< מִשְׁלֵי 24 >

אל-תקנא באנשי רעה ואל-תתאו להיות אתם 1
Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
כי-שד יהגה לבם ועמל שפתיהם תדברנה 2
kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
בחכמה יבנה בית ובתבונה יתכונן 3
Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
ובדעת חדרים ימלאו-- כל-הון יקר ונעים 4
kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
גבר-חכם בעוז ואיש-דעת מאמץ-כח 5
Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
כי בתחבלות תעשה-לך מלחמה ותשועה ברב יועץ 6
kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
ראמות לאויל חכמות בשער לא יפתח-פיהו 7
Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
מחשב להרע-- לו בעל-מזמות יקראו 8
Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
זמת אולת חטאת ותועבת לאדם לץ 9
Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
התרפית ביום צרה-- צר כחכה 10
Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
הצל לקחים למות ומטים להרג אם-תחשוך 11
Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
כי-תאמר-- הן לא-ידענו-זה הלא-תכן לבות הוא-יבין ונצר נפשך הוא ידע והשיב לאדם כפעלו 12
Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
אכל-בני דבש כי-טוב ונפת מתוק על-חכך 13
Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
כן דעה חכמה--לנפשך אם-מצאת ויש אחרית ותקותך לא תכרת 14
Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
אל-תארב רשע לנוה צדיק אל-תשדד רבצו 15
Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
כי שבע יפול צדיק וקם ורשעים יכשלו ברעה 16
Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
בנפל אויביך (אויבך) אל-תשמח ובכשלו אל-יגל לבך 17
Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
פן-יראה יהוה ורע בעיניו והשיב מעליו אפו 18
Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
אל-תתחר במרעים אל-תקנא ברשעים 19
Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
כי לא-תהיה אחרית לרע נר רשעים ידעך 20
kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
ירא-את-יהוה בני ומלך עם-שונים אל-תתערב 21
Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
כי-פתאם יקום אידם ופיד שניהם מי יודע 22
kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
גם-אלה לחכמים הכר-פנים במשפט בל-טוב 23
Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
אמר לרשע--צדיק אתה יקבהו עמים יזעמוהו לאמים 24
Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
ולמוכיחים ינעם ועליהם תבוא ברכת-טוב 25
Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
שפתים ישק משיב דברים נכחים 26
Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
הכן בחוץ מלאכתך--ועתדה בשדה לך אחר ובנית ביתך 27
Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
אל-תהי עד-חנם ברעך והפתית בשפתיך 28
Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
אל-תאמר--כאשר עשה-לי כן אעשה-לו אשיב לאיש כפעלו 29
Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
על-שדה איש-עצל עברתי ועל-כרם אדם חסר-לב 30
Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
והנה עלה כלו קמשנים--כסו פניו חרלים וגדר אבניו נהרסה 31
miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
ואחזה אנכי אשית לבי ראיתי לקחתי מוסר 32
Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
מעט שנות מעט תנומות מעט חבק ידים לשכב 33
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
ובא-מתהלך רישך ומחסריך כאיש מגן 34
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.

< מִשְׁלֵי 24 >