< מִשְׁלֵי 24 >
אל-תקנא באנשי רעה ואל-תתאו להיות אתם | 1 |
Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
כי-שד יהגה לבם ועמל שפתיהם תדברנה | 2 |
kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
בחכמה יבנה בית ובתבונה יתכונן | 3 |
Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
ובדעת חדרים ימלאו-- כל-הון יקר ונעים | 4 |
kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
גבר-חכם בעוז ואיש-דעת מאמץ-כח | 5 |
Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
כי בתחבלות תעשה-לך מלחמה ותשועה ברב יועץ | 6 |
kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
ראמות לאויל חכמות בשער לא יפתח-פיהו | 7 |
Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
מחשב להרע-- לו בעל-מזמות יקראו | 8 |
Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
זמת אולת חטאת ותועבת לאדם לץ | 9 |
Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
התרפית ביום צרה-- צר כחכה | 10 |
Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
הצל לקחים למות ומטים להרג אם-תחשוך | 11 |
Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
כי-תאמר-- הן לא-ידענו-זה הלא-תכן לבות הוא-יבין ונצר נפשך הוא ידע והשיב לאדם כפעלו | 12 |
Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
אכל-בני דבש כי-טוב ונפת מתוק על-חכך | 13 |
Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
כן דעה חכמה--לנפשך אם-מצאת ויש אחרית ותקותך לא תכרת | 14 |
Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
אל-תארב רשע לנוה צדיק אל-תשדד רבצו | 15 |
Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
כי שבע יפול צדיק וקם ורשעים יכשלו ברעה | 16 |
Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
בנפל אויביך (אויבך) אל-תשמח ובכשלו אל-יגל לבך | 17 |
Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
פן-יראה יהוה ורע בעיניו והשיב מעליו אפו | 18 |
Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
אל-תתחר במרעים אל-תקנא ברשעים | 19 |
Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
כי לא-תהיה אחרית לרע נר רשעים ידעך | 20 |
kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
ירא-את-יהוה בני ומלך עם-שונים אל-תתערב | 21 |
Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
כי-פתאם יקום אידם ופיד שניהם מי יודע | 22 |
kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
גם-אלה לחכמים הכר-פנים במשפט בל-טוב | 23 |
Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
אמר לרשע--צדיק אתה יקבהו עמים יזעמוהו לאמים | 24 |
Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
ולמוכיחים ינעם ועליהם תבוא ברכת-טוב | 25 |
Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
שפתים ישק משיב דברים נכחים | 26 |
Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
הכן בחוץ מלאכתך--ועתדה בשדה לך אחר ובנית ביתך | 27 |
Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
אל-תהי עד-חנם ברעך והפתית בשפתיך | 28 |
Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
אל-תאמר--כאשר עשה-לי כן אעשה-לו אשיב לאיש כפעלו | 29 |
Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
על-שדה איש-עצל עברתי ועל-כרם אדם חסר-לב | 30 |
Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
והנה עלה כלו קמשנים--כסו פניו חרלים וגדר אבניו נהרסה | 31 |
miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
ואחזה אנכי אשית לבי ראיתי לקחתי מוסר | 32 |
Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
מעט שנות מעט תנומות מעט חבק ידים לשכב | 33 |
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
ובא-מתהלך רישך ומחסריך כאיש מגן | 34 |
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.