< איכה 5 >
זכר יהוה מה היה לנו הביט (הביטה) וראה את חרפתנו | 1 |
Kumbuka, Yahweh, yaliyo tutokea na uone aibu yetu.
נחלתנו נהפכה לזרים בתינו לנכרים | 2 |
Urithi wetu umegeuziwa kwa wageni; nyumba zetu kwa wageni.
יתומים היינו אין (ואין) אב אמתינו כאלמנות | 3 |
Tumekuwa yatima, bila baba, na mama zetu ni kama wajane.
מימינו בכסף שתינו עצינו במחיר יבאו | 4 |
Lazima tulipe fedha kwa maji tunayo kunywa, na tulipe fedha kupata mbao zetu.
על צוארנו נרדפנו יגענו לא (ולא) הונח לנו | 5 |
Hao wanakuja kwetu wamekaribia nyuma yetu; tumechoka na hatuwezi pata mapumziko.
מצרים נתנו יד אשור לשבע לחם | 6 |
Tumejitoa kwa Misri na kwa Assiria tupate chakula cha kutosha.
אבתינו חטאו אינם (ואינם) אנחנו (ואנחנו) עונתיהם סבלנו | 7 |
Baba zetu walifanya dhambi, na hawapo tena, na tumebeba dhambi zao.
עבדים משלו בנו פרק אין מידם | 8 |
Watumwa walitutawala, na hakuna wa kutuokoa na mikono yao.
בנפשנו נביא לחמנו מפני חרב המדבר | 9 |
Tunapata mkate wetu pale tunapo hatarisha maisha, kwasababu ya upanga wa nyikani.
עורנו כתנור נכמרו מפני זלעפות רעב | 10 |
Ngozi zetu zimekuwa na moto kama jiko kwasababu ya joto la njaa.
נשים בציון ענו בתלת בערי יהודה | 11 |
Wanawake wanabakwa Sayuni, na mabikra katika mji wa Yuda.
שרים בידם נתלו פני זקנים לא נהדרו | 12 |
Watoto wa mfalme wamenyongwa na mikono yao, na hakuna heshima inayoonyeshwa kwa wazee.
בחורים טחון נשאו ונערים בעץ כשלו | 13 |
Wanaume vijana wanalizimishwa kusaga mbegu kwa jiwe la kusagia, na wavulana wanajikwa chini ya vifurushi vya kuni.
זקנים משער שבתו בחורים מנגינתם | 14 |
Wazee wameacha lango la mji, na vijana wameacha miziki.
שבת משוש לבנו נהפך לאבל מחלנו | 15 |
Furaha ya moyo imekoma na kucheza kwetu kumegeuka kilio.
נפלה עטרת ראשנו אוי נא לנו כי חטאנו | 16 |
Taji limeanguka kichwani mwetu; ole wetu, kwa kuwa tumetenda dhambi!
על זה היה דוה לבנו--על אלה חשכו עינינו | 17 |
Kwa kuwa moyo wetu umekuwa unaumwa, na machozi yetu ya fifia, kwa vitu hivi macho yetu yanafifia
על הר ציון ששמם שועלים הלכו בו | 18 |
maana Mlima Sayuni umelala ukiwa, mbwa wa mitaani wacheza juu yake.
אתה יהוה לעולם תשב כסאך לדור ודור | 19 |
Lakini wewe, Yahweh, unatawala milele, na utaketi katika kiti chako cha enzi vizazi na vizazi. Kwanini unatusahau milele?
למה לנצח תשכחנו תעזבנו לארך ימים | 20 |
Kwanini unatutelekeza kwa siku nyingi?
השיבנו יהוה אליך ונשוב (ונשובה) חדש ימינו כקדם | 21 |
Turejeshe kwako, Yahweh, na sisi tutarejea. Fanya upya siku zetu kama zilivyo kuwa hapo zamani -
כי אם מאס מאסתנו קצפת עלינו עד מאד | 22 |
vinginevyo labda uwe umetukataa na una hasira kwetu kupita kiasi.