< מִשְׁלֵי 26 >
כשלג בקיץ--וכמטר בקציר כן לא-נאוה לכסיל כבוד | 1 |
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
כצפור לנוד כדרור לעוף-- כן קללת חנם לא (לו) תבא | 2 |
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
שוט לסוס מתג לחמור ושבט לגו כסילים | 3 |
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
אל-תען כסיל כאולתו פן-תשוה-לו גם-אתה | 4 |
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
ענה כסיל כאולתו פן-יהיה חכם בעיניו | 5 |
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
מקצה רגלים חמס שתה-- שלח דברים ביד-כסיל | 6 |
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
דליו שקים מפסח ומשל בפי כסילים | 7 |
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
כצרור אבן במרגמה-- כן-נותן לכסיל כבוד | 8 |
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
חוח עלה ביד-שכור ומשל בפי כסילים | 9 |
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
רב מחולל-כל ושכר כסיל ושכר עברים | 10 |
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
ככלב שב על-קאו-- כסיל שונה באולתו | 11 |
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
ראית--איש חכם בעיניו תקוה לכסיל ממנו | 12 |
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
אמר עצל שחל בדרך ארי בין הרחבות | 13 |
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
הדלת תסוב על-צירה ועצל על-מטתו | 14 |
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
טמן עצל ידו בצלחת נלאה להשיבה אל-פיו | 15 |
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
חכם עצל בעיניו-- משבעה משיבי טעם | 16 |
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
מחזיק באזני-כלב-- עבר מתעבר על-ריב לא-לו | 17 |
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
כמתלהלה הירה זקים-- חצים ומות | 18 |
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
כן-איש רמה את-רעהו ואמר הלא-משחק אני | 19 |
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
באפס עצים תכבה-אש ובאין נרגן ישתק מדון | 20 |
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
פחם לגחלים ועצים לאש ואיש מדונים (מדינים) לחרחר-ריב | 21 |
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
דברי נרגן כמתלהמים והם ירדו חדרי-בטן | 22 |
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
כסף סיגים מצפה על-חרש-- שפתים דלקים ולב-רע | 23 |
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
בשפתו ינכר שונא ובקרבו ישית מרמה | 24 |
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
כי-יחנן קולו אל-תאמן-בו כי שבע תועבות בלבו | 25 |
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
תכסה שנאה במשאון תגלה רעתו בקהל | 26 |
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
כרה-שחת בה יפול וגולל אבן אליו תשוב | 27 |
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
לשון-שקר ישנא דכיו ופה חלק יעשה מדחה | 28 |
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.