< תהילים 101 >

לדוד מזמור חסד-ומשפט אשירה לך יהוה אזמרה 1
Nitaimba uaminifu wa agano lako na hukumu; kwako, Ee Yahwe, Nitakuimbia sifa.
אשכילה בדרך תמים-- מתי תבוא אלי אתהלך בתם-לבבי בקרב ביתי 2
Nitatembea katika njia ya uadilifu. Oh, ni lini utakuja kwangu? Nitatembea kwa uadilifu ndani ya nyumba yangu.
לא-אשית לנגד עיני-- דבר-בליעל עשה-סטים שנאתי לא ידבק בי 3
Sitaweka matendo maovu mbele ya macho yangu; ninachukia uovu usio na maana; hauta shikamana nami.
לבב עקש יסור ממני רע לא אדע 4
Watu waliopotoka wataniacha mimi; mimi sichangamani na uovu.
מלושני (מלשני) בסתר רעהו-- אותו אצמית גבה-עינים ורחב לבב-- אתו לא אוכל 5
Nitamwangamiza yeyote amsengenyaye jirani yake kwa siri. Sitamvumilia yeyote mwenye kiburi.
עיני בנאמני-ארץ-- לשבת עמדי הלך בדרך תמים-- הוא ישרתני 6
Nitawachagua walio waaminifu katika nchi wakae upande wangu. Wale watembeao katika njia ya uhadilifu watanitumikia.
לא-ישב בקרב ביתי-- עשה רמיה דבר שקרים-- לא-יכון לנגד עיני 7
Watu wadanganyifu hawatabaki ndani ya nyumba yangu; waongo hawatakaribishwa mbele ya macho yangu.
לבקרים אצמית כל-רשעי-ארץ להכרית מעיר-יהוה כל-פעלי און 8
Asubuhi hata asubuhi nitawaangamiza waovu wote kutoka nchini; nitawaondoa watendao maovu wote katika mji wa Yahwe.

< תהילים 101 >