< במדבר 2 >

וידבר יהוה אל משה ואל אהרן לאמר 1
Bwana aliwaambia Mose na Aroni:
איש על דגלו באתת לבית אבתם יחנו בני ישראל מנגד סביב לאהל מועד יחנו 2
“Waisraeli watapiga kambi zao kuzunguka Hema la Kukutania kwa umbali fulani kutoka kwenye hema, kila mwanaume chini ya alama yake pamoja na bendera ya jamaa yake.”
והחנים קדמה מזרחה דגל מחנה יהודה לצבאתם ונשיא לבני יהודה נחשון בן עמינדב 3
Kwa upande wa mashariki kuelekea mawio ya jua, kambi ya makundi ya Yuda watapiga kambi chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Yuda ni Nashoni mwana wa Aminadabu.
וצבאו ופקדיהם--ארבעה ושבעים אלף ושש מאות 4
Kundi lake lina watu 74,600.
והחנים עליו מטה יששכר ונשיא לבני יששכר נתנאל בן צוער 5
Kabila la Isakari watapiga kambi karibu na Yuda. Kiongozi wa watu wa Isakari ni Nethaneli mwana wa Suari.
וצבאו ופקדיו--ארבעה וחמשים אלף וארבע מאות 6
Kundi lake lina watu 54,400.
מטה זבולן ונשיא לבני זבולן אליאב בן חלן 7
Kabila la Zabuloni litafuata. Kiongozi wa watu wa Zabuloni ni Eliabu mwana wa Heloni.
וצבאו ופקדיו--שבעה וחמשים אלף וארבע מאות 8
Kundi lake lina watu 57,400.
כל הפקדים למחנה יהודה מאת אלף ושמנים אלף וששת אלפים וארבע מאות--לצבאתם ראשנה יסעו 9
Wanaume wote walio katika kambi ya Yuda, kufuatana na makundi yao, ni 186,400. Wao watatangulia kuondoka.
דגל מחנה ראובן תימנה לצבאתם ונשיא לבני ראובן אליצור בן שדיאור 10
Kwa upande wa kusini kutakuwa kambi ya makundi ya Reubeni chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Reubeni ni Elisuri mwana wa Shedeuri.
וצבאו ופקדיו--ששה וארבעים אלף וחמש מאות 11
Kundi lake lina watu 46,500.
והחונם עליו מטה שמעון ונשיא לבני שמעון שלמיאל בן צורישדי 12
Kabila la Simeoni watapiga kambi karibu na Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Surishadai.
וצבאו ופקדיהם--תשעה וחמשים אלף ושלש מאות 13
Kundi lake lina watu 59,300.
ומטה גד ונשיא לבני גד אליסף בן רעואל 14
Kabila la Gadi litafuata. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deueli.
וצבאו ופקדיהם--חמשה וארבעים אלף ושש מאות וחמשים 15
Kundi lake lina watu 45,650.
כל הפקדים למחנה ראובן מאת אלף ואחד וחמשים אלף וארבע מאות וחמשים--לצבאתם ושנים יסעו 16
Wanaume wote walio katika kambi ya Reubeni, kufuatana na makundi yao, ni 151,450. Nao watakuwa nafasi ya pili kuondoka.
ונסע אהל מועד מחנה הלוים בתוך המחנת כאשר יחנו כן יסעו איש על ידו לדגליהם 17
Kisha Hema la Kukutania na kambi ya Walawi vitakuwa katikati ya kambi zote. Wao watasafiri kwa utaratibu ule ule kama walivyopiga kambi, kila mmoja mahali pake mwenyewe chini ya alama yake.
דגל מחנה אפרים לצבאתם ימה ונשיא לבני אפרים אלישמע בן עמיהוד 18
Upande wa magharibi kutakuwepo na kambi ya makundi ya Efraimu chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi.
וצבאו ופקדיהם--ארבעים אלף וחמש מאות 19
Kundi lake lina watu 40,500.
ועליו מטה מנשה ונשיא לבני מנשה גמליאל בן פדהצור 20
Kabila la Manase litafuata baada ya Efraimu. Kiongozi wa watu wa Manase ni Gamalieli mwana wa Pedasuri.
וצבאו ופקדיהם--שנים ושלשים אלף ומאתים 21
Kundi lake lina watu 32,200.
ומטה בנימן ונשיא לבני בנימן אבידן בן גדעני 22
Kabila la Benyamini litafuata baada ya Manase. Kiongozi wa watu wa Benyamini ni Abidani mwana wa Gideoni.
וצבאו ופקדיהם--חמשה ושלשים אלף וארבע מאות 23
Kundi lake lina watu 35,400.
כל הפקדים למחנה אפרים מאת אלף ושמנת אלפים ומאה--לצבאתם ושלשים יסעו 24
Wanaume wote walio katika kambi ya Efraimu kufuatana na makundi yao ni 108,100. Nao watakuwa nafasi ya tatu kuondoka.
דגל מחנה דן צפנה לצבאתם ונשיא לבני דן אחיעזר בן עמישדי 25
Upande wa kaskazini kutakuwa na makundi ya kambi ya Dani, chini ya alama yao. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai.
וצבאו ופקדיהם--שנים וששים אלף ושבע מאות 26
Kundi lake lina watu 62,700.
והחנים עליו מטה אשר ונשיא לבני אשר פגעיאל בן עכרן 27
Kabila la Asheri watapiga kambi karibu na Dani. Kiongozi wa watu wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okrani.
וצבאו ופקדיהם--אחד וארבעים אלף וחמש מאות 28
Kundi lake lina watu 41,500.
ומטה נפתלי ונשיא לבני נפתלי אחירע בן עינן 29
Kabila la Naftali litafuata. Kiongozi wa watu wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani.
וצבאו ופקדיהם--שלשה וחמשים אלף וארבע מאות 30
Kundi lake lina watu 53,400.
כל הפקדים למחנה דן--מאת אלף ושבעה וחמשים אלף ושש מאות לאחרנה יסעו לדגליהם 31
Wanaume wote walio katika kambi ya Dani ni 157,600. Wao watakuwa wa mwisho kuondoka chini ya alama yao.
אלה פקודי בני ישראל לבית אבתם כל פקודי המחנת לצבאתם--שש מאות אלף ושלשת אלפים וחמש מאות וחמשים 32
Hawa ndio Waisraeli, wakiwa wamehesabiwa kufuatana na jamaa zao. Wote walio kambini kwa makundi yao ni watu 603,550.
והלוים--לא התפקדו בתוך בני ישראל כאשר צוה יהוה את משה 33
Hata hivyo, Walawi hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
ויעשו בני ישראל ככל אשר צוה יהוה את משה כן חנו לדגליהם וכן נסעו--איש למשפחתיו על בית אבתיו 34
Kwa hiyo Waisraeli wakafanya kila kitu Bwana alichomwamuru Mose. Hivyo ndivyo walivyopiga kambi chini ya alama zao, pia hivyo ndivyo walivyoondoka, kila mmoja akiwa na ukoo wake na jamaa yake.

< במדבר 2 >