< תהילים 46 >
למנצח לבני-קרח-- על-עלמות שיר ב אלהים לנו מחסה ועז עזרה בצרות נמצא מאד | 1 |
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya wana wa Kora. Mtindo wa alamothi. Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu, msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.
על-כן לא-נירא בהמיר ארץ ובמוט הרים בלב ימים | 2 |
Kwa hiyo hatutaogopa, hata kama dunia ikiondolewa nayo milima ikiangukia moyoni mwa bahari.
יהמו יחמרו מימיו ירעשו הרים בגאותו סלה | 3 |
Hata kama maji yake yatanguruma na kuumuka, milima nayo ikitetemeka kwa mawimbi yake.
נהר--פלגיו ישמחו עיר-אלהים קדש משכני עליון | 4 |
Kuna mto ambao vijito vyake vinaufurahisha mji wa Mungu, mahali patakatifu ambako Aliye Juu Sana anaishi.
אלהים בקרבה בל-תמוט יעזרה אלהים לפנות בקר | 5 |
Mungu yuko katikati yake, hautaanguka, Mungu atausaidia asubuhi na mapema.
המו גוים מטו ממלכות נתן בקולו תמוג ארץ | 6 |
Mataifa yanafanya ghasia, falme zinaanguka, Yeye huinua sauti yake, dunia ikayeyuka.
יהוה צבאות עמנו משגב-לנו אלהי יעקב סלה | 7 |
Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi, Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.
לכו-חזו מפעלות יהוה-- אשר-שם שמות בארץ | 8 |
Njooni mkaone kazi za Bwana jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.
משבית מלחמות עד-קצה הארץ קשת ישבר וקצץ חנית עגלות ישרף באש | 9 |
Anakomesha vita hata miisho ya dunia, anakata upinde na kuvunjavunja mkuki, anateketeza ngao kwa moto.
הרפו ודעו כי-אנכי אלהים ארום בגוים ארום בארץ | 10 |
“Tulieni, mjue ya kwamba mimi ndimi Mungu; nitatukuzwa katikati ya mataifa, nitatukuzwa katika dunia.”
יהוה צבאות עמנו משגב-לנו אלהי יעקב סלה | 11 |
Bwana Mwenye Nguvu Zote yu pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.