8
Fidia ya uhai ni gharama kubwa, hakuna malipo yoyote yanayotosha,
ויחי-עוד לנצח לא יראה השחת 9
ili kwamba aishi milele na asione uharibifu.
כי יראה חכמים ימותו-- יחד כסיל ובער יאבדו ועזבו לאחרים חילם 10
Wote wanaona kwamba watu wenye hekima hufa; wajinga na wapumbavu vivyo hivyo huangamia na kuwaachia wengine mali zao.
קרבם בתימו לעולם-- משכנתם לדור ודר קראו בשמותם עלי אדמות 11
Makaburi yao yatabaki kuwa nyumba zao za milele, makao yao vizazi vyote; ingawa walikuwa na mashamba na kuyaita kwa majina yao.
ואדם ביקר בל-ילין נמשל כבהמות נדמו 12
Lakini mwanadamu, licha ya utajiri wake, hadumu; anafanana na mnyama aangamiaye.
זה דרכם כסל למו ואחריהם בפיהם ירצו סלה 13
Hii ndiyo hatima ya wale wanaojitumainia wenyewe, pia ya wafuasi wao, waliothibitisha misemo yao.
כצאן לשאול שתו-- מות ירעם וירדו בם ישרים לבקר--וצירם (וצורם) לבלות שאול מזבל לו (Sheol h7585) 14
Kama kondoo, wamewekewa kwenda kaburini, nacho kifo kitawala. Wanyofu watawatawala asubuhi, maumbile yao yataozea kaburini, mbali na majumba yao makubwa ya fahari. (Sheol h7585)
אך-אלהים--יפדה נפשי מיד-שאול כי יקחני סלה (Sheol h7585) 15
Lakini Mungu atakomboa uhai wangu na kaburi, hakika atanichukua kwake. (Sheol h7585)
אל-תירא כי-יעשר איש כי-ירבה כבוד ביתו 16
Usitishwe mtu anapotajirika, fahari ya nyumba yake inapoongezeka,
כי לא במותו יקח הכל לא-ירד אחריו כבודו 17
kwa maana hatachukua chochote atakapokufa, fahari yake haitashuka pamoja naye.
כי-נפשו בחייו יברך ויודך כי-תיטיב לך 18
Ingawa alipokuwa akiishi alijihesabu kuwa heri, na wanadamu wanakusifu unapofanikiwa,
תבוא עד-דור אבותיו עד-נצח לא יראו-אור 19
atajiunga na kizazi cha baba zake, ambao hawataona kamwe nuru ya uzima.
אדם ביקר ולא יבין נמשל כבהמות נדמו 20
Mwanadamu mwenye utajiri bila ufahamu ni kama wanyama waangamiao.

< תהילים 49 >