< מִשְׁלֵי 17 >

טוב פת חרבה ושלוה-בה-- מבית מלא זבחי-ריב 1
Ni bora kuwa na utulivu pamoja chembe za mkate kuliko nyumba yenye sherehe nyingi pamoja na ugomvi.
עבד-משכיל--ימשל בבן מביש ובתוך אחים יחלק נחלה 2
Mtumishi mwenye busara atatawala juu ya mwana atendaye kwa aibu na atashiriki urithi kama mmoja wa ndugu.
מצרף לכסף וכור לזהב ובחן לבות יהוה 3
Kalibu ni kwa fedha na tanuu ni kwa dhahabu, bali Yehova huisafisha mioyo.
מרע מקשיב על-שפת-און שקר מזין על-לשון הות 4
Mtu atendaye mabaya huwasikiliza wale wanaosema maovu; muongo anausikivu kwa wale wanaosema mambo mabaya.
לעג לרש חרף עשהו שמח לאיד לא ינקה 5
Mwenye kumdhihaki masikini humtukana Muumba wake na anayefurahia msiba hatakosa adhabu.
עטרת זקנים בני בנים ותפארת בנים אבותם 6
Wajukuu ni taji ya wazee na wazazi huleta heshima kwa watoto wao.
לא-נאוה לנבל שפת-יתר אף כי-לנדיב שפת-שקר 7
Hotuba ya ushawishi haifai kwa mpumbavu; kidogo zaidi midomo ya uongo inafaa kwa ufalme.
אבן-חן השחד בעיני בעליו אל-כל-אשר יפנה ישכיל 8
Rushwa ni kama jiwe la kiini macho kwa yule ambaye atoaye; yeye anayeiacha, hufanikiwa.
מכסה-פשע מבקש אהבה ושנה בדבר מפריד אלוף 9
Anayesamehe kosa hutafuta upendo, bali yeye anayerudia jambo huwatenganisha marafiki wa karibu.
תחת גערה במבין-- מהכות כסיל מאה 10
Karipio hupenya ndani ya mtu mwenye ufahamu kuliko mapigo mamia kwenda kwa mpumbavu.
אך-מרי יבקש-רע ומלאך אכזרי ישלח-בו 11
Mtu mbaya hutafuta uasi tu, hivyo mjumbe katiri atatumwa dhidi yake.
פגוש דב שכול באיש ואל-כסיל באולתו 12
Ni bora kukutana na dubu aliyeporwa watoto wake kuliko kukutana na mpumbavu katika upumbavu wake.
משיב רעה תחת טובה-- לא-תמיש (תמוש) רעה מביתו 13
Mtu anaporudisha mabaya badala ya mema, mabaya hayatatoka katika nyumba yake.
פוטר מים ראשית מדון ולפני התגלע הריב נטוש 14
Mwanzo wa mafarakano ni kama mtu anayefungulia maji kila mahali, hivyo ondoka kwenye mabishano kabla ya kutokea.
מצדיק רשע ומרשיע צדיק-- תועבת יהוה גם-שניהם 15
Yeye ambaye huwaachilia watu waovu au kuwalaumu wale wanaotenda haki - watu hawa wote ni chukizo kwa Yehova.
למה-זה מחיר ביד-כסיל-- לקנות חכמה ולב-אין 16
Kwa nini mpumbavu alipe fedha kwa kujifunza hekima, wakati hana uwezo wa kujifunza?
בכל-עת אהב הרע ואח לצרה יולד 17
Rafiki hupenda kwa nyakati zote na ndugu amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.
אדם חסר-לב תוקע כף ערב ערבה לפני רעהו 18
Mtu asiyekuwa na akili hufanya ahadi zenye mashariti na kuanza kuwajibika kwa madeni ya jirani yake.
אהב פשע אהב מצה מגביה פתחו מבקש-שבר 19
Apendaye mafarakano anapenda dhambi; ambaye hutengeneza kizingiti kirefu sana kwenye mlango wake husababisha kuvunjia kwa mifupa.
עקש-לב לא ימצא-טוב ונהפך בלשונו יפול ברעה 20
Mtu mwenye moyo wa udanganyifu hapati chochote ambacho ni chema; na mwenye ulimi wa ukaidi huanguka kwenye janga.
ילד כסיל לתוגה לו ולא-ישמח אבי נבל 21
Mzazi wa mpumbavu huleta majonzi kwake mwenyewe; baba wa mpumbavu hana furaha.
לב שמח ייטיב גהה ורוח נכאה תיבש-גרם 22
Moyo mchangamfu ni dawa njema, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
שחד מחק רשע יקח-- להטות ארחות משפט 23
Mtu mwovu hukubali rushwa ya siri ili kupotosha njia za haki.
את-פני מבין חכמה ועיני כסיל בקצה-ארץ 24
Mwenye ufahamu huelekeza uso wake kwenye hekima, bali macho ya mpumbavu huelekea ncha za dunia.
כעס לאביו בן כסיל וממר ליולדתו 25
Mwana mpumbavu ni huzuni kwa baba yake na uchungu kwa mwanamke aliyemzaa.
גם ענוש לצדיק לא-טוב-- להכות נדיבים על-ישר 26
Pia, si vizuri kumwadhibu mwenye kutenda haki; wala si vema kuwachapa mjeledi watu waadilifu wenye ukamilifu.
חושך אמריו יודע דעת וקר- (יקר-) רוח איש תבונה 27
Mwenye maarifa hutumia maneno machache na mwenye ufahamu ni mtulivu.
גם אויל מחריש חכם יחשב אטם שפתיו נבון 28
Hata mpumbavu hudhaniwa kuwa na busara kama akikaa kimya; wakati anapokaa amefunga kinywa chake, anafikiriwa kuwa na akili.

< מִשְׁלֵי 17 >