< תהילים 108 >

שיר מזמור לדוד נכון לבי אלהים אשירה ואזמרה אף-כבודי 1
Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
עורה הנבל וכנור אעירה שחר 2
Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
אודך בעמים יהוה ואזמרך בלאמים 3
Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
כי-גדול מעל-שמים חסדך ועד-שחקים אמתך 4
Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
רומה על-שמים אלהים ועל כל-הארץ כבודך 5
Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
למען יחלצון ידידיך הושיעה ימינך וענני 6
Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
אלהים דבר בקדשו--אעלזה אחלקה שכם ועמק סכות אמדד 7
Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
לי גלעד לי מנשה ואפרים מעוז ראשי יהודה מחקקי 8
Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
מואב סיר רחצי--על-אדום אשליך נעלי עלי-פלשת אתרועע 9
Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
מי יבלני עיר מבצר מי נחני עד-אדום 10
Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
הלא-אלהים זנחתנו ולא-תצא אלהים בצבאתינו 11
Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
הבה-לנו עזרת מצר ושוא תשועת אדם 12
Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
באלהים נעשה-חיל והוא יבוס צרינו 13
Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.

< תהילים 108 >