< תהילים 144 >

לדוד ברוך יהוה צורי-- המלמד ידי לקרב אצבעותי למלחמה 1
Atukuzwe Yahwe, mwamba wangu, anifundishaye mikono yangu vita na vidole vyangu kupigana.
חסדי ומצודתי משגבי ומפלטי-לי מגני ובו חסיתי הרודד עמי תחתי 2
Wewe ni uaminifu wa agano langu na ngome yangu, mnara wangu mrefu na uniokoaye, ngao yangu na yule ambaye katika yeye napata kimbilio, uyatiishaye mataifa chini yangu.
יהוה--מה-אדם ותדעהו בן-אנוש ותחשבהו 3
Ee Yahwe, mtu ni kitu gani hata umtazame au mwana wa mtu hata umfikirie?
אדם להבל דמה ימיו כצל עובר 4
Mtu ni kama pumzi, siku zake ni kama uvuli upitao.
יהוה הט-שמיך ותרד גע בהרים ויעשנו 5
Ee Yahwe uziinamishe mbingu na ushuke chini, uiguse milima na uifanye kutoa moshi.
ברוק ברק ותפיצם שלח חציך ותהמם 6
Utume umeme uwatawanye adui zangu; upige mishale yako na uwavuruge.
שלח ידיך ממרום פצני והצילני ממים רבים מיד בני נכר 7
Nyosha mkono wako toka juu; uniokoe kutoka katika maji mengi, na kutoka katika mkono wa wageni.
אשר פיהם דבר-שוא וימינם ימין שקר 8
vinywa vyao hunena uongo, na mkono wao wa kuume ni mkono wa uongo.
אלהים--שיר חדש אשירה לך בנבל עשור אזמרה-לך 9
Nitakuimbia wimbo mpya, Mungu; kwa kinanda cha nyuzi kumi nitakuimbia sifa wewe,
הנותן תשועה למלכים הפוצה את-דוד עבדו--מחרב רעה 10
uwapaye wafalme wokovu, uliye muokoa Daudi mtumishi wako dhidi ya upanga wa uovu.
פצני והצילני מיד בני-נכר אשר פיהם דבר-שוא וימינם ימין שקר 11
Uniokoe na unitoe mkononi mwa wageni. Midomo yao huongea uongo, na mkono wao wa kuume ni mkono wa uongo.
אשר בנינו כנטעים-- מגדלים בנעוריהם בנותינו כזוית-- מחטבות תבנית היכל 12
Wana wetu na wawe kama mimea ikuayo kwa ukumbwa timilifu katika ujana wao na binti zetu kama nguzo za pembeni, zilizonakishiwa kwa kupamba jumba la kifahari.
מזוינו מלאים-- מפיקים מזן אל-זן צאוננו מאליפות מרבבות-- בחוצותינו 13
Ghala zetu na zijae akiba ya kila aina ya mazao, na kondoo wetu wazae elfu na makumi elfu mashambani mwetu.
אלופינו מסבלים אין-פרץ ואין יוצאת ואין צוחה ברחבתינו 14
Kisha ng'ombe wetu watakuwa na nddama wengi. Hakuna atakayevunja kuta zetu; hakutakuwa na uhamisho wala kilio mitaani mwetu.
אשרי העם שככה לו אשרי העם שיהוה אלהיו 15
Wamebarikiwa watu wenye baraka hizo; furaha ina watu ambao Mungu wao ni Yahwe.

< תהילים 144 >