< תהילים 111 >
הללו-יה אודה יהוה בכל-לבב בסוד ישרים ועדה | 1 |
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
גדלים מעשי יהוה דרושים לכל-חפציהם | 2 |
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
הוד-והדר פעלו וצדקתו עמדת לעד | 3 |
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
זכר עשה לנפלאותיו חנון ורחום יהוה | 4 |
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
טרף נתן ליראיו יזכר לעולם בריתו | 5 |
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
כח מעשיו הגיד לעמו-- לתת להם נחלת גוים | 6 |
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
מעשי ידיו אמת ומשפט נאמנים כל-פקודיו | 7 |
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
סמוכים לעד לעולם עשוים באמת וישר | 8 |
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
פדות שלח לעמו-- צוה-לעולם בריתו קדוש ונורא שמו | 9 |
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
ראשית חכמה יראת יהוה-- שכל טוב לכל-עשיהם תהלתו עמדת לעד | 10 |
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.