< מִשְׁלֵי 29 >

איש תוכחות מקשה-ערף-- פתע ישבר ואין מרפא 1
Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
ברבות צדיקים ישמח העם ובמשל רשע יאנח עם 2
Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
איש-אהב חכמה ישמח אביו ורעה זונות יאבד-הון 3
Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
מלך--במשפט יעמיד ארץ ואיש תרומות יהרסנה 4
Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
גבר מחליק על-רעהו רשת פורש על-פעמיו 5
Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
בפשע איש רע מוקש וצדיק ירון ושמח 6
Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
ידע צדיק דין דלים רשע לא-יבין דעת 7
Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
אנשי לצון יפיחו קריה וחכמים ישיבו אף 8
Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
איש-חכם--נשפט את-איש אויל ורגז ושחק ואין נחת 9
Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
אנשי דמים ישנאו-תם וישרים יבקשו נפשו 10
Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
כל-רוחו יוציא כסיל וחכם באחור ישבחנה 11
Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
משל מקשיב על-דבר-שקר-- כל-משרתיו רשעים 12
Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
רש ואיש תככים נפגשו-- מאיר עיני שניהם יהוה 13
Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
מלך שופט באמת דלים-- כסאו לעד יכון 14
Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
שבט ותוכחת יתן חכמה ונער משלח מביש אמו 15
Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
ברבות רשעים ירבה-פשע וצדיקים במפלתם יראו 16
Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
יסר בנך ויניחך ויתן מעדנים לנפשך 17
Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
באין חזון יפרע עם ושמר תורה אשרהו 18
Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
בדברים לא-יוסר עבד כי-יבין ואין מענה 19
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
חזית--איש אץ בדבריו תקוה לכסיל ממנו 20
Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
מפנק מנער עבדו ואחריתו יהיה מנון 21
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
איש-אף יגרה מדון ובעל חמה רב-פשע 22
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
גאות אדם תשפילנו ושפל-רוח יתמך כבוד 23
Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
חולק עם-גנב שונא נפשו אלה ישמע ולא יגיד 24
Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
חרדת אדם יתן מוקש ובוטח ביהוה ישגב 25
Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
רבים מבקשים פני-מושל ומיהוה משפט-איש 26
Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
תועבת צדיקים איש עול ותועבת רשע ישר-דרך 27
Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.

< מִשְׁלֵי 29 >