< מִשְׁלֵי 29 >
איש תוכחות מקשה-ערף-- פתע ישבר ואין מרפא | 1 |
Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
ברבות צדיקים ישמח העם ובמשל רשע יאנח עם | 2 |
Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
איש-אהב חכמה ישמח אביו ורעה זונות יאבד-הון | 3 |
Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
מלך--במשפט יעמיד ארץ ואיש תרומות יהרסנה | 4 |
Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
גבר מחליק על-רעהו רשת פורש על-פעמיו | 5 |
Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
בפשע איש רע מוקש וצדיק ירון ושמח | 6 |
Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
ידע צדיק דין דלים רשע לא-יבין דעת | 7 |
Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
אנשי לצון יפיחו קריה וחכמים ישיבו אף | 8 |
Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
איש-חכם--נשפט את-איש אויל ורגז ושחק ואין נחת | 9 |
Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
אנשי דמים ישנאו-תם וישרים יבקשו נפשו | 10 |
Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
כל-רוחו יוציא כסיל וחכם באחור ישבחנה | 11 |
Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
משל מקשיב על-דבר-שקר-- כל-משרתיו רשעים | 12 |
Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
רש ואיש תככים נפגשו-- מאיר עיני שניהם יהוה | 13 |
Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
מלך שופט באמת דלים-- כסאו לעד יכון | 14 |
Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
שבט ותוכחת יתן חכמה ונער משלח מביש אמו | 15 |
Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
ברבות רשעים ירבה-פשע וצדיקים במפלתם יראו | 16 |
Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
יסר בנך ויניחך ויתן מעדנים לנפשך | 17 |
Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
באין חזון יפרע עם ושמר תורה אשרהו | 18 |
Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
בדברים לא-יוסר עבד כי-יבין ואין מענה | 19 |
Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
חזית--איש אץ בדבריו תקוה לכסיל ממנו | 20 |
Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
מפנק מנער עבדו ואחריתו יהיה מנון | 21 |
Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
איש-אף יגרה מדון ובעל חמה רב-פשע | 22 |
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
גאות אדם תשפילנו ושפל-רוח יתמך כבוד | 23 |
Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
חולק עם-גנב שונא נפשו אלה ישמע ולא יגיד | 24 |
Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
חרדת אדם יתן מוקש ובוטח ביהוה ישגב | 25 |
Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
רבים מבקשים פני-מושל ומיהוה משפט-איש | 26 |
Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
תועבת צדיקים איש עול ותועבת רשע ישר-דרך | 27 |
Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.