< תהילים 107 >
הדו ליהוה כי-טוב כי לעולם חסדו | 1 |
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
יאמרו גאולי יהוה-- אשר גאלם מיד-צר | 2 |
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
ומארצות קבצם ממזרח וממערב מצפון ומים | 3 |
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
תעו במדבר בישימון דרך עיר מושב לא מצאו | 4 |
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
רעבים גם-צמאים-- נפשם בהם תתעטף | 5 |
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
ויצעקו אל-יהוה בצר להם ממצוקותיהם יצילם | 6 |
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
וידריכם בדרך ישרה-- ללכת אל-עיר מושב | 7 |
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם | 8 |
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
כי-השביע נפש שקקה ונפש רעבה מלא-טוב | 9 |
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
ישבי חשך וצלמות אסירי עני וברזל | 10 |
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
כי-המרו אמרי-אל ועצת עליון נאצו | 11 |
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
ויכנע בעמל לבם כשלו ואין עזר | 12 |
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
ויזעקו אל-יהוה בצר להם ממצקותיהם יושיעם | 13 |
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
יוציאם מחשך וצלמות ומוסרותיהם ינתק | 14 |
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם | 15 |
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
כי-שבר דלתות נחשת ובריחי ברזל גדע | 16 |
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
אולים מדרך פשעם ומעונתיהם יתענו | 17 |
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
כל-אכל תתעב נפשם ויגיעו עד-שערי מות | 18 |
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
ויזעקו אל-יהוה בצר להם ממצקותיהם יושיעם | 19 |
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
ישלח דברו וירפאם וימלט משחיתותם | 20 |
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם | 21 |
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
ויזבחו זבחי תודה ויספרו מעשיו ברנה | 22 |
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
] יורדי הים באניות עשי מלאכה במים רבים | 23 |
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
] המה ראו מעשי יהוה ונפלאותיו במצולה | 24 |
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
] ויאמר--ויעמד רוח סערה ותרומם גליו | 25 |
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
] יעלו שמים ירדו תהומות נפשם ברעה תתמוגג | 26 |
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
] יחוגו וינועו כשכור וכל-חכמתם תתבלע | 27 |
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
] ויצעקו אל-יהוה בצר להם וממצוקתיהם יוציאם | 28 |
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
יקם סערה לדממה ויחשו גליהם | 29 |
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
וישמחו כי-ישתקו וינחם אל-מחוז חפצם | 30 |
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
יודו ליהוה חסדו ונפלאותיו לבני אדם | 31 |
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
וירוממוהו בקהל-עם ובמושב זקנים יהללוהו | 32 |
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
ישם נהרות למדבר ומצאי מים לצמאון | 33 |
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
ארץ פרי למלחה מרעת יושבי בה | 34 |
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
ישם מדבר לאגם-מים וארץ ציה למצאי מים | 35 |
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
ויושב שם רעבים ויכוננו עיר מושב | 36 |
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
ויזרעו שדות ויטעו כרמים ויעשו פרי תבואה | 37 |
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
ויברכם וירבו מאד ובהמתם לא ימעיט | 38 |
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
וימעטו וישחו-- מעצר רעה ויגון | 39 |
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
] שפך בוז על-נדיבים ויתעם בתהו לא-דרך | 40 |
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
וישגב אביון מעוני וישם כצאן משפחות | 41 |
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
יראו ישרים וישמחו וכל-עולה קפצה פיה | 42 |
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
מי-חכם וישמר-אלה ויתבוננו חסדי יהוה | 43 |
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.