< במדבר 24 >
וירא בלעם כי טוב בעיני יהוה לברך את ישראל ולא הלך כפעם בפעם לקראת נחשים וישת אל המדבר פניו | 1 |
Balaamu alipooa kuwa ilimpendeza BWANA kubariki Israeli, hakwenda, kama hapo awali, kwa kutumia uganga, badala yake akatazama jangwani.
וישא בלעם את עיניו וירא את ישראל שכן לשבטיו ותהי עליו רוח אלהים | 2 |
Akayainua macho yake na kumwona Isreli akiwa kwenye kambi, kila mmoja kwa kabila yake, na Roho wa Mungu akamjia.
וישא משלו ויאמר נאם בלעם בנו בער ונאם הגבר שתם העין | 3 |
Akapokea huu unabii na kusema, “Balaamu mwana wa Beori anataka kusema, yeye ambaye macho yake yemefunuliwa sana.
נאם--שמע אמרי אל אשר מחזה שדי יחזה נפל וגלוי עינים | 4 |
Huongea na kusikia maneno ya Mungu. Huona maono toka kwa Mwenyezi, ambaye mbele zake humwinamia na macho yake yakiwa yamefumbuliwa.
מה טבו אהליך יעקב משכנתיך ישראל | 5 |
Jinsi zilivyo nzuri hema zako, ewe Yakobo, mahali unapoishi, Israeli!
כנחלים נטיו כגנת עלי נהר כאהלים נטע יהוה כארזים עלי מים | 6 |
Wamesambaa kama bonde, kama bustani zilizo pembezoni mwa mto, Kama miti ya mishubiri iliyopandwa na BWANA, ni kama mfano wa mielezi pembezoni mwa maji.
יזל מים מדליו וזרעו במים רבים וירם מאגג מלכו ותנשא מלכתו | 7 |
Maji yanatiririka katika ndoo zao, na mbegu zao zimemwagiwa maji vizuri. Mfalme wao atakuwa juu ya Agagi, na ufalme wao utaheshimiwa.
אל מוציאו ממצרים כתועפת ראם לו יאכל גוים צריו ועצמתיהם יגרם--וחציו ימחץ | 8 |
Mungu anamtoa Misri, na nguvu kama za nyati. Atawameza mataifa wanaopigana nao. Ataivunja mifupa yao katika vipande vipande. atawapiga kwa mishale yake.
כרע שכב כארי וכלביא מי יקימנו מברכיך ברוך וארריך ארור | 9 |
Ananyatia kama simba mume, na kamaa simba jike. Ni nani atakayejaribu kumsumbua? Kila mmoja anayembariki na abarikiwe; na kila mmoja anayemlaani na alaaniwe.”
ויחר אף בלק אל בלעם ויספק את כפיו ויאמר בלק אל בלעם לקב איבי קראתיך והנה ברכת ברך זה שלש פעמים | 10 |
Hasira za Balaki zikawaka dhidi ya Balaamu naye akaipiga mikono yake kwa pamoja. Balaki akamwambia Balaamu, “Nilkuita ili uwalaani maadui zangu, Lakini tazama, umewabariki mara tatu.
ועתה ברח לך אל מקומך אמרתי כבד אכבדך והנה מנעך יהוה מכבוד | 11 |
Kwa hiyo ondoka uende nyumbani uniache sasa hivi. Nilisema ningekupa zawadi kubwa sana, lakini BWANA amekuzuilia kupata zawadi.”
ויאמר בלעם אל בלק הלא גם אל מלאכיך אשר שלחת אלי--דברתי לאמר | 12 |
Ndipo Balaamu alipomjibu Balaki, “Niliwaambia wale wajumbe ulionitumia,
אם יתן לי בלק מלא ביתו כסף וזהב--לא אוכל לעבר את פי יהוה לעשות טובה או רעה מלבי אשר ידבר יהוה אתו אדבר | 13 |
'Hata kama Balaki atanipa ikulu yake ikiwa imejaa fedha na dhahabu, sitafanya zaidi ya maneno ya BWANA kwa lolote zuri au baya, au kwa chochote ambacho ningetaka kufanya. Ninaweza kusema kile tu ambacho BWANA ananiambia kusema,' Je, sikuwaambia haya?
ועתה הנני הולך לעמי לכה איעצך אשר יעשה העם הזה לעמך באחרית הימים | 14 |
Kwa hiyo sasa, tazama, nitarudi kwa watu wangu. Lakini kwanza nikuonye kile ambacho hawa watu watawafanyia watu wako katika siku zijazo.”
וישא משלו ויאמר נאם בלעם בנו בער ונאם הגבר שתם העין | 15 |
Balaamu alianza unabii huu. Akisema, “Balaamu mwana wa Beori anasema, Mtu yule aliyefumbuliwa macho yake.
נאם שמע אמרי אל וידע דעת עליון מחזה שדי יחזה נפל וגלוי עינים | 16 |
Huu ni unabii wa mtu alisikiaye neno la Mungu, aliye na maarifa toka kwake Yeye aliye juu, aliye na maono kutoka kwa Mwenyezi, Yeye ambaye humpigia magoti macho yakiwa yamefumbuliwa.
אראנו ולא עתה אשורנו ולא קרוב דרך כוכב מיעקב וקם שבט מישראל ומחץ פאתי מואב וקרקר כל בני שת | 17 |
Ninamwona, lakini hayuko hapa sasa. Ninamtazama, lakini siyo karibu. Nyota itatokea katika Yakobo, na fimbp ya enzi itatokea katika Israeli. Naye atawapigapiga viongozi wa Moabu na kuwaharibu wa uzao wa Sethi
והיה אדום ירשה והיה ירשה שעיר--איביו וישראל עשה חיל | 18 |
Ndipo Edomu atakapokuwa miliki ya Israeli, na Seiri pia itakuwa milki yao, maadui wa Israeli, ambao Israeli atawashinda kwa nguvu zake.
וירד מיעקב והאביד שריד מעיר | 19 |
Kutoka kwa Yakobo atatoka mfalme ambaye utawala wake naye atawaangamiza waliosalia katika mji.”
וירא את עמלק וישא משלו ויאמר ראשית גוים עמלק ואחריתו עדי אבד | 20 |
Kisha Balaamu akamtazama Amaleki na akaanza kutoa unabii wake. Alisema, “Amaleki alikuwa mkuu katika mataifa, lakini mwisho wake utakuwa uharibifu.”
וירא את הקיני וישא משלו ויאמר איתן מושבך ושים בסלע קנך | 21 |
Kisha Balaamu akawatazama Wakeni na akaanza kutoa unabii wake. Akasema, “Mahali unapoishi pana usalama, na viiota vyake viko kwenye miamba.
כי אם יהיה לבער קין--עד מה אשור תשבך | 22 |
Lakini pamoja na hayo, Kaini ataharibiwa na Ashuru atakapowachukua mateka.”
וישא משלו ויאמר אוי מי יחיה משמו אל | 23 |
Kisha Balaamu akanza unabii wake wa mwisho. Akasema, “Ole wake atakayesalia Mungu atakapoyafanya haya?
וצים מיד כתים וענו אשור וענו עבר וגם הוא עדי אבד | 24 |
Merikebu zitakuja toka pwani ya Kittimu; Zitaivamia Ashuru na kuiharibu Eberi, lakini wao pia wataishia kwenye uharibifu.”
ויקם בלעם וילך וישב למקמו וגם בלק הלך לדרכו | 25 |
Kisha Balaamu akainuka na kuondoka. Akarudi nyumbani kwake, na Balaki naye akaondoka.