< מִשְׁלֵי 29 >
איש תוכחות מקשה-ערף-- פתע ישבר ואין מרפא | 1 |
Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
ברבות צדיקים ישמח העם ובמשל רשע יאנח עם | 2 |
Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
איש-אהב חכמה ישמח אביו ורעה זונות יאבד-הון | 3 |
Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
מלך--במשפט יעמיד ארץ ואיש תרומות יהרסנה | 4 |
Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
גבר מחליק על-רעהו רשת פורש על-פעמיו | 5 |
Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
בפשע איש רע מוקש וצדיק ירון ושמח | 6 |
Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
ידע צדיק דין דלים רשע לא-יבין דעת | 7 |
Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
אנשי לצון יפיחו קריה וחכמים ישיבו אף | 8 |
Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
איש-חכם--נשפט את-איש אויל ורגז ושחק ואין נחת | 9 |
Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
אנשי דמים ישנאו-תם וישרים יבקשו נפשו | 10 |
Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
כל-רוחו יוציא כסיל וחכם באחור ישבחנה | 11 |
Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
משל מקשיב על-דבר-שקר-- כל-משרתיו רשעים | 12 |
Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
רש ואיש תככים נפגשו-- מאיר עיני שניהם יהוה | 13 |
Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
מלך שופט באמת דלים-- כסאו לעד יכון | 14 |
Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
שבט ותוכחת יתן חכמה ונער משלח מביש אמו | 15 |
Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
ברבות רשעים ירבה-פשע וצדיקים במפלתם יראו | 16 |
Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
יסר בנך ויניחך ויתן מעדנים לנפשך | 17 |
Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
באין חזון יפרע עם ושמר תורה אשרהו | 18 |
Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
בדברים לא-יוסר עבד כי-יבין ואין מענה | 19 |
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
חזית--איש אץ בדבריו תקוה לכסיל ממנו | 20 |
Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
מפנק מנער עבדו ואחריתו יהיה מנון | 21 |
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
איש-אף יגרה מדון ובעל חמה רב-פשע | 22 |
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
גאות אדם תשפילנו ושפל-רוח יתמך כבוד | 23 |
Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
חולק עם-גנב שונא נפשו אלה ישמע ולא יגיד | 24 |
Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
חרדת אדם יתן מוקש ובוטח ביהוה ישגב | 25 |
Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
רבים מבקשים פני-מושל ומיהוה משפט-איש | 26 |
Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
תועבת צדיקים איש עול ותועבת רשע ישר-דרך | 27 |
Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.