< מִשְׁלֵי 14 >
חכמות נשים בנתה ביתה ואולת בידיה תהרסנו | 1 |
Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
הולך בישרו ירא יהוה ונלוז דרכיו בוזהו | 2 |
Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
בפי-אויל חטר גאוה ושפתי חכמים תשמורם | 3 |
Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
באין אלפים אבוס בר ורב-תבואות בכח שור | 4 |
Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
עד אמונים לא יכזב ויפיח כזבים עד שקר | 5 |
Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
בקש-לץ חכמה ואין ודעת לנבון נקל | 6 |
Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
לך מנגד לאיש כסיל ובל-ידעת שפתי-דעת | 7 |
Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
חכמת ערום הבין דרכו ואולת כסילים מרמה | 8 |
Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
אולים יליץ אשם ובין ישרים רצון | 9 |
Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
לב--יודע מרת נפשו ובשמחתו לא-יתערב זר | 10 |
Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
בית רשעים ישמד ואהל ישרים יפריח | 11 |
Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
יש דרך ישר לפני-איש ואחריתה דרכי-מות | 12 |
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
גם-בשחק יכאב-לב ואחריתה שמחה תוגה | 13 |
Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
מדרכיו ישבע סוג לב ומעליו איש טוב | 14 |
Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
פתי יאמין לכל-דבר וערום יבין לאשרו | 15 |
Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
חכם ירא וסר מרע וכסיל מתעבר ובוטח | 16 |
Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
קצר-אפים יעשה אולת ואיש מזמות ישנא | 17 |
Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
נחלו פתאים אולת וערומים יכתרו דעת | 18 |
Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
שחו רעים לפני טובים ורשעים על-שערי צדיק | 19 |
Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
גם-לרעהו ישנא רש ואהבי עשיר רבים | 20 |
Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
בז-לרעהו חוטא ומחונן עניים (ענוים) אשריו | 21 |
Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
הלוא-יתעו חרשי רע וחסד ואמת חרשי טוב | 22 |
Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
בכל-עצב יהיה מותר ודבר-שפתים אך-למחסור | 23 |
Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
עטרת חכמים עשרם אולת כסילים אולת | 24 |
Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
מציל נפשות עד אמת ויפח כזבים מרמה | 25 |
Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
ביראת יהוה מבטח-עז ולבניו יהיה מחסה | 26 |
Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
יראת יהוה מקור חיים-- לסור ממקשי מות | 27 |
Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
ברב-עם הדרת-מלך ובאפס לאם מחתת רזון | 28 |
Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
ארך אפים רב-תבונה וקצר-רוח מרים אולת | 29 |
Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
חיי בשרים לב מרפא ורקב עצמות קנאה | 30 |
Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
עשק דל חרף עשהו ומכבדו חנן אביון | 31 |
Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
ברעתו ידחה רשע וחסה במותו צדיק | 32 |
Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
בלב נבון תנוח חכמה ובקרב כסילים תודע | 33 |
Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
צדקה תרומם-גוי וחסד לאמים חטאת | 34 |
Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
רצון-מלך לעבד משכיל ועברתו תהיה מביש | 35 |
Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.