< יהושע 15 >

ויהי הגורל למטה בני יהודה--למשפחתם אל גבול אדום מדבר צן נגבה מקצה תימן 1
Ugawanaji wa nchi kwa kabila la watu wa Yuda, walipewa kwa kufuatana na koo zao, kutoka upande wa kusini hadi mpaka wa Edomu, pamoja na nyika ya Sini iliyokuwa mbali sana kuelekea kusini.
ויהי להם גבול נגב מקצה ים המלח מן הלשן הפנה נגבה 2
Mpaka wao wa upande wa kusini ulianzia mwisho wa Bahari ya Chumvi, kutoka ghuba iliyokabili upande wa kusini.
ויצא אל מנגב למעלה עקרבים ועבר צנה ועלה מנגב לקדש ברנע ועבר חצרון ועלה אדרה ונסב הקרקעה 3
Mpaka wao mwingine ulielekea upande wa kusini wa mlima wa Akrabimu na kupita kuelekea Sini, na kupanda upande wa Kadeshi Barnea, karibu na Hezroni, hadi Addari mahali ambapo ulipinda kuelekea Karika.
ועבר עצמונה ויצא נחל מצרים והיה (והיו) תצאות הגבול ימה זה יהיה לכם גבול נגב 4
Ulipita katika Azimoni, kuelekea kijito cha Misri, na mwisho ulikuwa katika bahari. Huu ulikuwa ni mpaka wa kusini.
וגבול קדמה ים המלח עד קצה הירדן וגבול לפאת צפונה מלשון הים מקצה הירדן 5
Mpaka wa mashariki ulikuwa ni Bahari ya Chumvi, katika mdomo wa Yordani. Mpaka wa upande wa kasikazini ulianzia katika ghuba ya bahari katika mdomo wa Yordani.
ועלה הגבול בית חגלה ועבר מצפון לבית הערבה ועלה הגבול אבן בהן בן ראובן 6
Ulielekea mpaka Bethi Hogla na ulipita kaskazini mwa Bethi Araba. Kisha ulipanda hata JIwe la Bohani mwana wa Rubeni.
ועלה הגבול דברה מעמק עכור וצפונה פנה אל הגלגל אשר נכח למעלה אדמים אשר מנגב לנחל ועבר הגבול אל מי עין שמש והיו תצאתיו אל עין רגל 7
Basi mpaka ule ulienda hadi Debiri kutoka katika bonde la Akori, kuelekea upande wa kasikazini, kuendelea hadi Giligali, ambayo iko mkabala na mlima Adumimu, iliyo upande wa kusini wa bonde. Kisha mpaka uliendelea hata katika chemichemi za Eni Shemeshi na kufika Eni Rogeli.
ועלה הגבול גי בן הנם אל כתף היבוסי מנגב--היא ירושלם ועלה הגבול אל ראש ההר אשר על פני גי הנם ימה אשר בקצה עמק רפאים צפונה 8
kisha mpaka ulishuka hadi bonde la Beni Hinomu kuelekea upande wa kusini wa mji wa Wayebusi ( ambao ni Yerusalemu). Kisha ulipanda hata katika mlima ulio juu ya bonde la Hinomu, katika upande wa magharibi, ulio mwishoni mwa bonde la Refaimu katika upande wa kasikazini.
ותאר הגבול מראש ההר אל מעין מי נפתוח ויצא אל ערי הר עפרון ותאר הגבול בעלה היא קרית יערים 9
Kisha mpaka ulitanuka kutoka katika kilele cha milima hata chemichemi ya Nefutoa, na ulipanda kutoka hapo kuelekea miji ya Mlima Efroni. Kisha mpaka ulipiga kona kuelekea Baala ( ambao ndio Kiriathi Yearimu).
ונסב הגבול מבעלה ימה אל הר שעיר ועבר אל כתף הר יערים מצפונה היא כסלון וירד בית שמש ועבר תמנה 10
Baadaye mpaka ulizunguka kuelekea magharibi mwa Baala kukabili Mlima Seiri, na kupita kufuata upande wa Mlima wa Yearimu katika upande wa kasikazini (ambao ndio Kesaloni), ulienda chini hadi Bethi Shemeshi na kuvuka hata ng'ambo ya Timna.
ויצא הגבול אל כתף עקרון צפונה ותאר הגבול שכרונה ועבר הר הבעלה ויצא יבנאל והיו תצאות הגבול ימה 11
Mpaka uliendelea karibu na mlima wa kasikazini mwa mlima wa Ekroni, na kisha ukakata kona kuzunguka Shikeroni na kupita kuelekea sambasamba na Mlima Baala, kutoka hapo uliendelea hadi Yabneeli. Mpaka ule ulikomea katika bahari.
וגבול ים הימה הגדול וגבול זה גבול בני יהודה סביב--למשפחתם 12
Mpaka wa magharibi ulikuwa Bahari Kuu na katika ukanda wa pwani yake. Huu ndio mpaka uliozunguka kabila la Yuda, ukoo kwa ukoo.
ולכלב בן יפנה נתן חלק בתוך בני יהודה אל פי יהוה ליהושע--את קרית ארבע אבי הענק היא חברון 13
Katika kulitunza agizo la Yahweh kwa Yoshua, Yoshua alimpa Kalebu mwana wa Yefune mgao wa nchi ya. miongoni mwa kabila la Yuda, alimgawia nchi Kiriathi Arba, ambayo ndio Hebroni (Arba alikuwa ni baba wa Anaki).
וירש משם כלב את שלושה בני הענק--את ששי ואת אחימן ואת תלמי ילידי הענק 14
Kalebu aliwafukuzia mbali wana watatu wa Anaki: Sheshai, Ahimani na Talmai, wazawa wa Anaki.
ויעל משם אל ישבי דבר ושם דבר לפנים קרית ספר 15
Alipanda kutoka pale kinyume cha wenyeji wa Debiri (Debiri hapo mwanzo iliitwa Kiriathi Seferi).
ויאמר כלב אשר יכה את קרית ספר ולכדה--ונתתי לו את עכסה בתי לאשה 16
Kalebu akasema, “Mtu atakayeishambulia Kiriathi Seferi na kuiteka, nitampa binti yangau, Akisa, awe mke wake.
וילכדה עתניאל בן קנז אחי כלב ויתן לו את עכסה בתו לאשה 17
Wakati huo Othinieli mwana wa Kenazi, kaka yake na Kalebu, aliuteka mji, na Kalebu alimpatia Akisa, binti yake awe mke wake.
ויהי בבואה ותסיתהו לשאול מאת אביה שדה ותצנח מעל החמור ויאמר לה כלב מה לך 18
Mara baada ya hayo, Akisa alienda kwa Othinieli na alimsihi amwombe baba yake shamba. Na mara aliposhuka kutoka katika punda wake, Kalebu alimwambia Akisa, “Unataka nini?”
ותאמר תנה לי ברכה כי ארץ הנגב נתתני ונתתה לי גלת מים ויתן לה את גלת עליות ואת גלת תחתיות 19
Akisa akamjibu, “Nifanyie neema. Kwa kuwa umeshanipa nchi ya Negevu, nipe pia baadhi ya chemichemi za maji.” Na Kalebu alimpa chemichemi ya juu na chemichemi ya chini.
זאת נחלת מטה בני יהודה--למשפחתם 20
Huu ulikuwa ndio urithi wa kabila la Yuda, waliopewa kufuatana na koo zao.
ויהיו הערים מקצה למטה בני יהודה אל גבול אדום בנגבה--קבצאל ועדר ויגור 21
Miji iliyo mali ya kabila la Yuda katika upande wa kusini, kuelekea mpaka wa Edomu, ilikuwa ni Kabzeeli, Eda, Yaguri,
וקינה ודימונה ועדעדה 22
Kina, Dimona, Adada,
וקדש וחצור ויתנן 23
Kadeshi, Hazor, Ithinani,
זיף וטלם ובעלות 24
Zifu, Telemu, Bealothi.
וחצור חדתה וקריות חצרון היא חצור 25
Hazori Hadata, Keriothi Hezroni (mji huu ulijulikana kama Hazori),
אמם ושמע ומולדה 26
Amamu, shema, Molada,
וחצר גדה וחשמון ובית פלט 27
Hazari Gada, Heshimoni, Bethi Peleti,
וחצר שועל ובאר שבע ובזיותיה 28
Hazari Shuali, Beerisheba, Biziothia.
בעלה ועיים ועצם 29
Baala, Limu, Ezemu,
ואלתולד וכסיל וחרמה 30
Eltoladi, Kesili, Horma,
וצקלג ומדמנה וסנסנה 31
Ziklagi, Madimana, Sansana,
ולבאות ושלחים ועין ורמון כל ערים עשרים ותשע וחצריהן 32
Lebaothi, Shilihimu, Aini, na Rimoni. Miji hii ilikuwa ishirini na tisa kwa ujumla, kujumlisha na vijiji vyake.
בשפלה--אשתאול וצרעה ואשנה 33
Katika nchi iliyo chini ya mlima upande wa magharibi, kulikuwa na miji ya Eshtaoli, Zora, Ashina,
וזנוח ועין גנים תפוח והעינם 34
Zanaoa, Eni Ganimu, Tapua, Enamu,
ירמות ועדלם שוכה ועזקה 35
Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka,
ושערים ועדיתים והגדרה וגדרתים ערים ארבע עשרה וחצריהן 36
Shaaraimu, Adithaimu, na Gedera ( ambayo ndio Gederothaimu). Hesabu ya miji hii ilikuwa ni kumi na nne, pamoja na vijiji vyao.
צנן וחדשה ומגדל גד 37
Zena, Hadasha, Migidagadi,
ודלען והמצפה ויקתאל 38
Dileani, Mizipa, Yokitheeli,
לכיש ובצקת ועגלון 39
Lakishi, Bozikathi, Egloni.
וכבון ולחמס וכתליש 40
Kaboni, Lahmamu, Kitilishi,
וגדרות בית דגון ונעמה ומקדה ערים שש עשרה וחצריהן 41
Gederothi, Bethi Dagoni, Naama, Makeda. Hesabu ya miji hii ilikuwa kumi na sita, kujumlisha na vijiji vyao.
לבנה ועתר ועשן 42
Libna, Etheri, Ashani,
ויפתח ואשנה ונציב 43
Ifuta, Ashina, Nezibu,
וקעילה ואכזיב ומראשה ערים תשע וחצריהן 44
Keila, Akizibu, na Maresha. Hii ilikuwa ni miji tisa, kujumlisha na vijiji vyao.
עקרון ובנתיה וחצריה 45
Ekroni, pamoja na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka;
מעקרון וימה כל אשר על יד אשדוד וחצריהן 46
kutoka Ekroni kuelekea Bahari Kuu, makazi yote ambayo yalikuwa karibu na Ashidodi, pamoja na vijiji vyake.
אשדוד בנותיה וחצריה עזה בנותיה וחצריה--עד נחל מצרים והים הגבול (הגדול) וגבול 47
Ashidodi, na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; Gaza na miji na vijiji vyake vinavyoizunguka; hata kufika kijito cha Misri, na kuelekea Bahari Kuu pamoja na ukanda wake wa pwani.
ובהר--שמיר ויתיר ושוכה 48
Katika nchi ya milima, kuna miji ya Shamiri, Yatiri, Soko,
ודנה וקרית סנה היא דבר 49
Dana, Kiriathi Sana (ambayo ndio Debiri),
וענב ואשתמה וענים 50
Anabu, Eshitemo, Animu,
וגשן וחלן וגלה ערים אחת עשרה וחצריהן 51
Gosheni, Holoni, na Gilo. Hii ilikuwa ni miji kumi na moja, kujumuisha na vijiji vyake.
ארב ורומה ואשען 52
Arabu, Duma, Ehani,
וינים (וינום) ובית תפוח ואפקה 53
Yanimu, Bethi Tapua, Afeka,
וחמטה וקרית ארבע היא חברון--וציער ערים תשע וחצריהן 54
Humta, Kiriathi Arba (ambayo ndio Hebroni), na Ziori. Hii ilikuwa miji tisa, pamoja na vijiji vyake.
מעון כרמל וזיף ויוטה 55
Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta,
ויזרעאל ויקדעם וזנוח 56
Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa,
הקין גבעה ותמנה ערים עשר וחצריהן 57
Kaini, Gibea, na Timna. Hii ilikuwa ni miji kumi, kujumuisha na vijiji vyake.
חלחול בית צור וגדור 58
Halhuli, Bethi Zuri, Gedori,
ומערת ובית ענות ואלתקן ערים שש וחצריהן 59
Maarathi, Bethi Anothi, na Elitekoni. Hii ilikuwa miji sita, pamoja na vijiji vyake.
קרית בעל היא קרית יערים--והרבה ערים שתים וחצריהן 60
Kiriathi Baali (ambayo ndio Kiriathi Yearimu), na Raba. Hii ilikuwa ni miji miwili, pamoja na vijiji vyake.
במדבר--בית הערבה מדין וסככה 61
Katika nyika, kulikuwa na miji ya Bethi Araba, Midini, Sekaka,
והנבשן ועיר המלח ועין גדי ערים שש וחצריהן 62
Nibushani, mji wa chumvi, na Eni Gedi. Hii ilikuwa miji, pamoja na vijiji vyao.
ואת היבוסי יושבי ירושלם לא יוכלו (יכלו) בני יהודה להורישם וישב היבוסי את בני יהודה בירושלם עד היום הזה 63
Lakini kwa Wayebusi, wenyeji wa Yerusalemu, kabila la Yuda halikuweza kuwafukuza, na hivyo, Wayebusi wanaishi pamoja na kabila la Yuda hadi leo hii.

< יהושע 15 >