< מִשְׁלֵי 10 >

משלי שלמה בן חכם ישמח-אב ובן כסיל תוגת אמו 1
Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
לא-יועילו אוצרות רשע וצדקה תציל ממות 2
Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
לא-ירעיב יהוה נפש צדיק והות רשעים יהדף 3
Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
ראש--עשה כף-רמיה ויד חרוצים תעשיר 4
Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
אגר בקיץ בן משכיל נרדם בקציר בן מביש 5
Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
ברכות לראש צדיק ופי רשעים יכסה חמס 6
Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
זכר צדיק לברכה ושם רשעים ירקב 7
Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
חכם-לב יקח מצות ואויל שפתים ילבט 8
Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
הולך בתם ילך בטח ומעקש דרכיו יודע 9
Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
קרץ עין יתן עצבת ואויל שפתים ילבט 10
Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
מקור חיים פי צדיק ופי רשעים יכסה חמס 11
Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
שנאה תערר מדנים ועל כל-פשעים תכסה אהבה 12
Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
בשפתי נבון תמצא חכמה ושבט לגו חסר-לב 13
Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
חכמים יצפנו-דעת ופי-אויל מחתה קרבה 14
Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
הון עשיר קרית עזו מחתת דלים רישם 15
Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
פעלת צדיק לחיים תבואת רשע לחטאת 16
Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
ארח לחיים שומר מוסר ועזב תוכחת מתעה 17
Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
מכסה שנאה שפתי-שקר ומוצא דבה הוא כסיל 18
Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
ברב דברים לא יחדל-פשע וחושך שפתיו משכיל 19
Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
כסף נבחר לשון צדיק לב רשעים כמעט 20
Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
שפתי צדיק ירעו רבים ואוילים בחסר-לב ימותו 21
Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
ברכת יהוה היא תעשיר ולא-יוסף עצב עמה 22
Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
כשחוק לכסיל עשות זמה וחכמה לאיש תבונה 23
Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
מגורת רשע היא תבואנו ותאות צדיקים יתן 24
Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
כעבור סופה ואין רשע וצדיק יסוד עולם 25
Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
כחמץ לשנים--וכעשן לעינים כן העצל לשלחיו 26
Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
יראת יהוה תוסיף ימים ושנות רשעים תקצרנה 27
Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
תוחלת צדיקים שמחה ותקות רשעים תאבד 28
Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
מעוז לתם דרך יהוה ומחתה לפעלי און 29
Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
צדיק לעולם בל-ימוט ורשעים לא ישכנו-ארץ 30
Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
פי-צדיק ינוב חכמה ולשון תהפכות תכרת 31
Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
שפתי צדיק ידעון רצון ופי רשעים תהפכות 32
Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.

< מִשְׁלֵי 10 >