< תהילים 112 >
הללו-יה אשרי-איש ירא את-יהוה במצותיו חפץ מאד | 1 |
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
גבור בארץ יהיה זרעו דור ישרים יברך | 2 |
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
הון-ועשר בביתו וצדקתו עמדת לעד | 3 |
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
זרח בחשך אור לישרים חנון ורחום וצדיק | 4 |
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
טוב-איש חונן ומלוה יכלכל דבריו במשפט | 5 |
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
כי-לעולם לא-ימוט לזכר עולם יהיה צדיק | 6 |
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
משמועה רעה לא יירא נכון לבו בטח ביהוה | 7 |
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
סמוך לבו לא יירא עד אשר-יראה בצריו | 8 |
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
פזר נתן לאביונים-- צדקתו עמדת לעד קרנו תרום בכבוד | 9 |
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
רשע יראה וכעס-- שניו יחרק ונמס תאות רשעים תאבד | 10 |
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.