< תהילים 113 >
הללו-יה הללו עבדי יהוה הללו את-שם יהוה | 1 |
Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.
יהי שם יהוה מברך-- מעתה ועד-עולם | 2 |
Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.
ממזרח-שמש עד-מבואו-- מהלל שם יהוה | 3 |
Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.
רם על-כל-גוים יהוה על השמים כבודו | 4 |
Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.
מי כיהוה אלהינו-- המגביהי לשבת | 5 |
Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,
המשפילי לראות-- בשמים ובארץ | 6 |
ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?
מקימי מעפר דל מאשפת ירים אביון | 7 |
Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,
להושיבי עם-נדיבים עם נדיבי עמו | 8 |
huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
מושיבי עקרת הבית-- אם-הבנים שמחה הללו-יה | 9 |
Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.