< תהילים 132 >

שיר המעלות זכור-יהוה לדוד-- את כל-ענותו 1
Yahwe, kwa ajili ya Daudi kumbuka mateso yake yote.
אשר נשבע ליהוה נדר לאביר יעקב 2
Kumbuka ndiye aliye mwapia Yahwe, aliweka nadhiri kwa Shujaa wa Yakobo.
אם-אבא באהל ביתי אם-אעלה על-ערש יצועי 3
Alisema, sitaingia nyumbani mwangu wala sitaenda kitandani mwangu,
אם אתן שנת לעיני לעפעפי תנומה 4
sitayapa macho yangu usingizi wala kope zangu kupumzika
עד-אמצא מקום ליהוה משכנות לאביר יעקב 5
mpaka nitakapopata mahali kwa ajili ya Yahwe, na maskani kwa ajili ya Shujaa wa Yakobo.”
הנה-שמענוה באפרתה מצאנוה בשדי-יער 6
Tazama tulisikia kuhusu hilo katika Efrata; tuliipata katika konde la Yearimu.
נבואה למשכנותיו נשתחוה להדם רגליו 7
Tutaingia katika maskani ya Mungu; tutasujudu miguuni pake.
קומה יהוה למנוחתך אתה וארון עזך 8
Inuka, Ee Yahwe, uje mahali pako pa kupumzika, wewe na sanduku la nguvu zako!
כהניך ילבשו-צדק וחסידיך ירננו 9
Makuhani wako na wavikwe uadilifu; waaminifu wako washangilie.
בעבור דוד עבדך-- אל-תשב פני משיחך 10
Kwa ajili ya mtumishi wako Daudi, usimuache mfalme wako uliye mpaka mafuta.
נשבע-יהוה לדוד אמת-- לא-ישוב ממנה מפרי בטנך-- אשית לכסא-לך 11
Yahwe alimwapia Daudi kiapo cha uhakika, kiapo cha uhakika ambacho hatakivunja: “Nitamuweka mmoja wa wazawa wako kwenye kiti chako cha enzi.
אם-ישמרו בניך בריתי-- ועדתי זו אלמדם גם-בניהם עדי-עד-- ישבו לכסא-לך 12
Kama wana wako watalishika agano langu na sheria ambazo nitawafundisha, watoto wao pia watakaa kwenye kiti chako cha enzi milele.”
כי-בחר יהוה בציון אוה למושב לו 13
Hakika Yahwe ameichagua Sayuni, ameitamani kwa ajili ya makao yake.
זאת-מנוחתי עדי-עד פה-אשב כי אותיה 14
“Hapa ni mahali pangu pa kupumzika milele. Nitaishi hapa, kwa kuwa ninapatamani.
צידה ברך אברך אביוניה אשביע לחם 15
Nitapabariki sana kwa mahitaji. Nitawatosheleza maskini wake kwa mkate.
וכהניה אלביש ישע וחסידיה רנן ירננו 16
Nitawavisha makuhani wake kwa wokovu, waaminifu wake watashangilia kwa furaha.
שם אצמיח קרן לדוד ערכתי נר למשיחי 17
Hapo nitachipusha pembe kwa ajili ya Daudi na kuweka taa juu kwa ajili ya mpakwa mafuta wangu.
אויביו אלביש בשת ועליו יציץ נזרו 18
Nitawavisha adui kwa aibu, bali juu yake taji yake itang'aa.”

< תהילים 132 >