< איוב 23 >

ויען איוב ויאמר 1
Ndipo Ayubu akajibu:
גם-היום מרי שחי ידי כבדה על-אנחתי 2
“Hata leo malalamiko yangu ni chungu; mkono wake ni mzito juu yangu hata nikiugua.
מי-יתן ידעתי ואמצאהו אבוא עד-תכונתו 3
Laiti ningefahamu mahali pa kumwona; laiti ningeweza kwenda mahali akaapo!
אערכה לפניו משפט ופי אמלא תוכחות 4
Ningeliweka shauri langu mbele zake, na kukijaza kinywa changu na hoja.
אדעה מלים יענני ואבינה מה-יאמר לי 5
Ningejua kwamba angenijibu nini, na kuelewa lile ambalo angelisema.
הברב-כח יריב עמדי לא אך-הוא ישם בי 6
Je, angenipinga kwa nguvu nyingi? La, asingenigandamiza.
שם--ישר נוכח עמו ואפלטה לנצח משפטי 7
Hapo mtu mwadilifu angeweka shauri lake mbele zake, nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu.
הן קדם אהלך ואיננו ואחור ולא-אבין לו 8
“Lakini nikienda mashariki, hayupo; nikienda magharibi, simpati.
שמאול בעשתו ולא-אחז יעטף ימין ולא אראה 9
Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni; akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.
כי-ידע דרך עמדי בחנני כזהב אצא 10
Lakini anaijua njia niiendeayo; akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.
באשרו אחזה רגלי דרכו שמרתי ולא-אט 11
Nyayo zangu zimefuata hatua zake kwa karibu; nimeishika njia yake bila kukengeuka.
מצות שפתיו ולא אמיש מחקי צפנתי אמרי-פיו 12
Sijaziacha amri zilizotoka midomoni mwake; nimeyathamini maneno ya kinywa chake kuliko chakula changu cha kila siku.
והוא באחד ומי ישיבנו ונפשו אותה ויעש 13
“Lakini yeye husimama peke yake; ni nani awezaye kumpinga? Yeye hufanya lolote atakalo.
כי ישלים חקי וכהנה רבות עמו 14
Hutimiliza maagizo yake dhidi yangu, na bado anayo mipango mingi kama hiyo ambayo ameiweka akiba.
על-כן מפניו אבהל אתבונן ואפחד ממנו 15
Hiyo ndiyo sababu ninaingiwa na hofu mbele zake; nifikiriapo haya yote ninamwogopa.
ואל הרך לבי ושדי הבהילני 16
Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia; yeye Mwenyezi amenitia hofu.
כי-לא נצמתי מפני-חשך ומפני כסה-אפל 17
Hata hivyo sijanyamazishwa na giza, wala kwa giza nene linalofunika uso wangu.

< איוב 23 >