< איוב 5 >

קרא-נא היש עונך ואל-מי מקדשים תפנה 1
Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
כי-לאויל יהרג-כעש ופתה תמית קנאה 2
Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
אני-ראיתי אויל משריש ואקוב נוהו פתאם 3
Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
ירחקו בניו מישע וידכאו בשער ואין מציל 4
Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
אשר קצירו רעב יאכל--ואל-מצנים יקחהו ושאף צמים חילם 5
Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
כי לא-יצא מעפר און ומאדמה לא-יצמח עמל 6
Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
כי-אדם לעמל יולד ובני-רשף יגביהו עוף 7
Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
אולם--אני אדרש אל-אל ואל-אלהים אשים דברתי 8
Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
עשה גדלות ואין חקר נפלאות עד-אין מספר 9
yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
הנתן מטר על-פני-ארץ ושלח מים על-פני חוצות 10
Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
לשום שפלים למרום וקדרים שגבו ישע 11
Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
מפר מחשבות ערומים ולא-תעשנה ידיהם תשיה 12
Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
לכד חכמים בערמם ועצת נפתלים נמהרה 13
Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
יומם יפגשו-חשך וכלילה ימששו בצהרים 14
Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
וישע מחרב מפיהם ומיד חזק אביון 15
Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
ותהי לדל תקוה ועלתה קפצה פיה 16
Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
הנה אשרי אנוש יוכחנו אלוה ומוסר שדי אל-תמאס 17
Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
כי הוא יכאיב ויחבש ימחץ וידו תרפינה 18
Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
בשש צרות יצילך ובשבע לא-יגע בך רע 19
Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
ברעב פדך ממות ובמלחמה מידי חרב 20
Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
בשוט לשון תחבא ולא-תירא משד כי יבוא 21
Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
לשד ולכפן תשחק ומחית הארץ אל-תירא 22
Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
כי עם-אבני השדה בריתך וחית השדה השלמה-לך 23
Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
וידעת כי-שלום אהלך ופקדת נוך ולא תחטא 24
Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
וידעת כי-רב זרעך וצאצאיך כעשב הארץ 25
Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
תבוא בכלח אלי-קבר כעלות גדיש בעתו 26
Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
הנה-זאת חקרנוה כן-היא שמענה ואתה דע-לך 27
Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”

< איוב 5 >