< במדבר 10 >
עשה לך שתי חצוצרת כסף--מקשה תעשה אתם והיו לך למקרא העדה ולמסע את המחנות | 2 |
“Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka.
ותקעו בהן--ונועדו אליך כל העדה אל פתח אהל מועד | 3 |
Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania.
ואם באחת יתקעו--ונועדו אליך הנשיאים ראשי אלפי ישראל | 4 |
Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako.
ותקעתם תרועה--ונסעו המחנות החנים קדמה | 5 |
Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka.
ותקעתם תרועה שנית--ונסעו המחנות החנים תימנה תרועה יתקעו למסעיהם | 6 |
Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka.
ובהקהיל את הקהל--תתקעו ולא תריעו | 7 |
Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.
ובני אהרן הכהנים יתקעו בחצצרות והיו לכם לחקת עולם לדרתיכם | 8 |
“Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo.
וכי תבאו מלחמה בארצכם על הצר הצרר אתכם--והרעתם בחצצרת ונזכרתם לפני יהוה אלהיכם ונושעתם מאיביכם | 9 |
Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu.
וביום שמחתכם ובמועדיכם ובראשי חדשיכם--ותקעתם בחצצרת על עלתיכם ועל זבחי שלמיכם והיו לכם לזכרון לפני אלהיכם אני יהוה אלהיכם | 10 |
Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”
ויהי בשנה השנית בחדש השני--בעשרים בחדש נעלה הענן מעל משכן העדת | 11 |
Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda.
ויסעו בני ישראל למסעיהם ממדבר סיני וישכן הענן במדבר פארן | 12 |
Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani.
ויסעו בראשנה על פי יהוה ביד משה | 13 |
Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.
ויסע דגל מחנה בני יהודה בראשנה--לצבאתם ועל צבאו--נחשון בן עמינדב | 14 |
Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao.
ועל צבא--מטה בני יששכר נתנאל בן צוער | 15 |
Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari,
ועל צבא--מטה בני זבולן אליאב בן חלן | 16 |
naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni.
והורד המשכן ונסעו בני גרשון ובני מררי נשאי המשכן | 17 |
Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.
ונסע דגל מחנה ראובן--לצבאתם ועל צבאו--אליצור בן שדיאור | 18 |
Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao.
ועל צבא--מטה בני שמעון שלמיאל בן צורישדי | 19 |
Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni,
ועל צבא מטה בני גד אליסף בן דעואל | 20 |
naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi.
ונסעו הקהתים נשאי המקדש והקימו את המשכן עד באם | 21 |
Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.
ונסע דגל מחנה בני אפרים--לצבאתם ועל צבאו--אלישמע בן עמיהוד | 22 |
Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao.
ועל צבא--מטה בני מנשה גמליאל בן פדהצור | 23 |
Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase,
ועל צבא--מטה בני בנימן אבידן בן גדעוני | 24 |
naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.
ונסע דגל מחנה בני דן--מאסף לכל המחנת לצבאתם ועל צבאו--אחיעזר בן עמישדי | 25 |
Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao.
ועל צבא--מטה בני אשר פגעיאל בן עכרן | 26 |
Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri,
ועל צבא--מטה בני נפתלי אחירע בן עינן | 27 |
naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali.
אלה מסעי בני ישראל לצבאתם ויסעו | 28 |
Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.
ויאמר משה לחבב בן רעואל המדיני חתן משה נסעים אנחנו אל המקום אשר אמר יהוה אתו אתן לכם לכה אתנו והטבנו לך כי יהוה דבר טוב על ישראל | 29 |
Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”
ויאמר אליו לא אלך כי אם אל ארצי ואל מולדתי אלך | 30 |
Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”
ויאמר אל נא תעזב אתנו כי על כן ידעת חנתנו במדבר והיית לנו לעינים | 31 |
Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu.
והיה כי תלך עמנו והיה הטוב ההוא אשר ייטיב יהוה עמנו--והטבנו לך | 32 |
Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”
ויסעו מהר יהוה דרך שלשת ימים וארון ברית יהוה נסע לפניהם דרך שלשת ימים לתור להם מנוחה | 33 |
Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika.
וענן יהוה עליהם יומם בנסעם מן המחנה ] | 34 |
Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.
ויהי בנסע הארן ויאמר משה קומה יהוה ויפצו איביך וינסו משנאיך מפניך | 35 |
Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema, “Ee Bwana, inuka! Watesi wako na watawanyike; adui zako na wakimbie mbele zako.”
ובנחה יאמר שובה יהוה רבבות אלפי ישראל ] | 36 |
Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema, “Ee Bwana, rudi, kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”