< תהילים 110 >

לדוד מזמור נאם יהוה לאדני--שב לימיני עד-אשית איביך הדם לרגליך 1
Yahwe humwambia bwana wangu, “Kaa mkono wangu wa kuume mpaka nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”
מטה-עזך--ישלח יהוה מציון רדה בקרב איביך 2
Yahwe atainyosha fimbo ya nguvu yako toka Sayuni; utawale kati ya adui zako.
עמך נדבת ביום חילך בהדרי-קדש מרחם משחר לך טל ילדתיך 3
Siku ile ya uweza wako watu wako watakufuata wakiwa katika mavazi matakatifu ya hiari yao wenyewe; tokea tumbo la alfajiri ujana wako utakuwa kwako kama umande.
נשבע יהוה ולא ינחם-- אתה-כהן לעולם על-דברתי מלכי-צדק 4
Yahwe ameapa, na hatabadilika: “Wewe ni kuhani milele, baada ya namna ya Melkizedeki.”
אדני על-ימינך מחץ ביום-אפו מלכים 5
Bwana yuko mkono wako wa kuume. Siku ile ya hasira yake atawaua wafalme.
ידין בגוים מלא גויות מחץ ראש על-ארץ רבה 6
Yeye atahukumu matifa; ataujaza uwanja wa vita kwa maiti; atawauwa viongozi kaitka nchi nyingi.
מנחל בדרך ישתה על-כן ירים ראש 7
Atakunywa maji ya kijito njiani, kisha baada ya ushindi atainua kichwa chake juu.

< תהילים 110 >