< איוב 22 >
Ndipo Elifazi Mtemani akajibu:
הלאל יסכן-גבר-- כי-יסכן עלימו משכיל | 2 |
“Je, mwanadamu aweza kuwa wa faida kwa Mungu? Je, hata mtu mwenye hekima aweza kumfaidi?
החפץ לשדי כי תצדק ואם-בצע כי-תתם דרכיך | 3 |
Je, Mwenyezi angefurahia nini kama ungekuwa mwadilifu? Au je, yeye angepata faida gani kama njia zako zingekuwa kamilifu?
המיראתך יכיחך יבוא עמך במשפט | 4 |
“Je, ni kwa ajili ya utaua wako ndiyo maana anakukemea na kuleta mashtaka dhidi yako?
הלא רעתך רבה ואין-קץ לעונתיך | 5 |
Je, uovu wako si mkuu? Dhambi zako si hazina mwisho?
כי-תחבל אחיך חנם ובגדי ערומים תפשיט | 6 |
Umedai dhamana kwa ndugu zako bila sababu; umewavua watu nguo zao, ukawaacha uchi.
לא-מים עיף תשקה ומרעב תמנע-לחם | 7 |
Hukumpa maji aliyechoka, nawe ulimnyima chakula mwenye njaa,
ואיש זרוע לו הארץ ונשוא פנים ישב בה | 8 |
ingawa ulikuwa mtu mwenye uwezo ukimiliki nchi: mtu uliyeheshimiwa, ukiishi ndani yake.
אלמנות שלחת ריקם וזרעות יתמים ידכא | 9 |
Umewafukuza wajane mikono mitupu na kuzivunja nguvu za yatima.
על-כן סביבותיך פחים ויבהלך פחד פתאם | 10 |
Ndiyo sababu mitego imekuzunguka pande zote, hatari ya ghafula inakutia hofu,
או-חשך לא-תראה ושפעת-מים תכסך | 11 |
ndiyo sababu ni giza sana huwezi kuona, tena ndiyo sababu mafuriko ya maji yamekufunika.
הלא-אלוה גבה שמים וראה ראש כוכבים כי-רמו | 12 |
“Je, Mungu hayuko katika mbingu za juu? Juu kuliko nyota zilizo juu sana!
ואמרת מה-ידע אל הבעד ערפל ישפוט | 13 |
Hivyo wewe wasema, ‘Mungu anajua nini?’ Je, yeye huhukumu katika giza kama hilo?
עבים סתר-לו ולא יראה וחוג שמים יתהלך | 14 |
Mawingu mazito ni pazia lake, hivyo hatuoni sisi atembeapo juu ya anga la dunia.
הארח עולם תשמור-- אשר דרכו מתי-און | 15 |
Je, utaifuata njia ya zamani, ambayo watu waovu waliikanyaga?
אשר-קמטו ולא-עת נהר יוצק יסודם | 16 |
Waliondolewa kabla ya wakati wao, misingi yao ikachukuliwa na mafuriko.
האמרים לאל סור ממנו ומה-יפעל שדי למו | 17 |
Walimwambia Mungu, ‘Tuache sisi! Huyo Mwenyezi aweza kutufanyia nini?’
והוא מלא בתיהם טוב ועצת רשעים רחקה מני | 18 |
Lakini ndiye alizijaza nyumba zao na vitu vizuri, hivyo ninajitenga mbali na mashauri ya waovu.
יראו צדיקים וישמחו ונקי ילעג-למו | 19 |
“Wenye haki wanaona maangamizi yao na kufurahi, nao wasio na hatia huwadhihaki, wakisema,
אם-לא נכחד קימנו ויתרם אכלה אש | 20 |
‘Hakika adui zetu wameangamizwa, nao moto umeteketeza mali zao.’
הסכן-נא עמו ושלם בהם תבואתך טובה | 21 |
“Mjue sana Mungu ili uwe na amani, ndipo mema yatakapokujia.
קח-נא מפיו תורה ושים אמריו בלבבך | 22 |
Uyapokee mafundisho toka kinywani mwake, na maneno yake uyaweke moyoni mwako.
אם-תשוב עד-שדי תבנה תרחיק עולה מאהלך | 23 |
Kama ukimrudia Mwenyezi, utarudishwa upya: Kama ukiuondoa uovu uwe mbali na hema lako,
ושית-על-עפר בצר ובצור נחלים אופיר | 24 |
kama dhahabu yako ukiihesabu kama mavumbi, dhahabu yako ya Ofiri kama miamba ya mabondeni,
והיה שדי בצריך וכסף תועפות לך | 25 |
ndipo Mwenyezi atakuwa dhahabu yako, naye atakuwa fedha yako iliyo bora.
כי-אז על-שדי תתענג ותשא אל-אלוה פניך | 26 |
Hakika ndipo utakapojifurahisha kwa Mwenyezi, nawe utamwinulia Mungu uso wako.
תעתיר אליו וישמעך ונדריך תשלם | 27 |
Utamwomba yeye, naye atakusikia, nawe utazitimiza nadhiri zako.
ותגזר-אמר ויקם לך ועל-דרכיך נגה אור | 28 |
Utakusudia jambo nalo litatendeka, nao mwanga utaangazia njia zako.
כי-השפילו ותאמר גוה ושח עינים יושע | 29 |
Watu watakaposhushwa, nawe ukasema, ‘Wainue!’ ndipo atamwokoa aliyevunjika moyo.
ימלט אי-נקי ונמלט בבר כפיך | 30 |
Atamwokoa hata yule ambaye ana hatia, ataokolewa kwa sababu ya usafi wa mikono yako.”