< איוב 7 >

הלא-צבא לאנוש על- (עלי-) ארץ וכימי שכיר ימיו 1
“Je, mwanadamu hana kazi ngumu duniani? Siku zake si kama zile za mtu aliyeajiriwa?
כעבד ישאף-צל וכשכיר יקוה פעלו 2
Kama mtumwa anavyovionea shauku vivuli vya jioni, au mtu aliyeajiriwa anavyoungojea mshahara wake,
כן הנחלתי לי ירחי-שוא ולילות עמל מנו-לי 3
ndivyo nilivyogawiwa miezi ya ubatili, nami nimeandikiwa huzuni usiku hata usiku.
אם-שכבתי-- ואמרתי מתי אקום ומדד-ערב ושבעתי נדדים עדי-נשף 4
Wakati nilalapo ninawaza, ‘Itachukua muda gani kabla sijaamka?’ Usiku huwa mrefu, nami najigeuzageuza hadi mapambazuko.
לבש בשרי רמה וגיש (וגוש) עפר עורי רגע וימאס 5
Mwili wangu umevikwa mabuu na uchafu, ngozi yangu imetumbuka na kutunga usaha.
ימי קלו מני-ארג ויכלו באפס תקוה 6
“Siku zangu zinapita upesi kuliko mtande wa kufuma, nazo zinafikia mwisho wake bila matumaini.
זכר כי-רוח חיי לא-תשוב עיני לראות טוב 7
Kumbuka, Ee Mungu, maisha yangu ni kama pumzi; macho yangu kamwe hayataona tena raha.
לא-תשורני עין ראי עיניך בי ואינני 8
Lile jicho linaloniona sasa halitaniona tena; utanitafuta, wala sitakuwepo.
כלה ענן וילך כן יורד שאול לא יעלה (Sheol h7585) 9
Kama vile wingu liondokavyo na kutoweka, vivyo hivyo yeye ashukaye kaburini harudi tena. (Sheol h7585)
לא-ישוב עוד לביתו ולא-יכירנו עוד מקמו 10
Kamwe harudi tena nyumbani mwake; wala mahali pake hapatamjua tena.
גם-אני לא אחשך-פי אדברה בצר רוחי אשיחה במר נפשי 11
“Kwa hiyo sitanyamaza; nitanena kutokana na maumivu makuu ya roho yangu, nitalalama kwa uchungu wa nafsi yangu.
הים-אני אם-תנין כי-תשים עלי משמר 12
Je, mimi ni bahari, au mnyama mkubwa mno akaaye vilindini, hata uniweke chini ya ulinzi?
כי-אמרתי תנחמני ערשי ישא בשיחי משכבי 13
Ninapofikiri kwamba kitanda changu kitanifariji, nacho kiti changu cha fahari kitapunguza malalamiko yangu,
וחתתני בחלמות ומחזינות תבעתני 14
ndipo wanitisha kwa ndoto na kunitia hofu kwa maono,
ותבחר מחנק נפשי מות מעצמותי 15
hivyo ninachagua kujinyonga na kufa, kuliko huu mwili wangu.
מאסתי לא-לעלם אחיה חדל ממני כי-הבל ימי 16
Ninayachukia maisha yangu; nisingetamani kuendelea kuishi. Niache; siku zangu ni ubatili.
מה-אנוש כי תגדלנו וכי-תשית אליו לבך 17
“Mwanadamu ni kitu gani hata umjali kiasi hiki, kwamba unamtia sana maanani,
ותפקדנו לבקרים לרגעים תבחננו 18
kwamba unamwangalia kila asubuhi na kumjaribu kila wakati?
כמה לא-תשעה ממני לא-תרפני עד-בלעי רקי 19
Je, hutaacha kamwe kunitazama, au kuniacha japo kwa kitambo kidogo tu?
חטאתי מה אפעל לך-- נצר האדם למה שמתני למפגע לך ואהיה עלי למשא 20
Ikiwa nimetenda dhambi, nimekufanyia nini, Ewe mlinzi wa wanadamu? Kwa nini umeniweka niwe shabaha yako? Je, nimekuwa mzigo kwako?
ומה לא-תשא פשעי-- ותעביר את-עוני כי-עתה לעפר אשכב ושחרתני ואינני 21
Kwa nini husamehi makosa yangu na kuachilia dhambi zangu? Kwa kuwa hivi karibuni nitalala mavumbini; nawe utanitafuta, wala sitakuwepo.”

< איוב 7 >