< מִשְׁלֵי 17 >
טוב פת חרבה ושלוה-בה-- מבית מלא זבחי-ריב | 1 |
Ni bora kuwa na utulivu pamoja chembe za mkate kuliko nyumba yenye sherehe nyingi pamoja na ugomvi.
עבד-משכיל--ימשל בבן מביש ובתוך אחים יחלק נחלה | 2 |
Mtumishi mwenye busara atatawala juu ya mwana atendaye kwa aibu na atashiriki urithi kama mmoja wa ndugu.
מצרף לכסף וכור לזהב ובחן לבות יהוה | 3 |
Kalibu ni kwa fedha na tanuu ni kwa dhahabu, bali Yehova huisafisha mioyo.
מרע מקשיב על-שפת-און שקר מזין על-לשון הות | 4 |
Mtu atendaye mabaya huwasikiliza wale wanaosema maovu; muongo anausikivu kwa wale wanaosema mambo mabaya.
לעג לרש חרף עשהו שמח לאיד לא ינקה | 5 |
Mwenye kumdhihaki masikini humtukana Muumba wake na anayefurahia msiba hatakosa adhabu.
עטרת זקנים בני בנים ותפארת בנים אבותם | 6 |
Wajukuu ni taji ya wazee na wazazi huleta heshima kwa watoto wao.
לא-נאוה לנבל שפת-יתר אף כי-לנדיב שפת-שקר | 7 |
Hotuba ya ushawishi haifai kwa mpumbavu; kidogo zaidi midomo ya uongo inafaa kwa ufalme.
אבן-חן השחד בעיני בעליו אל-כל-אשר יפנה ישכיל | 8 |
Rushwa ni kama jiwe la kiini macho kwa yule ambaye atoaye; yeye anayeiacha, hufanikiwa.
מכסה-פשע מבקש אהבה ושנה בדבר מפריד אלוף | 9 |
Anayesamehe kosa hutafuta upendo, bali yeye anayerudia jambo huwatenganisha marafiki wa karibu.
תחת גערה במבין-- מהכות כסיל מאה | 10 |
Karipio hupenya ndani ya mtu mwenye ufahamu kuliko mapigo mamia kwenda kwa mpumbavu.
אך-מרי יבקש-רע ומלאך אכזרי ישלח-בו | 11 |
Mtu mbaya hutafuta uasi tu, hivyo mjumbe katiri atatumwa dhidi yake.
פגוש דב שכול באיש ואל-כסיל באולתו | 12 |
Ni bora kukutana na dubu aliyeporwa watoto wake kuliko kukutana na mpumbavu katika upumbavu wake.
משיב רעה תחת טובה-- לא-תמיש (תמוש) רעה מביתו | 13 |
Mtu anaporudisha mabaya badala ya mema, mabaya hayatatoka katika nyumba yake.
פוטר מים ראשית מדון ולפני התגלע הריב נטוש | 14 |
Mwanzo wa mafarakano ni kama mtu anayefungulia maji kila mahali, hivyo ondoka kwenye mabishano kabla ya kutokea.
מצדיק רשע ומרשיע צדיק-- תועבת יהוה גם-שניהם | 15 |
Yeye ambaye huwaachilia watu waovu au kuwalaumu wale wanaotenda haki - watu hawa wote ni chukizo kwa Yehova.
למה-זה מחיר ביד-כסיל-- לקנות חכמה ולב-אין | 16 |
Kwa nini mpumbavu alipe fedha kwa kujifunza hekima, wakati hana uwezo wa kujifunza?
בכל-עת אהב הרע ואח לצרה יולד | 17 |
Rafiki hupenda kwa nyakati zote na ndugu amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.
אדם חסר-לב תוקע כף ערב ערבה לפני רעהו | 18 |
Mtu asiyekuwa na akili hufanya ahadi zenye mashariti na kuanza kuwajibika kwa madeni ya jirani yake.
אהב פשע אהב מצה מגביה פתחו מבקש-שבר | 19 |
Apendaye mafarakano anapenda dhambi; ambaye hutengeneza kizingiti kirefu sana kwenye mlango wake husababisha kuvunjia kwa mifupa.
עקש-לב לא ימצא-טוב ונהפך בלשונו יפול ברעה | 20 |
Mtu mwenye moyo wa udanganyifu hapati chochote ambacho ni chema; na mwenye ulimi wa ukaidi huanguka kwenye janga.
ילד כסיל לתוגה לו ולא-ישמח אבי נבל | 21 |
Mzazi wa mpumbavu huleta majonzi kwake mwenyewe; baba wa mpumbavu hana furaha.
לב שמח ייטיב גהה ורוח נכאה תיבש-גרם | 22 |
Moyo mchangamfu ni dawa njema, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
שחד מחק רשע יקח-- להטות ארחות משפט | 23 |
Mtu mwovu hukubali rushwa ya siri ili kupotosha njia za haki.
את-פני מבין חכמה ועיני כסיל בקצה-ארץ | 24 |
Mwenye ufahamu huelekeza uso wake kwenye hekima, bali macho ya mpumbavu huelekea ncha za dunia.
כעס לאביו בן כסיל וממר ליולדתו | 25 |
Mwana mpumbavu ni huzuni kwa baba yake na uchungu kwa mwanamke aliyemzaa.
גם ענוש לצדיק לא-טוב-- להכות נדיבים על-ישר | 26 |
Pia, si vizuri kumwadhibu mwenye kutenda haki; wala si vema kuwachapa mjeledi watu waadilifu wenye ukamilifu.
חושך אמריו יודע דעת וקר- (יקר-) רוח איש תבונה | 27 |
Mwenye maarifa hutumia maneno machache na mwenye ufahamu ni mtulivu.
גם אויל מחריש חכם יחשב אטם שפתיו נבון | 28 |
Hata mpumbavu hudhaniwa kuwa na busara kama akikaa kimya; wakati anapokaa amefunga kinywa chake, anafikiriwa kuwa na akili.