< תהילים 104 >
ברכי נפשי את-יהוה יהוה אלהי גדלת מאד הוד והדר לבשת | 1 |
Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana. Ee Bwana Mungu wangu, wewe ni mkuu sana, umejivika utukufu na enzi.
עטה-אור כשלמה נוטה שמים כיריעה | 2 |
Amejifunika katika nuru kama vile kwa vazi, amezitandaza mbingu kama hema
המקרה במים עליותיו השם-עבים רכובו המהלך על-כנפי-רוח | 3 |
na kuziweka nguzo za orofa yake juu ya maji. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, na hupanda kwenye mbawa za upepo.
עשה מלאכיו רוחות משרתיו אש להט | 4 |
Huzifanya pepo kuwa wajumbe wake, miali ya moto watumishi wake.
יסד-ארץ על-מכוניה בל-תמוט עולם ועד | 5 |
Ameiweka dunia kwenye misingi yake, haiwezi kamwe kuondoshwa.
תהום כלבוש כסיתו על-הרים יעמדו מים | 6 |
Uliifunika kwa kilindi kama kwa vazi, maji yalisimama juu ya milima.
מן-גערתך ינוסון מן-קול רעמך יחפזון | 7 |
Lakini kwa kukemea kwako maji yalikimbia, kwa sauti ya radi yako yakatoroka,
יעלו הרים ירדו בקעות-- אל-מקום זה יסדת להם | 8 |
yakapanda milima, yakateremka mabondeni, hadi mahali pale ulipoyakusudia.
גבול-שמת בל-יעברון בל-ישבון לכסות הארץ | 9 |
Uliyawekea mpaka ambao hayawezi kuuvuka, kamwe hayataifunika dunia tena.
המשלח מעינים בנחלים בין הרים יהלכון | 10 |
Huzifanya chemchemi zimwage maji mabondeni, hutiririka kati ya milima.
ישקו כל-חיתו שדי ישברו פראים צמאם | 11 |
Huwapa maji wanyama wote wa kondeni, punda-mwitu huzima kiu yao.
עליהם עוף-השמים ישכון מבין עפאים יתנו-קול | 12 |
Ndege wa angani hufanya viota kando ya maji, huimba katikati ya matawi.
משקה הרים מעליותיו מפרי מעשיך תשבע הארץ | 13 |
Huinyeshea milima kutoka orofa zake, dunia inatoshelezwa kwa matunda ya kazi yake.
מצמיח חציר לבהמה ועשב לעבדת האדם להוציא לחם מן-הארץ | 14 |
Huyafanya majani ya mifugo yaote, na mimea kwa watu kulima, wajipatie chakula kutoka ardhini:
ויין ישמח לבב-אנוש-- להצהיל פנים משמן ולחם לבב-אנוש יסעד | 15 |
divai ya kuufurahisha moyo wa mwanadamu, mafuta kwa ajili ya kungʼarisha uso wake, na mkate wa kutia mwili nguvu.
ישבעו עצי יהוה-- ארזי לבנון אשר נטע | 16 |
Miti ya Bwana inanyeshewa vizuri, mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.
אשר-שם צפרים יקננו חסידה ברושים ביתה | 17 |
Humo ndege hufanya viota vyao, korongo ana nyumba yake kwenye msunobari.
הרים הגבהים ליעלים סלעים מחסה לשפנים | 18 |
Milima mirefu ni makao ya mbuzi-mwitu, majabali ni kimbilio la pelele.
עשה ירח למועדים שמש ידע מבואו | 19 |
Mwezi hugawanya majira, na jua hutambua wakati wake wa kutua.
תשת-חשך ויהי לילה-- בו-תרמש כל-חיתו-יער | 20 |
Unaleta giza, kunakuwa usiku, wanyama wote wa mwituni huzurura.
הכפירים שאגים לטרף ולבקש מאל אכלם | 21 |
Simba hunguruma kwa mawindo yao, na kutafuta chakula chao kutoka kwa Mungu.
תזרח השמש יאספון ואל-מעונתם ירבצון | 22 |
Jua huchomoza, nao huondoka, hurudi na kulala katika mapango yao.
יצא אדם לפעלו ולעבדתו עדי-ערב | 23 |
Kisha mwanadamu huenda kazini mwake, katika kazi yake mpaka jioni.
מה-רבו מעשיך יהוה-- כלם בחכמה עשית מלאה הארץ קנינך | 24 |
Ee Bwana, jinsi matendo yako yalivyo mengi! Kwa hekima ulizifanya zote, dunia imejaa viumbe vyako.
זה הים גדול-- ורחב ידים שם-רמש ואין מספר חיות קטנות עם-גדלות | 25 |
Pale kuna bahari, kubwa na yenye nafasi tele, imejaa viumbe visivyo na idadi, vitu vyenye uhai vikubwa na vidogo.
שם אניות יהלכון לויתן זה-יצרת לשחק-בו | 26 |
Huko meli huenda na kurudi, pia Lewiathani, uliyemuumba acheze ndani yake.
כלם אליך ישברון-- לתת אכלם בעתו | 27 |
Hawa wote wanakutazamia wewe, uwape chakula chao kwa wakati wake.
תתן להם ילקטון תפתח ידך ישבעון טוב | 28 |
Wakati unapowapa, wanakikusanya, unapofumbua mkono wako, wao wanashibishwa mema.
תסתיר פניך יבהלון תסף רוחם יגועון ואל-עפרם ישובון | 29 |
Unapoficha uso wako, wanapata hofu, unapoondoa pumzi yao, wanakufa na kurudi mavumbini.
תשלח רוחך יבראון ותחדש פני אדמה | 30 |
Unapopeleka Roho wako, wanaumbwa, nawe huufanya upya uso wa dunia.
יהי כבוד יהוה לעולם ישמח יהוה במעשיו | 31 |
Utukufu wa Bwana na udumu milele, Bwana na azifurahie kazi zake:
המביט לארץ ותרעד יגע בהרים ויעשנו | 32 |
yeye aitazamaye dunia, nayo ikatetemeka, aigusaye milima, nayo ikatoa moshi.
אשירה ליהוה בחיי אזמרה לאלהי בעודי | 33 |
Nitamwimbia Bwana maisha yangu yote; nitaimba sifa kwa Mungu wangu muda wote ninaoishi.
יערב עליו שיחי אנכי אשמח ביהוה | 34 |
Kutafakari kwangu na kumpendeze yeye, ninapofurahi katika Bwana.
יתמו חטאים מן-הארץ ורשעים עוד אינם-- ברכי נפשי את-יהוה הללו-יה | 35 |
Lakini wenye dhambi na watoweke katika dunia na waovu wasiwepo tena. Ee nafsi yangu, msifu Bwana. Msifuni Bwana.