< מִשְׁלֵי 10 >
משלי שלמה בן חכם ישמח-אב ובן כסיל תוגת אמו | 1 |
Mithali za Solomoni: Mwana mwenye hekima huleta furaha kwa baba yake, lakini mwana mpumbavu huleta huzuni kwa mama yake.
לא-יועילו אוצרות רשע וצדקה תציל ממות | 2 |
Hazina zilizopatikana kwa njia mbaya hazifai, lakini uadilifu huokoa kutoka mautini.
לא-ירעיב יהוה נפש צדיק והות רשעים יהדף | 3 |
Bwana hawaachi waadilifu kukaa njaa, lakini hupinga tamaa ya mtu mwovu.
ראש--עשה כף-רמיה ויד חרוצים תעשיר | 4 |
Mikono mivivu hufanya mtu kuwa maskini lakini mikono yenye bidii huleta utajiri.
אגר בקיץ בן משכיל נרדם בקציר בן מביש | 5 |
Yeye akusanyaye mazao wakati wa kiangazi ni mwana mwenye hekima, lakini yeye alalaye wakati wa mavuno ni mwana mwenye kuaibisha.
ברכות לראש צדיק ופי רשעים יכסה חמס | 6 |
Baraka huwa taji kichwani mwa mwenye haki, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
זכר צדיק לברכה ושם רשעים ירקב | 7 |
Kumbukumbu ya mwenye haki itakuwa baraka, lakini jina la mwovu litaoza.
חכם-לב יקח מצות ואויל שפתים ילבט | 8 |
Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
הולך בתם ילך בטח ומעקש דרכיו יודע | 9 |
Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
קרץ עין יתן עצבת ואויל שפתים ילבט | 10 |
Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
מקור חיים פי צדיק ופי רשעים יכסה חמס | 11 |
Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
שנאה תערר מדנים ועל כל-פשעים תכסה אהבה | 12 |
Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
בשפתי נבון תמצא חכמה ושבט לגו חסר-לב | 13 |
Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
חכמים יצפנו-דעת ופי-אויל מחתה קרבה | 14 |
Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
הון עשיר קרית עזו מחתת דלים רישם | 15 |
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
פעלת צדיק לחיים תבואת רשע לחטאת | 16 |
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
ארח לחיים שומר מוסר ועזב תוכחת מתעה | 17 |
Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
מכסה שנאה שפתי-שקר ומוצא דבה הוא כסיל | 18 |
Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
ברב דברים לא יחדל-פשע וחושך שפתיו משכיל | 19 |
Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
כסף נבחר לשון צדיק לב רשעים כמעט | 20 |
Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
שפתי צדיק ירעו רבים ואוילים בחסר-לב ימותו | 21 |
Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
ברכת יהוה היא תעשיר ולא-יוסף עצב עמה | 22 |
Baraka ya Bwana hutajirisha, wala haichanganyi huzuni.
כשחוק לכסיל עשות זמה וחכמה לאיש תבונה | 23 |
Mpumbavu hufurahia tabia mbaya, lakini mtu mwenye ufahamu hupendezwa na hekima.
מגורת רשע היא תבואנו ותאות צדיקים יתן | 24 |
Kile anachoogopa mwovu ndicho kitakachompata; kile anachoonea shauku mwenye haki atapewa.
כעבור סופה ואין רשע וצדיק יסוד עולם | 25 |
Tufani inapopita, waovu hutoweka, lakini wenye haki husimama imara milele.
כחמץ לשנים--וכעשן לעינים כן העצל לשלחיו | 26 |
Kama siki ilivyo kwa meno na moshi kwa macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
יראת יהוה תוסיף ימים ושנות רשעים תקצרנה | 27 |
Kumcha Bwana huongeza urefu wa maisha, lakini miaka ya mwovu inafupishwa.
תוחלת צדיקים שמחה ותקות רשעים תאבד | 28 |
Tarajio la mwenye haki ni furaha, bali matumaini ya mwovu huwa si kitu.
מעוז לתם דרך יהוה ומחתה לפעלי און | 29 |
Njia ya Bwana ni kimbilio kwa wenye haki, lakini ni maangamizi ya wale watendao mabaya.
צדיק לעולם בל-ימוט ורשעים לא ישכנו-ארץ | 30 |
Kamwe wenye haki hawataondolewa, bali waovu hawatasalia katika nchi.
פי-צדיק ינוב חכמה ולשון תהפכות תכרת | 31 |
Kinywa cha mwenye haki hutoa hekima, bali ulimi wa upotovu utakatwa.
שפתי צדיק ידעון רצון ופי רשעים תהפכות | 32 |
Midomo ya wenye haki inajua kile kinachofaa, bali kinywa cha mwovu hujua kile kilichopotoka tu.