< תהילים 1 >

אשרי האיש-- אשר לא הלך בעצת רשעים ובדרך חטאים לא עמד ובמושב לצים לא ישב 1
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
כי אם בתורת יהוה חפצו ובתורתו יהגה יומם ולילה 2
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
והיה-- כעץ שתול על-פלגי-מים אשר פריו יתן בעתו--ועלהו לא-יבול וכל אשר-יעשה יצליח 3
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
לא-כן הרשעים כי אם-כמץ אשר-תדפנו רוח 4
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
על-כן לא-יקמו רשעים--במשפט וחטאים בעדת צדיקים 5
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
כי-יודע יהוה דרך צדיקים ודרך רשעים תאבד 6
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.

< תהילים 1 >