< איוב 26 >
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
מה-עזרת ללא-כח הושעת זרוע לא-עז | 2 |
“Mmemsaidiaje aliyedhaifu!
מה-יעצת ללא חכמה ותשיה לרב הודעת | 3 |
Jinsi gani mmemshauri asiye na hekima na kutamka maneno yenye maarifa kwake!
את-מי הגדת מלין ונשמת-מי יצאה ממך | 4 |
Kwa msaada wa nani mmesema maneno haya? Ni roho ya nani iliyotoka ndani yenu?
הרפאים יחוללו-- מתחת מים ושכניהם | 5 |
Maiti inatetemeka chini ya maji, na vyote wilivyomo ndani yake.
ערום שאול נגדו ואין כסות לאבדון (Sheol ) | 6 |
Kuzimu kuko wazi mbele ya Mungu; uharibifu hauna kizuizi dhidi yake. (Sheol )
נטה צפון על-תהו תלה ארץ על-בלימה | 7 |
Huitandaza kaskazi juu ya nafasi wazi na kuining'iniza dunia hewani.
צרר-מים בעביו ולא-נבקע ענן תחתם | 8 |
Huyafunga maji katika mawingu yake mazito, lakini hayagawanyiki chini yake.
מאחז פני-כסה פרשז עליו עננו | 9 |
Huufunika uso wa mwezi na kueneza mawingu yake juu yake.
חק-חג על-פני-מים-- עד-תכלית אור עם-חשך | 10 |
Amechora ukingo wa duara juu ya maji kama mpaka kati ya nuru na giza.
עמודי שמים ירופפו ויתמהו מגערתו | 11 |
Nguzo za mbinguni zinatikisika na zimestushwa na kukemea kwake.
בכחו רגע הים ובתובנתו (ובתבונתו) מחץ רהב | 12 |
Aliituliza bahari kwa uwezo wake; kwa ufahamu wake alimwaribu Rahab
ברוחו שמים שפרה חללה ידו נחש ברח | 13 |
Kwa pumzi yake, aliziondoa mbingu kwa dhorubu; mbingu ziliondolewa kwa dhorubu; mkono wake ulimchoma nyoka anayekimbia.
הן-אלה קצות דרכו-- ומה-שמץ דבר נשמע-בו ורעם גבורתו מי יתבונן | 14 |
Tazama, hizi si zaidi ya madogo ya njia zake; Jinsi gani tunasikia akitunong'oneza! Ni nani awezaye kufahamu uwezo wake.