< תהילים 147 >
הללו-יה כי-טוב זמרה אלהינו-- כי-נעים נאוה תהלה | 1 |
Msifuni Bwana. Tazama jinsi ilivyo vyema kumwimbia Mungu wetu sifa, jinsi inavyopendeza na kustahili kumsifu yeye!
בונה ירושלם יהוה נדחי ישראל יכנס | 2 |
Bwana hujenga Yerusalemu, huwakusanya Israeli walio uhamishoni.
הרפא לשבורי לב ומחבש לעצבותם | 3 |
Anawaponya waliovunjika mioyo na kuvifunga vidonda vyao.
מונה מספר לכוכבים לכלם שמות יקרא | 4 |
Huzihesabu nyota na huipa kila moja jina lake.
גדול אדונינו ורב-כח לתבונתו אין מספר | 5 |
Bwana wetu ni mkuu na mwenye uwezo mwingi, ufahamu wake hauna kikomo.
מעודד ענוים יהוה משפיל רשעים עדי-ארץ | 6 |
Bwana huwahifadhi wanyenyekevu lakini huwashusha waovu mpaka mavumbini.
ענו ליהוה בתודה זמרו לאלהינו בכנור | 7 |
Mwimbieni Bwana kwa shukrani, mpigieni Mungu wetu kinubi.
המכסה שמים בעבים-- המכין לארץ מטר המצמיח הרים חציר | 8 |
Yeye huzifunika anga kwa mawingu, huinyeshea ardhi mvua, na kuzifanya nyasi kuota juu ya vilima.
נותן לבהמה לחמה לבני ערב אשר יקראו | 9 |
Huwapa chakula mifugo na pia makinda ya kunguru yanapolia.
לא בגבורת הסוס יחפץ לא-בשוקי האיש ירצה | 10 |
Furaha yake haipo katika nguvu za farasi, wala furaha yake kwenye miguu ya mwanadamu.
רוצה יהוה את-יראיו-- את-המיחלים לחסדו | 11 |
Bwana hupendezwa na wale wamchao, wale wanaoweka tumaini lao katika upendo wake usiokoma.
שבחי ירושלם את-יהוה הללי אלהיך ציון | 12 |
Mtukuze Bwana, ee Yerusalemu, msifu Mungu wako, ee Sayuni,
כי-חזק בריחי שעריך ברך בניך בקרבך | 13 |
kwa maana huimarisha makomeo ya malango yako na huwabariki watu wako walio ndani yako.
השם-גבולך שלום חלב חטים ישביעך | 14 |
Huwapa amani mipakani mwenu na kukushibisha kwa ngano safi kabisa.
השלח אמרתו ארץ עד-מהרה ירוץ דברו | 15 |
Hutuma amri yake duniani, neno lake hukimbia kasi.
הנתן שלג כצמר כפור כאפר יפזר | 16 |
Anatandaza theluji kama sufu na kutawanya umande kama majivu.
משליך קרחו כפתים לפני קרתו מי יעמד | 17 |
Huvurumisha mvua yake ya mawe kama changarawe. Ni nani awezaye kustahimili ukali wa baridi yake?
ישלח דברו וימסם ישב רוחו יזלו-מים | 18 |
Hutuma neno lake na kuviyeyusha, huvumisha upepo wake, nayo maji hutiririka.
מגיד דברו ליעקב חקיו ומשפטיו לישראל | 19 |
Amemfunulia Yakobo neno lake, sheria zake na maagizo yake kwa Israeli.
לא עשה כן לכל-גוי-- ומשפטים בל-ידעום הללו-יה | 20 |
Hajafanya hivyo kwa taifa lingine lolote, hawazijui sheria zake. Msifuni Bwana.