< תהילים 103 >
לדוד ברכי נפשי את-יהוה וכל-קרבי את-שם קדשו | 1 |
Nitamsifu Yahwe maisha yangu yote, na vyote vilivyomo ndani yangu, nitalisifu jina lake takatifu.
ברכי נפשי את-יהוה ואל-תשכחי כל-גמוליו | 2 |
Maishani mwangu mwote nitamsifu Yahwe, na kukumbuka matendo yake yote mazuri.
הסלח לכל-עונכי הרפא לכל-תחלואיכי | 3 |
Yeye husamehe dhambi zako zote; huponya magonjwa yako yote.
הגואל משחת חייכי המעטרכי חסד ורחמים | 4 |
Huukomboa uhai wako dhidi ya uharubifu; hukuvika taji kwa uaminifu wa agano lake na hutenda kwa rehema.
המשביע בטוב עדיך תתחדש כנשר נעוריכי | 5 |
Huyatosheleza maisha yako kwa mambo mema ili kwamba ujana wako ufanywe upya kama tai.
עשה צדקות יהוה ומשפטים לכל-עשוקים | 6 |
Yahwe hutenda yaliyo haki naye hutenda hukumu ya haki kwa ajili ya wote walio onewa.
יודיע דרכיו למשה לבני ישראל עלילותיו | 7 |
Alimjulisha Musa njia zake, matendo yake kwa uzao wa Israeli.
רחום וחנון יהוה ארך אפים ורב-חסד | 8 |
Yahwe ni wa huruma na neema; ni mvumilivu; ana agano kuu la uaminifu.
לא-לנצח יריב ולא לעולם יטור | 9 |
Hataadhibu siku zote; hakasiriki siku zote.
לא כחטאינו עשה לנו ולא כעונתינו גמל עלינו | 10 |
Hatushughulikii sisi kama dhambi zetu zinavyostahili au kutulipa kulingana na uhitaji wa dhambi zetu.
כי כגבה שמים על-הארץ-- גבר חסדו על-יראיו | 11 |
Kama mbingu zilivyo juu zaidi ya nchi, ndivyo ulivyo ukuu wa uaminifu wa agano lake kwao wale wanaomcha yeye.
כרחק מזרח ממערב-- הרחיק ממנו את-פשעינו | 12 |
Kama vile mashariki ilivyo mbali na magharibi, hivi ndivyo ameondoa hatia zetu za dhambi zetu mbali nasi.
כרחם אב על-בנים-- רחם יהוה על-יראיו | 13 |
Kama vile baba alivyo na huruma kwa watoto wake, ndivyo Yahwe alivyo na huruma kwao wamchao.
כי-הוא ידע יצרנו זכור כי-עפר אנחנו | 14 |
Maana anajua tulivyo umbwa; anajua kuwa tu mavumbi.
אנוש כחציר ימיו כציץ השדה כן יציץ | 15 |
Kama ilivyo kwa mwanadamu, siku zake ni kama majani; hustawi kama ua katika shamba.
כי רוח עברה-בו ואיננו ולא-יכירנו עוד מקומו | 16 |
Upepo hulipiga, nalo hutoweka, na hakuna hata mmoja awezaye kuelezea mahali lilipokua.
וחסד יהוה מעולם ועד-עולם-- על-יראיו וצדקתו לבני בנים | 17 |
Lakini agano la uaminifu wa Yahwe uko kwa wale wamchao yeye milele hata milele. Haki yake ni endelevu kwa uzao wao.
לשמרי בריתו ולזכרי פקדיו לעשותם | 18 |
Wanashika agano lake na kukumbuka kutii maagizo yake.
יהוה--בשמים הכין כסאו ומלכותו בכל משלה | 19 |
Yahwe ameweka kiti chake cha enzi mbinguni, na ufalme wake watawala juu ya kila mtu.
ברכו יהוה מלאכיו גברי כח עשי דברו לשמע בקול דברו | 20 |
Msifuni Yahwe, enyi malaika zake, ninyi hodari wenye nguvu na mtendao neno lake, na kutii sauti ya neno lake.
ברכו יהוה כל-צבאיו-- משרתיו עשי רצונו | 21 |
Msifuni Yahwe, enyi jeshi la malaika wote, ninyi ni watumishi mfanyao mapenzi yake.
ברכו יהוה כל-מעשיו-- בכל-מקמות ממשלתו ברכי נפשי את-יהוה | 22 |
Msifuni Yahwe, viumbe wake wote, mahali popote atawalapo. Nitamsifu Yahwe maisha yangu yote.