< תהילים 139 >
למנצח לדוד מזמור יהוה חקרתני ותדע | 1 |
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, umenichunguza na kunijua.
אתה ידעת שבתי וקומי בנתה לרעי מרחוק | 2 |
Unajua ninapoketi na ninapoinuka; unatambua mawazo yangu tokea mbali.
ארחי ורבעי זרית וכל-דרכי הסכנתה | 3 |
Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu; unaelewa njia zangu zote.
כי אין מלה בלשוני הן יהוה ידעת כלה | 4 |
Kabla neno halijafika katika ulimi wangu, wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.
אחור וקדם צרתני ותשת עלי כפכה | 5 |
Umenizunguka nyuma na mbele; umeweka mkono wako juu yangu.
פלאיה (פליאה) דעת ממני נשגבה לא-אוכל לה | 6 |
Maarifa haya ni ya ajabu mno kwangu, ni ya juu sana kwangu kuyafikia.
אנה אלך מרוחך ואנה מפניך אברח | 7 |
Niende wapi nijiepushe na Roho yako? Niende wapi niukimbie uso wako?
אם אסק שמים שם אתה ואציעה שאול הנך (Sheol ) | 8 |
Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko; nikifanya vilindi kuwa kitanda changu, wewe uko huko. (Sheol )
אשא כנפי-שחר אשכנה באחרית ים | 9 |
Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko, kama nikikaa pande za mbali za bahari,
גם-שם ידך תנחני ותאחזני ימינך | 10 |
hata huko mkono wako utaniongoza, mkono wako wa kuume utanishika kwa uthabiti.
ואמר אך-חשך ישופני ולילה אור בעדני | 11 |
Kama nikisema, “Hakika giza litanificha na nuru inayonizunguka iwe usiku,”
גם-חשך לא-יחשיך ממך ולילה כיום יאיר-- כחשיכה כאורה | 12 |
hata giza halitakuwa giza kwako, usiku utangʼaa kama mchana, kwa kuwa giza ni kama nuru kwako.
כי-אתה קנית כליתי תסכני בבטן אמי | 13 |
Kwa maana wewe ndiwe uliyeumba utu wangu wa ndani; uliniunga pamoja tumboni mwa mama yangu.
אודך-- על כי נוראות נפליתי נפלאים מעשיך ונפשי ידעת מאד | 14 |
Ninakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa namna ya ajabu na ya kutisha; kazi zako ni za ajabu, ninajua hayo kikamilifu.
לא-נכחד עצמי ממך אשר-עשיתי בסתר רקמתי בתחתיות ארץ | 15 |
Umbile langu halikufichika kwako, nilipoumbwa mahali pa siri. Nilipoungwa pamoja kwa ustadi katika vilindi vya nchi,
גלמי ראו עיניך ועל-ספרך כלם יכתבו ימים יצרו ולא (ולו) אחד בהם | 16 |
macho yako yaliniona kabla mwili wangu haujakamilika. Siku zangu zote ulizonipangia ziliandikwa katika kitabu chako kabla haijakuwepo hata moja.
ולי--מה-יקרו רעיך אל מה עצמו ראשיהם | 17 |
Tazama jinsi yalivyo ya thamani mawazo yako kwangu, Ee Mungu! Jinsi jumla yake ilivyo kubwa!
אספרם מחול ירבון הקיצתי ועודי עמך | 18 |
Kama ningezihesabu, zingekuwa nyingi kuliko mchanga. Niamkapo, bado niko pamoja nawe.
אם-תקטל אלוה רשע ואנשי דמים סורו מני | 19 |
Laiti ungewachinja waovu, Ee Mungu! Ondokeni kwangu, ninyi wamwaga damu!
אשר ימרוך למזמה נשוא לשוא עריך | 20 |
Wanazungumza juu yako wakiwa na kusudi baya, adui zako wanatumia vibaya jina lako.
הלוא-משנאיך יהוה אשנא ובתקוממיך אתקוטט | 21 |
Ee Bwana, je, nisiwachukie wanaokuchukia? Nisiwachukie sana wanaoinuka dhidi yako?
תכלית שנאה שנאתים לאויבים היו לי | 22 |
Sina kitu zaidi ya chuki dhidi yao, ninawahesabu ni adui zangu.
חקרני אל ודע לבבי בחנני ודע שרעפי | 23 |
Ee Mungu, nichunguze, uujue moyo wangu, nijaribu na ujue mawazo yangu.
וראה אם-דרך-עצב בי ונחני בדרך עולם | 24 |
Uone kama kuna njia iletayo machukizo ndani yangu, uniongoze katika njia ya milele.