< איוב 23 >
גם-היום מרי שחי ידי כבדה על-אנחתי | 2 |
“Hata leo malalamiko yangu ni chungu; mkono wake ni mzito juu yangu hata nikiugua.
מי-יתן ידעתי ואמצאהו אבוא עד-תכונתו | 3 |
Laiti ningefahamu mahali pa kumwona; laiti ningeweza kwenda mahali akaapo!
אערכה לפניו משפט ופי אמלא תוכחות | 4 |
Ningeliweka shauri langu mbele zake, na kukijaza kinywa changu na hoja.
אדעה מלים יענני ואבינה מה-יאמר לי | 5 |
Ningejua kwamba angenijibu nini, na kuelewa lile ambalo angelisema.
הברב-כח יריב עמדי לא אך-הוא ישם בי | 6 |
Je, angenipinga kwa nguvu nyingi? La, asingenigandamiza.
שם--ישר נוכח עמו ואפלטה לנצח משפטי | 7 |
Hapo mtu mwadilifu angeweka shauri lake mbele zake, nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu.
הן קדם אהלך ואיננו ואחור ולא-אבין לו | 8 |
“Lakini nikienda mashariki, hayupo; nikienda magharibi, simpati.
שמאול בעשתו ולא-אחז יעטף ימין ולא אראה | 9 |
Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni; akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.
כי-ידע דרך עמדי בחנני כזהב אצא | 10 |
Lakini anaijua njia niiendeayo; akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.
באשרו אחזה רגלי דרכו שמרתי ולא-אט | 11 |
Nyayo zangu zimefuata hatua zake kwa karibu; nimeishika njia yake bila kukengeuka.
מצות שפתיו ולא אמיש מחקי צפנתי אמרי-פיו | 12 |
Sijaziacha amri zilizotoka midomoni mwake; nimeyathamini maneno ya kinywa chake kuliko chakula changu cha kila siku.
והוא באחד ומי ישיבנו ונפשו אותה ויעש | 13 |
“Lakini yeye husimama peke yake; ni nani awezaye kumpinga? Yeye hufanya lolote atakalo.
כי ישלים חקי וכהנה רבות עמו | 14 |
Hutimiliza maagizo yake dhidi yangu, na bado anayo mipango mingi kama hiyo ambayo ameiweka akiba.
על-כן מפניו אבהל אתבונן ואפחד ממנו | 15 |
Hiyo ndiyo sababu ninaingiwa na hofu mbele zake; nifikiriapo haya yote ninamwogopa.
ואל הרך לבי ושדי הבהילני | 16 |
Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia; yeye Mwenyezi amenitia hofu.
כי-לא נצמתי מפני-חשך ומפני כסה-אפל | 17 |
Hata hivyo sijanyamazishwa na giza, wala kwa giza nene linalofunika uso wangu.