< איוב 22 >

ויען אליפז התמני ויאמר 1
Ndipo Elifazi Mtemani akajibu:
הלאל יסכן-גבר-- כי-יסכן עלימו משכיל 2
“Je, mwanadamu aweza kuwa wa faida kwa Mungu? Je, hata mtu mwenye hekima aweza kumfaidi?
החפץ לשדי כי תצדק ואם-בצע כי-תתם דרכיך 3
Je, Mwenyezi angefurahia nini kama ungekuwa mwadilifu? Au je, yeye angepata faida gani kama njia zako zingekuwa kamilifu?
המיראתך יכיחך יבוא עמך במשפט 4
“Je, ni kwa ajili ya utaua wako ndiyo maana anakukemea na kuleta mashtaka dhidi yako?
הלא רעתך רבה ואין-קץ לעונתיך 5
Je, uovu wako si mkuu? Dhambi zako si hazina mwisho?
כי-תחבל אחיך חנם ובגדי ערומים תפשיט 6
Umedai dhamana kwa ndugu zako bila sababu; umewavua watu nguo zao, ukawaacha uchi.
לא-מים עיף תשקה ומרעב תמנע-לחם 7
Hukumpa maji aliyechoka, nawe ulimnyima chakula mwenye njaa,
ואיש זרוע לו הארץ ונשוא פנים ישב בה 8
ingawa ulikuwa mtu mwenye uwezo ukimiliki nchi: mtu uliyeheshimiwa, ukiishi ndani yake.
אלמנות שלחת ריקם וזרעות יתמים ידכא 9
Umewafukuza wajane mikono mitupu na kuzivunja nguvu za yatima.
על-כן סביבותיך פחים ויבהלך פחד פתאם 10
Ndiyo sababu mitego imekuzunguka pande zote, hatari ya ghafula inakutia hofu,
או-חשך לא-תראה ושפעת-מים תכסך 11
ndiyo sababu ni giza sana huwezi kuona, tena ndiyo sababu mafuriko ya maji yamekufunika.
הלא-אלוה גבה שמים וראה ראש כוכבים כי-רמו 12
“Je, Mungu hayuko katika mbingu za juu? Juu kuliko nyota zilizo juu sana!
ואמרת מה-ידע אל הבעד ערפל ישפוט 13
Hivyo wewe wasema, ‘Mungu anajua nini?’ Je, yeye huhukumu katika giza kama hilo?
עבים סתר-לו ולא יראה וחוג שמים יתהלך 14
Mawingu mazito ni pazia lake, hivyo hatuoni sisi atembeapo juu ya anga la dunia.
הארח עולם תשמור-- אשר דרכו מתי-און 15
Je, utaifuata njia ya zamani, ambayo watu waovu waliikanyaga?
אשר-קמטו ולא-עת נהר יוצק יסודם 16
Waliondolewa kabla ya wakati wao, misingi yao ikachukuliwa na mafuriko.
האמרים לאל סור ממנו ומה-יפעל שדי למו 17
Walimwambia Mungu, ‘Tuache sisi! Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?’
והוא מלא בתיהם טוב ועצת רשעים רחקה מני 18
Lakini ndiye alizijaza nyumba zao na vitu vizuri, hivyo ninajitenga mbali na mashauri ya waovu.
יראו צדיקים וישמחו ונקי ילעג-למו 19
“Wenye haki wanaona maangamizi yao na kufurahi, nao wasio na hatia huwadhihaki, wakisema,
אם-לא נכחד קימנו ויתרם אכלה אש 20
‘Hakika adui zetu wameangamizwa, nao moto umeteketeza mali zao.’
הסכן-נא עמו ושלם בהם תבואתך טובה 21
“Mjue sana Mungu ili uwe na amani, ndipo mema yatakapokujia.
קח-נא מפיו תורה ושים אמריו בלבבך 22
Uyapokee mafundisho toka kinywani mwake, na maneno yake uyaweke moyoni mwako.
אם-תשוב עד-שדי תבנה תרחיק עולה מאהלך 23
Kama ukimrudia Mwenyezi, utarudishwa upya: Kama ukiuondoa uovu uwe mbali na hema lako,
ושית-על-עפר בצר ובצור נחלים אופיר 24
kama dhahabu yako ukiihesabu kama mavumbi, dhahabu yako ya Ofiri kama miamba ya mabondeni,
והיה שדי בצריך וכסף תועפות לך 25
ndipo Mwenyezi atakuwa dhahabu yako, naye atakuwa fedha yako iliyo bora.
כי-אז על-שדי תתענג ותשא אל-אלוה פניך 26
Hakika ndipo utakapojifurahisha kwa Mwenyezi, nawe utamwinulia Mungu uso wako.
תעתיר אליו וישמעך ונדריך תשלם 27
Utamwomba yeye, naye atakusikia, nawe utazitimiza nadhiri zako.
ותגזר-אמר ויקם לך ועל-דרכיך נגה אור 28
Utakusudia jambo nalo litatendeka, nao mwanga utaangazia njia zako.
כי-השפילו ותאמר גוה ושח עינים יושע 29
Watu watakaposhushwa, nawe ukasema, ‘Wainue!’ ndipo atamwokoa aliyevunjika moyo.
ימלט אי-נקי ונמלט בבר כפיך 30
Atamwokoa hata yule ambaye ana hatia, ataokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.”

< איוב 22 >