< מִשְׁלֵי 17 >
טוב פת חרבה ושלוה-בה-- מבית מלא זבחי-ריב | 1 |
Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
עבד-משכיל--ימשל בבן מביש ובתוך אחים יחלק נחלה | 2 |
Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
מצרף לכסף וכור לזהב ובחן לבות יהוה | 3 |
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
מרע מקשיב על-שפת-און שקר מזין על-לשון הות | 4 |
Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
לעג לרש חרף עשהו שמח לאיד לא ינקה | 5 |
Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
עטרת זקנים בני בנים ותפארת בנים אבותם | 6 |
Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
לא-נאוה לנבל שפת-יתר אף כי-לנדיב שפת-שקר | 7 |
Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
אבן-חן השחד בעיני בעליו אל-כל-אשר יפנה ישכיל | 8 |
Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
מכסה-פשע מבקש אהבה ושנה בדבר מפריד אלוף | 9 |
Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
תחת גערה במבין-- מהכות כסיל מאה | 10 |
Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
אך-מרי יבקש-רע ומלאך אכזרי ישלח-בו | 11 |
Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
פגוש דב שכול באיש ואל-כסיל באולתו | 12 |
Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
משיב רעה תחת טובה-- לא-תמיש (תמוש) רעה מביתו | 13 |
Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
פוטר מים ראשית מדון ולפני התגלע הריב נטוש | 14 |
Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
מצדיק רשע ומרשיע צדיק-- תועבת יהוה גם-שניהם | 15 |
Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
למה-זה מחיר ביד-כסיל-- לקנות חכמה ולב-אין | 16 |
Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
בכל-עת אהב הרע ואח לצרה יולד | 17 |
Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
אדם חסר-לב תוקע כף ערב ערבה לפני רעהו | 18 |
Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
אהב פשע אהב מצה מגביה פתחו מבקש-שבר | 19 |
Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
עקש-לב לא ימצא-טוב ונהפך בלשונו יפול ברעה | 20 |
Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
ילד כסיל לתוגה לו ולא-ישמח אבי נבל | 21 |
Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
לב שמח ייטיב גהה ורוח נכאה תיבש-גרם | 22 |
Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
שחד מחק רשע יקח-- להטות ארחות משפט | 23 |
Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
את-פני מבין חכמה ועיני כסיל בקצה-ארץ | 24 |
Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
כעס לאביו בן כסיל וממר ליולדתו | 25 |
Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
גם ענוש לצדיק לא-טוב-- להכות נדיבים על-ישר | 26 |
Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
חושך אמריו יודע דעת וקר- (יקר-) רוח איש תבונה | 27 |
Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
גם אויל מחריש חכם יחשב אטם שפתיו נבון | 28 |
Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.