< תהילים 132 >
שיר המעלות זכור-יהוה לדוד-- את כל-ענותו | 1 |
Yahwe, kwa ajili ya Daudi kumbuka mateso yake yote.
אשר נשבע ליהוה נדר לאביר יעקב | 2 |
Kumbuka ndiye aliye mwapia Yahwe, aliweka nadhiri kwa Shujaa wa Yakobo.
אם-אבא באהל ביתי אם-אעלה על-ערש יצועי | 3 |
Alisema, sitaingia nyumbani mwangu wala sitaenda kitandani mwangu,
אם אתן שנת לעיני לעפעפי תנומה | 4 |
sitayapa macho yangu usingizi wala kope zangu kupumzika
עד-אמצא מקום ליהוה משכנות לאביר יעקב | 5 |
mpaka nitakapopata mahali kwa ajili ya Yahwe, na maskani kwa ajili ya Shujaa wa Yakobo.”
הנה-שמענוה באפרתה מצאנוה בשדי-יער | 6 |
Tazama tulisikia kuhusu hilo katika Efrata; tuliipata katika konde la Yearimu.
נבואה למשכנותיו נשתחוה להדם רגליו | 7 |
Tutaingia katika maskani ya Mungu; tutasujudu miguuni pake.
קומה יהוה למנוחתך אתה וארון עזך | 8 |
Inuka, Ee Yahwe, uje mahali pako pa kupumzika, wewe na sanduku la nguvu zako!
כהניך ילבשו-צדק וחסידיך ירננו | 9 |
Makuhani wako na wavikwe uadilifu; waaminifu wako washangilie.
בעבור דוד עבדך-- אל-תשב פני משיחך | 10 |
Kwa ajili ya mtumishi wako Daudi, usimuache mfalme wako uliye mpaka mafuta.
נשבע-יהוה לדוד אמת-- לא-ישוב ממנה מפרי בטנך-- אשית לכסא-לך | 11 |
Yahwe alimwapia Daudi kiapo cha uhakika, kiapo cha uhakika ambacho hatakivunja: “Nitamuweka mmoja wa wazawa wako kwenye kiti chako cha enzi.
אם-ישמרו בניך בריתי-- ועדתי זו אלמדם גם-בניהם עדי-עד-- ישבו לכסא-לך | 12 |
Kama wana wako watalishika agano langu na sheria ambazo nitawafundisha, watoto wao pia watakaa kwenye kiti chako cha enzi milele.”
כי-בחר יהוה בציון אוה למושב לו | 13 |
Hakika Yahwe ameichagua Sayuni, ameitamani kwa ajili ya makao yake.
זאת-מנוחתי עדי-עד פה-אשב כי אותיה | 14 |
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele. Nitaishi hapa, kwa kuwa ninapatamani.
צידה ברך אברך אביוניה אשביע לחם | 15 |
Nitapabariki sana kwa mahitaji. Nitawatosheleza maskini wake kwa mkate.
וכהניה אלביש ישע וחסידיה רנן ירננו | 16 |
Nitawavisha makuhani wake kwa wokovu, waaminifu wake watashangilia kwa furaha.
שם אצמיח קרן לדוד ערכתי נר למשיחי | 17 |
Hapo nitachipusha pembe kwa ajili ya Daudi na kuweka taa juu kwa ajili ya mpakwa mafuta wangu.
אויביו אלביש בשת ועליו יציץ נזרו | 18 |
Nitawavisha adui kwa aibu, bali juu yake taji yake itang'aa.”