< מִשְׁלֵי 2 >

בני אם-תקח אמרי ומצותי תצפן אתך 1
Mwanangu, kama ukiyapokea maneno yangu na kuzitunza amri zangu,
להקשיב לחכמה אזנך תטה לבך לתבונה 2
usikilize hekima na utaelekeza moyo wako katika ufahamu.
כי אם לבינה תקרא לתבונה תתן קולך 3
kama utalilia ufahamu na kupaza sauti yako kwa ajili ya ufahamu,
אם-תבקשנה ככסף וכמטמונים תחפשנה 4
kama utautafuta kama fedha na kupekua ufahamu kama unatafuta hazina iliyojificha,
אז--תבין יראת יהוה ודעת אלהים תמצא 5
ndipo utakapofahamu hofu ya Yehova na utapata maarifa ya Mungu.
כי-יהוה יתן חכמה מפיו דעת ותבונה 6
Kwa kuwa Yohova hutoa hekima, katika kinywa chake hutoka maarifa na ufahamu.
וצפן (יצפן) לישרים תושיה מגן להלכי תם 7
Yeye huhifadhi sauti ya hekima kwa wale wampendezao, yeye ni ngao kwa wale waendao katika uadilifu,
לנצר ארחות משפט ודרך חסידו ישמר 8
huongoza katika njia za haki na atalinda njia ya waaminifu kwake.
אז--תבין צדק ומשפט ומישרים כל-מעגל-טוב 9
Ndipo utakapoelewa wema, haki, usawa na kila njia njema.
כי-תבוא חכמה בלבך ודעת לנפשך ינעם 10
Maana hekima itaingia moyoni mwako na maarifa yataipendeza nafsi yako.
מזמה תשמר עליך תבונה תנצרכה 11
Busara itakulinda, ufahamu utakuongoza.
להצילך מדרך רע מאיש מדבר תהפכות 12
Vitakuokoa kutoka katika njia ya uovu, kutoka kwa wale waongeao mambo potovu.
העזבים ארחות ישר-- ללכת בדרכי-חשך 13
Ambao huziacha njia za wema na kutembea katika njia za giza.
השמחים לעשות רע יגילו בתהפכות רע 14
Hufurahia wanapotenda maovu na hupendezwa katika upotovu.
אשר ארחתיהם עקשים ונלוזים במעגלותם 15
Hufuata njia za udanganyifu na kwa kutumia ghilba huficha mapito yao.
להצילך מאשה זרה מנכריה אמריה החליקה 16
Busara na hekima zitakuokoa kutoka kwa mwanamke malaya, kutoka kwa mwanamke anayetafuta visa na mwenye maneno ya kubembeleza.
העזבת אלוף נעוריה ואת-ברית אלהיה שכחה 17
Yeye humwacha mwenzi wa ujana wake na kusahau agano la Mungu wake.
כי שחה אל-מות ביתה ואל-רפאים מעגלתיה 18
Maana nyumba yake huinama na kufa na mapito yake yatakupeleka kwa wale walioko kaburini.
כל-באיה לא ישובון ולא-ישיגו ארחות חיים 19
Wote waiendeao njia yake hawatarudi tena na wala hawataziona njia za uzima.
למען--תלך בדרך טובים וארחות צדיקים תשמר 20
kwa hiyo utatembea katika njia ya watu wema na kufuata njia za wale watendao mema.
כי-ישרים ישכנו-ארץ ותמימים יותרו בה 21
Kwa wale watendao mema watafanya makazi yao katika nchi, na wale wenye uadilifu watadumu katika nchi.
ורשעים מארץ יכרתו ובוגדים יסחו ממנה 22
Lakini waovu wataondolewa katika nchi na wale wasioamini wataondolewa katika nchi.

< מִשְׁלֵי 2 >