< איוב 33 >

ואולם--שמע-נא איוב מלי וכל-דברי האזינה 1
Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
הנה-נא פתחתי פי דברה לשוני בחכי 2
Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
ישר-לבי אמרי ודעת שפתי ברור מללו 3
Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
רוח-אל עשתני ונשמת שדי תחיני 4
Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
אם-תוכל השיבני ערכה לפני התיצבה 5
Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
הן-אני כפיך לאל מחמר קרצתי גם-אני 6
Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
הנה אמתי לא תבעתך ואכפי עליך לא-יכבד 7
Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
אך אמרת באזני וקול מלין אשמע 8
Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
זך אני בלי-פשע חף אנכי ולא עון לי 9
'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
הן תנואות עלי ימצא יחשבני לאויב לו 10
Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
ישם בסד רגלי ישמר כל-ארחתי 11
Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
הן-זאת לא-צדקת אענך כי-ירבה אלוה מאנוש 12
Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
מדוע אליו ריבות כי כל-דבריו לא יענה 13
Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
כי-באחת ידבר-אל ובשתים לא ישורנה 14
Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
בחלום חזיון לילה--בנפל תרדמה על-אנשים בתנומות עלי משכב 15
Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
אז יגלה אזן אנשים ובמסרם יחתם 16
basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
להסיר אדם מעשה וגוה מגבר יכסה 17
kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
יחשך נפשו מני-שחת וחיתו מעבר בשלח 18
Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
והוכח במכאוב על-משכבו וריב (ורוב) עצמיו אתן 19
Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
וזהמתו חיתו לחם ונפשו מאכל תאוה 20
ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
יכל בשרו מראי ושפי (ושפו) עצמתיו לא ראו 21
Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
ותקרב לשחת נפשו וחיתו לממתים 22
Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
אם-יש עליו מלאך--מליץ אחד מני-אלף להגיד לאדם ישרו 23
Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
ויחננו--ויאמר פדעהו מרדת שחת מצאתי כפר 24
na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
רטפש בשרו מנער ישוב לימי עלומיו 25
kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
יעתר אל-אלוה וירצהו וירא פניו בתרועה וישב לאנוש צדקתו 26
Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
ישר על-אנשים ויאמר חטאתי וישר העויתי ולא-שוה לי 27
Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
פדה נפשי (נפשו) מעבר בשחת וחיתי (וחיתו) באור תראה 28
Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
הן-כל-אלה יפעל-אל-- פעמים שלוש עם-גבר 29
Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
להשיב נפשו מני-שחת-- לאור באור החיים 30
kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
הקשב איוב שמע-לי החרש ואנכי אדבר 31
Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
אם-יש-מלין השיבני דבר כי-חפצתי צדקך 32
Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
אם-אין אתה שמע-לי החרש ואאלפך חכמה 33
Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”

< איוב 33 >