< תהילים 103 >

לדוד ברכי נפשי את-יהוה וכל-קרבי את-שם קדשו 1
Nitamsifu Yahwe maisha yangu yote, na vyote vilivyomo ndani yangu, nitalisifu jina lake takatifu.
ברכי נפשי את-יהוה ואל-תשכחי כל-גמוליו 2
Maishani mwangu mwote nitamsifu Yahwe, na kukumbuka matendo yake yote mazuri.
הסלח לכל-עונכי הרפא לכל-תחלואיכי 3
Yeye husamehe dhambi zako zote; huponya magonjwa yako yote.
הגואל משחת חייכי המעטרכי חסד ורחמים 4
Huukomboa uhai wako dhidi ya uharubifu; hukuvika taji kwa uaminifu wa agano lake na hutenda kwa rehema.
המשביע בטוב עדיך תתחדש כנשר נעוריכי 5
Huyatosheleza maisha yako kwa mambo mema ili kwamba ujana wako ufanywe upya kama tai.
עשה צדקות יהוה ומשפטים לכל-עשוקים 6
Yahwe hutenda yaliyo haki naye hutenda hukumu ya haki kwa ajili ya wote walio onewa.
יודיע דרכיו למשה לבני ישראל עלילותיו 7
Alimjulisha Musa njia zake, matendo yake kwa uzao wa Israeli.
רחום וחנון יהוה ארך אפים ורב-חסד 8
Yahwe ni wa huruma na neema; ni mvumilivu; ana agano kuu la uaminifu.
לא-לנצח יריב ולא לעולם יטור 9
Hataadhibu siku zote; hakasiriki siku zote.
לא כחטאינו עשה לנו ולא כעונתינו גמל עלינו 10
Hatushughulikii sisi kama dhambi zetu zinavyostahili au kutulipa kulingana na uhitaji wa dhambi zetu.
כי כגבה שמים על-הארץ-- גבר חסדו על-יראיו 11
Kama mbingu zilivyo juu zaidi ya nchi, ndivyo ulivyo ukuu wa uaminifu wa agano lake kwao wale wanaomcha yeye.
כרחק מזרח ממערב-- הרחיק ממנו את-פשעינו 12
Kama vile mashariki ilivyo mbali na magharibi, hivi ndivyo ameondoa hatia zetu za dhambi zetu mbali nasi.
כרחם אב על-בנים-- רחם יהוה על-יראיו 13
Kama vile baba alivyo na huruma kwa watoto wake, ndivyo Yahwe alivyo na huruma kwao wamchao.
כי-הוא ידע יצרנו זכור כי-עפר אנחנו 14
Maana anajua tulivyo umbwa; anajua kuwa tu mavumbi.
אנוש כחציר ימיו כציץ השדה כן יציץ 15
Kama ilivyo kwa mwanadamu, siku zake ni kama majani; hustawi kama ua katika shamba.
כי רוח עברה-בו ואיננו ולא-יכירנו עוד מקומו 16
Upepo hulipiga, nalo hutoweka, na hakuna hata mmoja awezaye kuelezea mahali lilipokua.
וחסד יהוה מעולם ועד-עולם-- על-יראיו וצדקתו לבני בנים 17
Lakini agano la uaminifu wa Yahwe uko kwa wale wamchao yeye milele hata milele. Haki yake ni endelevu kwa uzao wao.
לשמרי בריתו ולזכרי פקדיו לעשותם 18
Wanashika agano lake na kukumbuka kutii maagizo yake.
יהוה--בשמים הכין כסאו ומלכותו בכל משלה 19
Yahwe ameweka kiti chake cha enzi mbinguni, na ufalme wake watawala juu ya kila mtu.
ברכו יהוה מלאכיו גברי כח עשי דברו לשמע בקול דברו 20
Msifuni Yahwe, enyi malaika zake, ninyi hodari wenye nguvu na mtendao neno lake, na kutii sauti ya neno lake.
ברכו יהוה כל-צבאיו-- משרתיו עשי רצונו 21
Msifuni Yahwe, enyi jeshi la malaika wote, ninyi ni watumishi mfanyao mapenzi yake.
ברכו יהוה כל-מעשיו-- בכל-מקמות ממשלתו ברכי נפשי את-יהוה 22
Msifuni Yahwe, viumbe wake wote, mahali popote atawalapo. Nitamsifu Yahwe maisha yangu yote.

< תהילים 103 >