< תהילים 111 >

הללו-יה אודה יהוה בכל-לבב בסוד ישרים ועדה 1
Msifuni Bwana. Nitamtukuza Bwana kwa moyo wangu wote, katika baraza la wanyofu na katika kusanyiko.
גדלים מעשי יהוה דרושים לכל-חפציהם 2
Kazi za Bwana ni kuu, wote wanaopendezwa nazo huzitafakari.
הוד-והדר פעלו וצדקתו עמדת לעד 3
Kazi zake zimejaa fahari na utukufu, haki yake hudumu daima.
זכר עשה לנפלאותיו חנון ורחום יהוה 4
Amefanya maajabu yake yakumbukwe, Bwana ni mwenye neema na huruma.
טרף נתן ליראיו יזכר לעולם בריתו 5
Huwapa chakula wale wanaomcha, hulikumbuka agano lake milele.
כח מעשיו הגיד לעמו-- לתת להם נחלת גוים 6
Amewaonyesha watu wake uwezo wa kazi zake, akiwapa nchi za mataifa mengine.
מעשי ידיו אמת ומשפט נאמנים כל-פקודיו 7
Kazi za mikono yake ni za uaminifu na haki, mausia yake yote ni ya kuaminika.
סמוכים לעד לעולם עשוים באמת וישר 8
Zinadumu milele na milele, zikifanyika kwa uaminifu na unyofu.
פדות שלח לעמו-- צוה-לעולם בריתו קדוש ונורא שמו 9
Aliwapa watu wake ukombozi, aliamuru agano lake milele: jina lake ni takatifu na la kuogopwa.
ראשית חכמה יראת יהוה-- שכל טוב לכל-עשיהם תהלתו עמדת לעד 10
Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, wote wanaozifuata amri zake wana busara. Sifa zake zadumu milele.

< תהילים 111 >