< תהילים 37 >
לדוד אל-תתחר במרעים אל-תקנא בעשי עולה | 1 |
Usikereshwe na wafanyao maovu; usiwaonee wivu wale watendao yasiyo haki.
כי כחציר מהרה ימלו וכירק דשא יבולון | 2 |
Kwa kuwa muda mfupi watakauka kama nyasi na kukauka kama vile mimea ya kijani ikaukavyo wakati wa kiangazi.
בטח ביהוה ועשה-טוב שכן-ארץ ורעה אמונה | 3 |
Uwamini Mungu na kufanya yaliyo mema; uishi katika nchi na uongezeke katika imani.
והתענג על-יהוה ויתן-לך משאלת לבך | 4 |
Kisha ufurahi mwenyewe katika Yahwe, naye atakupa matamanio ya moyo wako.
גול על-יהוה דרכך ובטח עליו והוא יעשה | 5 |
Umkabidhi njia zako Yahwe; uamini katika yeye, naye atatenda kwa niaba yako.
והוציא כאור צדקך ומשפטך כצהרים | 6 |
Yeye ataidhihilisha haki yako kama mchana na usafi wako kama mwangaza wa mchana.
דום ליהוה-- והתחולל-לו אל-תתחר במצליח דרכו באיש עשה מזמות | 7 |
Uwe kumya mbele za Yahwe na umsubiri yeye kwa uvumilivu. Usikasirike ikiwa kuna mtu anafanikiwa kwa kile afanyacho, au afanyapo njama za uovu.
הרף מאף ועזב חמה אל-תתחר אך-להרע | 8 |
Usikasilile na kugadhabika. Usiogope. Hii huleta matatizo tu.
כי-מרעים יכרתון וקוי יהוה המה יירשו-ארץ | 9 |
Watendao maovu watafutiliwa mbali, bali wale wamngojao Yahwe watairithi nchi.
ועוד מעט ואין רשע והתבוננת על-מקומו ואיננו | 10 |
Katika muda mfupi mtu mwovu atatoweka; wewe utatazama mahali pake, wala hautamuona.
וענוים יירשו-ארץ והתענגו על-רב שלום | 11 |
Lakini wapole watairithi nchi nao watafurahia katika mafanikio makubwa.
זמם רשע לצדיק וחרק עליו שניו | 12 |
Mtu mwovu hupanga njama kinyume na mwenye haki na kumsagia meno.
אדני ישחק-לו כי-ראה כי-יבא יומו | 13 |
Bwana humcheka, kwa maana anaona siku yake inakuja.
חרב פתחו רשעים-- ודרכו קשתם להפיל עני ואביון לטבוח ישרי-דרך | 14 |
Waovu wametoa nje panga zao na wametayarisha pinde zao ili kuwaangamiza wanyonge na wahitaji, na kuwaua wenye haki.
חרבם תבוא בלבם וקשתותם תשברנה | 15 |
Panga zao zitawaua wenyewe, na pinde zao zitavunjika.
טוב-מעט לצדיק-- מהמון רשעים רבים | 16 |
Ni bora kuwa mwenye haki maskini kuliko tajiri mwenye mali nyingi.
כי זרועות רשעים תשברנה וסומך צדיקים יהוה | 17 |
Kwa maana mikono ya watu waovu itavunjika, bali Yahwe huwasaidia watu wenye haki.
יודע יהוה ימי תמימם ונחלתם לעולם תהיה | 18 |
Yahwe huwalinda watu wasio na lawama siku hadi siku, na urithi wao utakuwa wa milele.
לא-יבשו בעת רעה ובימי רעבון ישבעו | 19 |
Hawata aibika siku mbaya zijapo. Wakati wa njaa ufikapo wao watakuwa na chakula cha kutosha.
כי רשעים יאבדו ואיבי יהוה כיקר כרים כלו בעשן כלו | 20 |
Bali waovu wataangamia. Maadui wa Yahwe watakuwa kama vile utukufu wa malisho; watamalizwa na kupotezwa katika moshi.
לוה רשע ולא ישלם וצדיק חונן ונותן | 21 |
Mtu mwovu hukopa lakini halipi, bali mtu mwenye haki ni mkarimu na hutoa.
כי מברכיו יירשו ארץ ומקלליו יכרתו | 22 |
Wale walio barikiwa na Mungu watairithi nchi; wale aliowalaani watafutiliwa mbali.
מיהוה מצעדי-גבר כוננו ודרכו יחפץ | 23 |
Hatua za mwanadamu zinaimarishwa na Yahwe, mtu ambaye njia zake zinakubalika machoni pa Mungu.
כי-יפל לא-יוטל כי-יהוה סומך ידו | 24 |
Ajapojikwaa, hataanguka chini, kwa kuwa Yahwe anamshikilia kwa mkono wake.
נער הייתי-- גם-זקנתי ולא-ראיתי צדיק נעזב וזרעו מבקש-לחם | 25 |
Nilikuwa kijana na sasa ni mzee; sijawahi kumuona mtu mwenye haki ametelekezwa wala watoto wake kuombaomba mkate.
כל-היום חונן ומלוה וזרעו לברכה | 26 |
Wakati wote yeye ni mkarimu na hukopesha, nao watoto wake hufanyika baraka.
סור מרע ועשה-טוב ושכן לעולם | 27 |
Acha uovu na ufanye yaliyo mema; ndipo utakapokuwa salama milele.
כי יהוה אהב משפט ולא-יעזב את-חסידיו לעולם נשמרו וזרע רשעים נכרת | 28 |
Kwa maana Yahwe hupenda haki naye hawaachi wafuasi waaminifu. Wao hutunzwa milele, lakini uzao wa waovu utafutiliwa mabli.
צדיקים יירשו-ארץ וישכנו לעד עליה | 29 |
Wenye haki watairithi nchi na kuaa huko milele.
פי-צדיק יהגה חכמה ולשונו תדבר משפט | 30 |
Mdomo wa mwenye haki huongea hekima na huongeza haki.
תורת אלהיו בלבו לא תמעד אשריו | 31 |
Sheria ya Mungu wake imo moyoni mwake; miguu yake haitelezi.
צופה רשע לצדיק ומבקש להמיתו | 32 |
Mtu mwovu humvizia mwenye haki na kutafuta kumuua.
יהוה לא-יעזבנו בידו ולא ירשיענו בהשפטו | 33 |
Yahwe hatamuacha yeye kwenye mkono wa mtu mwovu wala kumlaumu atakapohukumiwa.
קוה אל-יהוה ושמר דרכו וירוממך לרשת ארץ בהכרת רשעים תראה | 34 |
Umngoje Yahwe na uishike njia yake, naye atakuinua uimiliki nchi. Atakapo waondosha waovu wewe utaona.
ראיתי רשע עריץ ומתערה כאזרח רענן | 35 |
Nimewaona waovu na mtu wa kutisha akienea kama mti wa kijani katika udongo wa asili.
ויעבר והנה איננו ואבקשהו ולא נמצא | 36 |
Lakini nilipopita tana mara nyingine, hakuwepo pale. nilimtafuta, lakini sikumpata.
שמר-תם וראה ישר כי-אחרית לאיש שלום | 37 |
Uwachunguze watu waadilifu, na uwatambue wenye haki; kuna hatima nzuri kwa ajili ya mtu wa amani.
ופשעים נשמדו יחדו אחרית רשעים נכרתה | 38 |
Mwenye dhambi wataharibiwa kabisa; hatima ya mtu mwovu ni kuondoshwa.
ותשועת צדיקים מיהוה מעוזם בעת צרה | 39 |
Wokovu wa haki unatoka kwa Yahwe; yeye huwalinda wao nyakati za shida.
ויעזרם יהוה ויפלטם יפלטם מרשעים ויושיעם--כי-חסו בו | 40 |
Yahwe huwasaidia na kuwaokoa. Yeye huwaokoa dhidi ya watu waovu na kuwanusuru wao kwa sababu wao wamemkimbilia yeye kwa ajili ya usalama.