< מִשְׁלֵי 14 >

חכמות נשים בנתה ביתה ואולת בידיה תהרסנו 1
Mwanamke mwenye busara huijenga nyumba yake, bali mwanamke mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
הולך בישרו ירא יהוה ונלוז דרכיו בוזהו 2
Yeye aendaye kwa uaminifu humcha Yehova, bali mkaidi humdharau katika njia zake.
בפי-אויל חטר גאוה ושפתי חכמים תשמורם 3
Katika kinywa cha mpumbavu hutoka chipukizi la kiburi chake, bali midomo ya wenye busara itawalinda.
באין אלפים אבוס בר ורב-תבואות בכח שור 4
Pale pasipo na mifugo hori la kulishia ni safi, bali mazao mengi huweza kupatikana kwa nguvu za maksai.
עד אמונים לא יכזב ויפיח כזבים עד שקר 5
Shahidi mwaminifu hasemi uongo, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
בקש-לץ חכמה ואין ודעת לנבון נקל 6
Mwenye dharau hutafuta hekima na hakuna hata, bali maarifa huja kwa urahisi kwa mwenye ufahamu.
לך מנגד לאיש כסיל ובל-ידעת שפתי-דעת 7
Nenda mbali kutoka kwa mtu mpumbavu, maana hutapata maarifa kwenye midomo yake.
חכמת ערום הבין דרכו ואולת כסילים מרמה 8
Hekima ya mtu mwenye busara ni kuifahamu njia yake mwenyewe, bali upuuzi wa wapumbavu ni udanganyifu.
אולים יליץ אשם ובין ישרים רצון 9
Wapumbavu hudharau wakati sadaka ya hatia inapotolewa, bali miongoni mwao waaminifu hushiriki fadhila.
לב--יודע מרת נפשו ובשמחתו לא-יתערב זר 10
Moyo unayajua machungu yake mwenyewe na hakuna mgeni anayeshiriki furaha yake.
בית רשעים ישמד ואהל ישרים יפריח 11
Nyumba ya waovu itaangamizwa, bali hema ya watu waaminifu itasitawi.
יש דרך ישר לפני-איש ואחריתה דרכי-מות 12
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, lakini mwisho wake huelekea mauti tu.
גם-בשחק יכאב-לב ואחריתה שמחה תוגה 13
Moyo unaweza kucheka lakini bado ukawa katika maumivu na furaha inaweza kukoma ikawa huzuni.
מדרכיו ישבע סוג לב ומעליו איש טוב 14
Yule asiyemwaminifu atapata anachostahili kwa njia zake, bali mtu mwema atapata kilicho chake.
פתי יאמין לכל-דבר וערום יבין לאשרו 15
Yeye ambaye hakufundishwa huamini kila kitu, bali mtu mwenye hekima huzifikiria hatua zake.
חכם ירא וסר מרע וכסיל מתעבר ובוטח 16
Mtu mwenye hekima huogopa na kutoka kwenye ubaya, bali mpumbavu huliacha onyo kwa ujasiri.
קצר-אפים יעשה אולת ואיש מזמות ישנא 17
Yeye ambaye anakuwa na hasira kwa haraka hufanya mambo ya kipumbavu, na mtu anayefanya hila mbaya huchukiwa.
נחלו פתאים אולת וערומים יכתרו דעת 18
Wajinga hurithi upumbavu, lakini watu wenye hekima wamezingirwa kwa maarifa.
שחו רעים לפני טובים ורשעים על-שערי צדיק 19
Hao ambao ni waovu watainama mbele yao walio wema na wale wenye uovu watasujudu kwenye malango ya wenye haki.
גם-לרעהו ישנא רש ואהבי עשיר רבים 20
Mtu masikini huchukiwa hata na marafiki zake, bali watu matajiri wanamarafiki wengi.
בז-לרעהו חוטא ומחונן עניים (ענוים) אשריו 21
Yeye ambaye huonyesha dharau kwa jirani yake anafanya dhambi, bali yule ambaye huonyesha fadhila kwa masikini anafuraha.
הלוא-יתעו חרשי רע וחסד ואמת חרשי טוב 22
Je wale wanaofanya njama mbaya hawapotei? Bali wale wenye mpango wa kutenda mema watapokea agano la uaminifu na udhamini
בכל-עצב יהיה מותר ודבר-שפתים אך-למחסור 23
Katika kazi zote ngumu huja faida, bali palipo na maongezi tu, huelekea kwenye umasikini.
עטרת חכמים עשרם אולת כסילים אולת 24
Taji ya watu wenye busara ni utajiri wao, bali upuuzi wa wapumbavu huwaletea upuu zaidi.
מציל נפשות עד אמת ויפח כזבים מרמה 25
Shahidi mkweli huokoa maisha, bali shahidi wa uongo hupumua uongo.
ביראת יהוה מבטח-עז ולבניו יהיה מחסה 26
Mtu anapokuwa na hofu ya Yehova, pia anakuwa na matumaini zaidi ndani yake; vitu hivi vitakuwa kama sehemu imara ya ulinzi kwa watoto wa mtu huyu.
יראת יהוה מקור חיים-- לסור ממקשי מות 27
Kumcha Yehova ni chemchemi ya uzima, ili kwamba mtu aweze kujiepusha kutoka katika mitego ya mauti.
ברב-עם הדרת-מלך ובאפס לאם מחתת רזון 28
Utukufu wa mfalme upo katika idadi kubwa ya watu wake, bali pasipo watu mfalme huangamia.
ארך אפים רב-תבונה וקצר-רוח מרים אולת 29
Mtu mvumilivu anaufahamu mkubwa, bali mtu mwepesi wa kuhamaki hukuza upuuzi.
חיי בשרים לב מרפא ורקב עצמות קנאה 30
Moyo wenye raha ni uzima wa mwili, bali husuda huozesha mifupa.
עשק דל חרף עשהו ומכבדו חנן אביון 31
Anayemkandamiza masikini humlaani Muumba wake, bali anayeonyesha fadhila kwa wahitaji humtukuza yeye.
ברעתו ידחה רשע וחסה במותו צדיק 32
Mtu mwovu huangushwa chini kwa matendo yake mabaya, bali mtu mwenye haki anakimbilio hata katika kifo.
בלב נבון תנוח חכמה ובקרב כסילים תודע 33
Hekima hukaa katika moyo wa ufahamu, bali hata miongoni mwa wapumbavu hujiachilia mwenyewe kwa kujulikana
צדקה תרומם-גוי וחסד לאמים חטאת 34
Kutenda haki huliinua taifa, bali dhambi ni chukizo kwa watu wowote.
רצון-מלך לעבד משכיל ועברתו תהיה מביש 35
Fadhila ya mfalme ni kwa mtumishi mwenye kutenda kwa hekima, bali hasira yake ni kwa yule atendaye kwa kuaibisha.

< מִשְׁלֵי 14 >