< איוב 34 >
שמעו חכמים מלי וידעים האזינו לי | 2 |
“Sikieni maneno yangu, enyi watu wenye hekima; nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye maarifa.
כי-אזן מלין תבחן וחך יטעם לאכל | 3 |
Kwa kuwa sikio huyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula.
משפט נבחרה-לנו נדעה בינינו מה-טוב | 4 |
Tujichagulie wenyewe yaliyo sawa, nasi tujifunze pamoja yaliyo mema.
כי-אמר איוב צדקתי ואל הסיר משפטי | 5 |
“Ayubu anasema, ‘Mimi sina hatia, lakini Mungu ameninyima haki yangu.
על-משפטי אכזב אנוש חצי בלי-פשע | 6 |
Ingawa niko sawa, ninaonekana mwongo; nami ingawa sina kosa, kidonda changu hakiponi.’
מי-גבר כאיוב ישתה-לעג כמים | 7 |
Ni mtu gani aliye kama Ayubu, anywaye dharau kama maji?
וארח לחברה עם-פעלי און וללכת עם-אנשי-רשע | 8 |
Ashirikianaye na watenda mabaya na kuchangamana na watu waovu.
כי-אמר לא יסכן-גבר-- ברצתו עם-אלהים | 9 |
Kwa kuwa anasema, ‘Haimfaidi mwanadamu kitu chochote anapojitahidi kumpendeza Mungu.’
לכן אנשי לבב-- שמעו-לי חללה לאל מרשע ושדי מעול | 10 |
“Hivyo nisikilizeni mimi, ninyi watu wenye ufahamu. Kamwe Mungu hatendi uovu, Mwenyezi hafanyi kosa.
כי פעל אדם ישלם-לו וכארח איש ימצאנו | 11 |
Humlipa mwanadamu kwa ajili ya lile alilotenda; huleta juu yake kile ambacho matendo yake yanastahili.
אף-אמנם אל לא-ירשיע ושדי לא-יעות משפט | 12 |
Ni jambo lisiloweza kufikiriwa kwamba Mungu angefanya makosa, kwamba Mwenyezi angepotosha hukumu.
מי-פקד עליו ארצה ומי שם תבל כלה | 13 |
Je, ni nani aliyemtawaza juu ya dunia? Ni nani aliyemweka kuwa mwangalizi wa ulimwengu wote?
אם-ישים אליו לבו רוחו ונשמתו אליו יאסף | 14 |
Kama lilikuwa kusudi la Mungu, naye akaiondoa Roho yake na pumzi yake,
יגוע כל-בשר יחד ואדם על-עפר ישוב | 15 |
wanadamu wote wangeliangamia kwa pamoja, na mtu angerudi mavumbini.
ואם-בינה שמעה-זאת האזינה לקול מלי | 16 |
“Kama ninyi mnaufahamu, sikieni hili; sikilizeni hili nisemalo.
האף שונא משפט יחבוש ואם-צדיק כביר תרשיע | 17 |
Je, yeye aichukiaye haki aweza kutawala? Je, utamhukumu mwenye haki, Aliye na Nguvu Zote?
האמר למלך בליעל-- רשע אל-נדיבים | 18 |
Je, si ni yeye awaambiaye wafalme, ‘Ninyi hamfai kitu,’ nao watu mashuhuri, ‘Ninyi ni waovu,’
אשר לא-נשא פני שרים ולא נכר-שוע לפני-דל כי-מעשה ידיו כלם | 19 |
yeye asiyependelea wakuu, wala haonyeshi upendeleo kwa matajiri kuliko maskini, kwa kuwa wote ni kazi ya mikono yake?
רגע ימתו-- וחצות לילה יגעשו עם ויעברו ויסירו אביר לא ביד | 20 |
Wanakufa ghafula, usiku wa manane; watu wanatikiswa nao hupita; wenye nguvu huondolewa bila mkono wa mwanadamu.
כי-עיניו על-דרכי-איש וכל-צעדיו יראה | 21 |
“Macho yake yanazitazama njia za wanadamu; anaona kila hatua yao.
אין-חשך ואין צלמות-- להסתר שם פעלי און | 22 |
Hakuna mahali penye giza nene, wala uvuli mkubwa, ambapo watenda mabaya wanaweza kujificha.
כי לא על-איש ישים עוד-- להלך אל-אל במשפט | 23 |
Mungu hana haja ya kumchunguza mtu sana, ili apate kuja mbele zake kwa hukumu.
ירע כבירים לא-חקר ויעמד אחרים תחתם | 24 |
Bila kuuliza huwapondaponda wenye nguvu nyingi na kuwaweka wengine mahali pao.
לכן--יכיר מעבדיהם והפך לילה וידכאו | 25 |
Kwa sababu huyaangalia matendo yao yote, huwaondoa usiku, nao wakaangamia.
תחת-רשעים ספקם-- במקום ראים | 26 |
Anawaadhibu kwa ajili ya uovu wao mahali ambapo kila mmoja ataweza kuwaona,
אשר על-כן סרו מאחריו וכל-דרכיו לא השכילו | 27 |
kwa sababu wameacha kumfuata Mungu, nao hawakuiheshimu njia yake hata moja.
להביא עליו צעקת-דל וצעקת עניים ישמע | 28 |
Wamesababisha kilio cha maskini kifike mbele zake, hivyo akasikia kilio cha wahitaji.
והוא ישקט ומי ירשע-- ויסתר פנים ומי ישורנו ועל-גוי ועל-אדם יחד | 29 |
Lakini kama akinyamaza kimya, ni nani awezaye kumhukumu? Kama akiuficha uso wake, ni nani awezaye kumwona? Ikiwa ni taifa au mtu mmoja, kwake ni sawa,
ממלך אדם חנף-- ממקשי עם | 30 |
ili kumzuia mtu mwovu kutawala, au wale ambao huwategea watu mitego.
כי-אל-אל האמר נשאתי-- לא אחבל | 31 |
“Kama mwanadamu akimwambia Mungu, ‘Nimekosa lakini sitatenda dhambi tena.
בלעדי אחזה אתה הרני אם-עול פעלתי לא אסיף | 32 |
Nifundishe nisichoweza kuona; kama nimekukosea, sitafanya hivyo tena.’
המעמך ישלמנה כי-מאסת--כי-אתה תבחר ולא-אני ומה-ידעת דבר | 33 |
Je basi, Mungu atakulipa kwa masharti yako, wakati wewe umekataa kutubu? Yakupasa wewe uamue, wala si mimi; sasa niambie lile ulijualo.
אנשי לבב יאמרו לי וגבר חכם שמע לי | 34 |
“Wanadamu wenye ufahamu husema, wenye hekima wanaonisikia huniambia,
איוב לא-בדעת ידבר ודבריו לא בהשכיל | 35 |
‘Ayubu huongea bila maarifa; maneno yake hayana busara.’
אבי--יבחן איוב עד-נצח על-תשבת באנשי-און | 36 |
Laiti Ayubu angejaribiwa hadi kikomo cha mwisho, kwa sababu anajibu kama mtu mwovu!
כי יסיף על-חטאתו פשע בינינו יספוק וירב אמריו לאל | 37 |
Kwenye dhambi yake huongeza uasi; kwa dharau hupiga makofi miongoni mwetu, na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”