< תהילים 120 >
שיר המעלות אל-יהוה בצרתה לי-- קראתי ויענני | 1 |
Katika dhiki yangu nilimuita Yahwe, naye akanijibu.
יהוה--הצילה נפשי משפת-שקר מלשון רמיה | 2 |
Uiokoe nasfi yangu, yahwe, dhidi ya wale wadanganyao kwa midomo yao na wanenao hila kwa ndimi zao.
מה-יתן לך ומה-יסיף לך-- לשון רמיה | 3 |
Yahwe atawaadhibu vipi, na atawafanyia kitu gani zaidi, ninyi mlio na ulimi mdanganyifu?
חצי גבור שנונים עם גחלי רתמים | 4 |
Atawaadhibu kwa mishale ya shujaa iliyo nolewa kwa makaa ya moto ya mretemu.
אויה-לי כי-גרתי משך שכנתי עם-אהלי קדר | 5 |
Ole wangu mimi kwa sababu ninaishi kwa muda Mesheki; huko nyuma niliishi kati ya maskani ya Kedari.
רבת שכנה-לה נפשי-- עם שונא שלום | 6 |
Kwa muda mrefu sana niliisha na wale waichukiao amani.
אני-שלום וכי אדבר המה למלחמה | 7 |
Nipo kwa ajili ya amani, lakini ninenapo, wao wako kwa ajili ya vita.