< תהילים 49 >
למנצח לבני-קרח מזמור ב שמעו-זאת כל-העמים האזינו כל-ישבי חלד | 1 |
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Sikieni haya, enyi mataifa yote, sikilizeni, ninyi wote mkaao dunia hii.
גם-בני אדם גם-בני-איש-- יחד עשיר ואביון | 2 |
Wakubwa kwa wadogo, matajiri na maskini pamoja:
פי ידבר חכמות והגות לבי תבונות | 3 |
Kinywa changu kitasema maneno ya hekima, usemi wa moyo wangu utatoa ufahamu.
אטה למשל אזני אפתח בכנור חידתי | 4 |
Nitatega sikio langu nisikilize mithali, nitafafanua kitendawili kwa zeze:
למה אירא בימי רע-- עון עקבי יסובני | 5 |
Kwa nini niogope siku mbaya zinapokuja, wakati wadanganyifu waovu wanaponizunguka,
הבטחים על-חילם וברב עשרם יתהללו | 6 |
wale wanaotegemea mali zao na kujivunia utajiri wao mwingi?
אח--לא פדה יפדה איש לא-יתן לאלהים כפרו | 7 |
Hakuna mwanadamu awaye yote awezaye kuukomboa uhai wa mwingine, au kumpa Mungu fidia kwa ajili yake.
ויקר פדיון נפשם וחדל לעולם | 8 |
Fidia ya uhai ni gharama kubwa, hakuna malipo yoyote yanayotosha,
ויחי-עוד לנצח לא יראה השחת | 9 |
ili kwamba aishi milele na asione uharibifu.
כי יראה חכמים ימותו-- יחד כסיל ובער יאבדו ועזבו לאחרים חילם | 10 |
Wote wanaona kwamba watu wenye hekima hufa; wajinga na wapumbavu vivyo hivyo huangamia na kuwaachia wengine mali zao.
קרבם בתימו לעולם-- משכנתם לדור ודר קראו בשמותם עלי אדמות | 11 |
Makaburi yao yatabaki kuwa nyumba zao za milele, makao yao vizazi vyote; ingawa walikuwa na mashamba na kuyaita kwa majina yao.
ואדם ביקר בל-ילין נמשל כבהמות נדמו | 12 |
Lakini mwanadamu, licha ya utajiri wake, hadumu; anafanana na mnyama aangamiaye.
זה דרכם כסל למו ואחריהם בפיהם ירצו סלה | 13 |
Hii ndiyo hatima ya wale wanaojitumainia wenyewe, pia ya wafuasi wao, waliothibitisha misemo yao.
כצאן לשאול שתו-- מות ירעם וירדו בם ישרים לבקר--וצירם (וצורם) לבלות שאול מזבל לו (Sheol ) | 14 |
Kama kondoo, wamewekewa kwenda kaburini, nacho kifo kitawala. Wanyofu watawatawala asubuhi, maumbile yao yataozea kaburini, mbali na majumba yao makubwa ya fahari. (Sheol )
אך-אלהים--יפדה נפשי מיד-שאול כי יקחני סלה (Sheol ) | 15 |
Lakini Mungu atakomboa uhai wangu na kaburi, hakika atanichukua kwake. (Sheol )
אל-תירא כי-יעשר איש כי-ירבה כבוד ביתו | 16 |
Usitishwe mtu anapotajirika, fahari ya nyumba yake inapoongezeka,
כי לא במותו יקח הכל לא-ירד אחריו כבודו | 17 |
kwa maana hatachukua chochote atakapokufa, fahari yake haitashuka pamoja naye.
כי-נפשו בחייו יברך ויודך כי-תיטיב לך | 18 |
Ingawa alipokuwa akiishi alijihesabu kuwa heri, na wanadamu wanakusifu unapofanikiwa,
תבוא עד-דור אבותיו עד-נצח לא יראו-אור | 19 |
atajiunga na kizazi cha baba zake, ambao hawataona kamwe nuru ya uzima.
אדם ביקר ולא יבין נמשל כבהמות נדמו | 20 |
Mwanadamu mwenye utajiri bila ufahamu ni kama wanyama waangamiao.