< איוב 35 >
Aidha, Elihu aliendelea kusema,
הזאת חשבת למשפט אמרת צדקי מאל | 2 |
“Je unadhani hii ni sawa unaposema, 'Haki yangu mbele ya Mungu?
כי-תאמר מה-יסכן-לך מה-אעיל מחטאתי | 3 |
Kwa kuwa unauliza, 'Inafaa nini kwangu' na 'Ingekuwa nzuri kwangu kama ningekuwa nimetenda dhambi?'
אני אשיבך מלין-- ואת-רעיך עמך | 4 |
Nitakujibu, wewe pamoja na marafiki zako.
הבט שמים וראה ושור שחקים גבהו ממך | 5 |
Tazama juu angani, na ulione; angalia anga, ambalo liko juu sana kuliko wewe.
אם-חטאת מה-תפעל-בו ורבו פשעיך מה-תעשה-לו | 6 |
Kama umetenda dhambi, ni madhara gani huwa unayafanya kwa Mungu? Ikiwa makosa yako yameongezeka zaidi, je huwa unafanya nini kwake?
אם-צדקת מה-תתן-לו או מה-מידך יקח | 7 |
Kama wewe ni mwenye haki, unaweza kumpa nini? Je atapokea nini mkononi mwako?
לאיש-כמוך רשעך ולבן-אדם צדקתך | 8 |
Uovu wako waweza kuwaumiza mtu, kama ulivyo wewe ni mtu, na haki yako yaweza kumnufaisha mwana mwingine wa mtu.
מרב עשוקים יזעיקו ישועו מזרוע רבים | 9 |
Watu wanalia kwasababu ya matendo mengi ya unyanyasaji; wanaomba msaada katika mikono ya watu wenye nguvu.
ולא-אמר--איה אלוה עשי נתן זמרות בלילה | 10 |
Lakini hakuna hata mmoja asemaye, ' Mungu Muumba wangu yuko wapi, ambaye hutoa nyimbo wakati wa usiku,
מלפנו מבהמות ארץ ומעוף השמים יחכמנו | 11 |
ambaye hutufundisha sisi zaidi anavyowafundisha wanyama wa dunia, na ambaye hutufanya sisi kuwa wenye hekima kuliko ndege wa angani?
שם יצעקו ולא יענה-- מפני גאון רעים | 12 |
Huko wanalia, lakini Mungu hawajibu kwasababu ya kibriu ya watu waovu.
אך-שוא לא-ישמע אל ושדי לא ישורנה | 13 |
Kwa hakika Mungu hatasikia kilio cha kipumbavu; Mwenye nguvu wala hatajali.
אף כי-תאמר לא תשורנו דין לפניו ותחולל לו | 14 |
Ni kwa namna gani atakujibu ikiwa unasema haumwoni, na ya kwamba hoja yako iko mbele yake, na ya kuwa unamngojea yeye!
ועתה--כי-אין פקד אפו ולא-ידע בפש מאד | 15 |
Ni kwa jinsi gani atakujibu kama unasema kwamba hamwadhibu yeyote kwa hasira, na ya kwamba hajishughulishi na kiburi cha watu.
ואיוב הבל יפצה-פיהו בבלי-דעת מלין יכבר | 16 |
Basi Ayubu hufumbua kinywa chake tu ili kusema upumbavu; huongeza maneno bila maarifa.”