< תהילים 46 >

למנצח לבני-קרח-- על-עלמות שיר ב אלהים לנו מחסה ועז עזרה בצרות נמצא מאד 1
Mungu kwetu ni kimbilio la usalama na nguvu, upatikanao tele wakati wa mateso.
על-כן לא-נירא בהמיר ארץ ובמוט הרים בלב ימים 2
Hivyo hatutaogopa, hata kama dunia italazimika kubadilika, hata kama milima italazimika kutetemeka na kuangukia kwenye mtima wa bahari, hata kama maji yatavuma kwa kishindo kikuu,
יהמו יחמרו מימיו ירעשו הרים בגאותו סלה 3
hata kama milima itatetemeka kwa vurugu ya maji. (Selah)
נהר--פלגיו ישמחו עיר-אלהים קדש משכני עליון 4
Kuna mto, mikondo yake huufanya mji wa Mungu kufurahi, mahali patakatifu pa hema ya Aliye Juu.
אלהים בקרבה בל-תמוט יעזרה אלהים לפנות בקר 5
Mungu yuko katikati yake; naye hatasogezwa; Mungu atamsaidia, naye atafanya hivyo asubuhi na mapema.
המו גוים מטו ממלכות נתן בקולו תמוג ארץ 6
Mataifa yalikasirika na falme zikataharuki; yeye alipaza sauti yake, na nchi ikayeyuka.
יהוה צבאות עמנו משגב-לנו אלהי יעקב סלה 7
Yahwe wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. (Selah)
לכו-חזו מפעלות יהוה-- אשר-שם שמות בארץ 8
Njoni, mtazame matendo ya Yahwe, uharibifu alioufanya juu ya nchi.
משבית מלחמות עד-קצה הארץ קשת ישבר וקצץ חנית עגלות ישרף באש 9
Anaisitisha vita kwenye nchi; yeye anauvunja upinde na kuikata vipande vipande mishale; anazichoma ngao.
הרפו ודעו כי-אנכי אלהים ארום בגוים ארום בארץ 10
Mkae kimya na mjue kuwa mimi ni Mungu; nitainuliwa juu ya nchi.
יהוה צבאות עמנו משגב-לנו אלהי יעקב סלה 11
Mungu wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. Serah

< תהילים 46 >