< תהילים 106 >

הללו-יה הודו ליהוה כי-טוב-- כי לעולם חסדו 1
Msifuni Bwana. Mshukuruni Bwana, kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
מי--ימלל גבורות יהוה ישמיע כל-תהלתו 2
Ni nani awezaye kusimulia matendo makuu ya Bwana au kutangaza kikamilifu sifa zake?
אשרי שמרי משפט עשה צדקה בכל-עת 3
Heri wale wanaodumisha haki, ambao daima wanafanya yaliyo mema.
זכרני יהוה ברצון עמך פקדני בישועתך 4
Ee Bwana, unikumbuke unapowatendea mema watu wako, uwe msaada wangu unapowaokoa,
לראות בטובת בחיריך-- לשמח בשמחת גויך להתהלל עם-נחלתך 5
ili niweze kufurahia mafanikio ya wateule wako, niweze kushiriki katika furaha ya taifa lako, na kuungana na urithi wako katika kukusifu.
חטאנו עם-אבותינו העוינו הרשענו 6
Tumetenda dhambi, kama vile baba zetu walivyotenda, tumekosa na tumetenda uovu.
אבותינו במצרים לא-השכילו נפלאותיך-- לא זכרו את-רב חסדיך וימרו על-ים בים-סוף 7
Wakati baba zetu walipokuwa Misri, hawakuzingatia maajabu yako, wala hawakukumbuka wingi wa fadhili zako, bali waliasi kando ya bahari, Bahari ya Shamu.
ויושיעם למען שמו-- להודיע את-גבורתו 8
Hata hivyo aliwaokoa kwa ajili ya jina lake, ili apate kudhihirisha uweza wake mkuu.
ויגער בים-סוף ויחרב ויוליכם בתהמות כמדבר 9
Alikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka, akawaongoza katika vilindi vyake kama vile jangwani.
ויושיעם מיד שונא ויגאלם מיד אויב 10
Aliwaokoa mikononi mwa adui; kutoka mikononi mwa adui aliwakomboa.
ויכסו-מים צריהם אחד מהם לא נותר 11
Maji yaliwafunika adui zao, hakunusurika hata mmoja.
ויאמינו בדבריו ישירו תהלתו 12
Ndipo walipoamini ahadi zake, nao wakaimba sifa zake.
מהרו שכחו מעשיו לא-חכו לעצתו 13
Lakini mara walisahau aliyowatendea, wala hawakungojea shauri lake.
ויתאוו תאוה במדבר וינסו-אל בישימון 14
Jangwani walitawaliwa na tamaa zao, walimjaribu Mungu nyikani.
ויתן להם שאלתם וישלח רזון בנפשם 15
Kwa hiyo aliwapa kile walichoomba, lakini akatuma juu yao ugonjwa wa kudhoofisha.
ויקנאו למשה במחנה לאהרן קדוש יהוה 16
Kambini walimwonea wivu Mose, na pia Aroni aliyekuwa amewekwa wakfu kwa Bwana.
תפתח-ארץ ותבלע דתן ותכס על-עדת אבירם 17
Ardhi ilifunguka ikawameza Dathani, ikawazika Abiramu na kundi lake.
ותבער-אש בעדתם להבה תלהט רשעים 18
Moto uliwaka katikati ya wafuasi wao, mwali wa moto uliwateketeza waovu.
יעשו-עגל בחרב וישתחוו למסכה 19
Huko Horebu walitengeneza ndama, na kuabudu sanamu ya kusubu kwa chuma.
וימירו את-כבודם בתבנית שור אכל עשב 20
Waliubadilisha Utukufu wao kwa sanamu ya fahali, ambaye hula majani.
שכחו אל מושיעם-- עשה גדלות במצרים 21
Walimsahau Mungu aliyewaokoa, aliyekuwa ametenda mambo makuu huko Misri,
נפלאות בארץ חם נוראות על-ים-סוף 22
miujiza katika nchi ya Hamu na mambo ya kutisha huko Bahari ya Shamu.
ויאמר להשמידם לולי משה בחירו-- עמד בפרץ לפניו להשיב חמתו מהשחית 23
Kwa hiyo alisema kwamba angewaangamiza: kama Mose mteule wake, asingesimama kati yao na Mungu kuizuia ghadhabu yake kuwaangamiza.
וימאסו בארץ חמדה לא-האמינו לדברו 24
Kisha waliidharau ile nchi nzuri, hawakuiamini ahadi yake.
וירגנו באהליהם לא שמעו בקול יהוה 25
Walinungʼunika ndani ya mahema yao, wala hawakumtii Bwana.
וישא ידו להם-- להפיל אותם במדבר 26
Kwa hiyo akaapa kwa mkono ulioinuliwa kwamba atawafanya waanguke jangwani,
ולהפיל זרעם בגוים ולזרותם בארצות 27
kuwatawanya wazao wao waanguke miongoni mwa mataifa, na kuwatawanya katika nchi zote.
ויצמדו לבעל פעור ויאכלו זבחי מתים 28
Walijifunga nira na Baali wa Peori, wakala dhabihu zilizotolewa kwa miungu isiyo na uhai.
ויכעיסו במעלליהם ותפרץ-בם מגפה 29
Waliichochea hasira ya Bwana, wakamkasirisha kwa matendo yao maovu, nayo tauni ikazuka katikati yao.
ויעמד פינחס ויפלל ותעצר המגפה 30
Lakini Finehasi alisimama na kuingilia kati, nayo tauni ikazuiliwa.
ותחשב לו לצדקה לדר ודר עד-עולם 31
Hili likahesabiwa kwake haki, kwa vizazi visivyo na mwisho vijavyo.
ויקציפו על-מי מריבה וירע למשה בעבורם 32
Kwenye maji ya Meriba, walimkasirisha Bwana, janga likampata Mose kwa sababu yao;
כי-המרו את-רוחו ויבטא בשפתיו 33
kwa maana walimwasi Roho wa Mungu, na maneno yasiyofaa yakatoka midomoni kwa Mose.
לא-השמידו את-העמים-- אשר אמר יהוה להם 34
Hawakuyaangamiza yale mataifa kama Bwana alivyowaagiza,
ויתערבו בגוים וילמדו מעשיהם 35
bali walijichanganya na mataifa na wakazikubali desturi zao.
ויעבדו את-עצביהם ויהיו להם למוקש 36
Waliabudu sanamu zao, zikawa mtego kwao.
ויזבחו את-בניהם ואת-בנותיהם-- לשדים 37
Wakawatoa wana wao na binti zao dhabihu kwa mashetani.
וישפכו דם נקי דם-בניהם ובנותיהם-- אשר זבחו לעצבי כנען ותחנף הארץ בדמים 38
Walimwaga damu isiyo na hatia, damu za wana wao na binti zao, ambao waliwatoa dhabihu kwa sanamu za Kanaani, nayo nchi ikanajisika kwa damu zao.
ויטמאו במעשיהם ויזנו במעלליהם 39
Wakajinajisi wenyewe kwa yale waliyotenda; kwa matendo yao wenyewe wakajifanyia ukahaba.
ויחר-אף יהוה בעמו ויתעב את-נחלתו 40
Kwa hiyo Bwana akawakasirikia watu wake na akauchukia sana urithi wake.
ויתנם ביד-גוים וימשלו בהם שנאיהם 41
Akawakabidhi kwa mataifa na adui zao wakawatawala.
וילחצום אויביהם ויכנעו תחת ידם 42
Adui zao wakawaonea na kuwatia chini ya mamlaka yao.
פעמים רבות יצילם והמה ימרו בעצתם וימכו בעונם 43
Mara nyingi aliwaokoa lakini walikuwa wamezama kwenye uasi, nao wakajiharibu katika dhambi zao.
וירא בצר להם-- בשמעו את-רנתם 44
Lakini akaangalia mateso yao wakati aliposikia kilio chao;
ויזכר להם בריתו וינחם כרב חסדו 45
kwa ajili yao akakumbuka agano lake, na kutokana na upendo wake mkuu akapooza hasira yake.
ויתן אותם לרחמים-- לפני כל-שוביהם 46
Akawafanya wahurumiwe na wote waliowashikilia mateka.
הושיענו יהוה אלהינו וקבצנו מן-הגוים להדות לשם קדשך להשתבח בתהלתך 47
Ee Bwana Mungu wetu, tuokoe. Tukusanye tena kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.
ברוך יהוה אלהי ישראל מן-העולם ועד העולם-- ואמר כל-העם אמן הללו-יה 48
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Watu wote na waseme, “Amen!” Msifuni Bwana.

< תהילים 106 >