< איוב 21 >
Kisha Ayubu akajibu na kusema,
שמעו שמוע מלתי ותהי-זאת תנחומתיכם | 2 |
“Sikilizeni hotuba yangu kwa makini, hii na iwe faraja yenu.
שאוני ואנכי אדבר ואחר דברי תלעיג | 3 |
Nimeteswa, lakini pia nitasema; nikisha kusema, endeleeni kudhihaki.
האנכי לאדם שיחי ואם-מדוע לא-תקצר רוחי | 4 |
Lakini kwangu mimi, malalamikio yangu ni kwa mtu? Kwa nini nisiwe mwenye subira?
פנו-אלי והשמו ושימו יד על-פה | 5 |
Nitazameni na mshangae, nanyi wekeni mkono wenu midomoni mwenu.
ואם-זכרתי ונבהלתי ואחז בשרי פלצות | 6 |
Ninapoyafikiria mateso yangu, ninaumizwa, mwili wangu unaogopa.
מדוע רשעים יחיו עתקו גם-גברו חיל | 7 |
Kwa nini waovu wanaendelea kuishi, wanazeeka, na kuwa na uwezo katika madaraka?
זרעם נכון לפניהם עמם וצאצאיהם לעיניהם | 8 |
Wazao wao wanathibitishwa mbele zao, na uzao wao unaimarika machoni pao.
בתיהם שלום מפחד ולא שבט אלוה עליהם | 9 |
Nyumba zao ziko salama mbali na hofu; wala fimbo ya Mungu haiko juu yao.
שורו עבר ולא יגעל תפלט פרתו ולא תשכל | 10 |
Dume lao la ng'ombe linazalisha; halishindwi kufanya hivyo; ng'ombe wao anazaa na hafishi ndama wake akiwa mchanga.
ישלחו כצאן עויליהם וילדיהם ירקדון | 11 |
Wanawapeleka wadogo wao kama kundi la kondoo, na watoto wao hucheza.
ישאו כתף וכנור וישמחו לקול עוגב | 12 |
Wanaimba kwa tari na vinubi na hufurahi kwa muziki na zomari.
יבלו (יכלו) בטוב ימיהם וברגע שאול יחתו (Sheol ) | 13 |
Wanatumia siku zao katika mafanikio, na wanashuka kuzimu kwa utulivu. (Sheol )
ויאמרו לאל סור ממנו ודעת דרכיך לא חפצנו | 14 |
Wanamwambia Mungu, 'Ondoka kwetu kwani hatutaki ufahamu wowote juu ya njia zako.
מה-שדי כי-נעבדנו ומה-נועיל כי נפגע-בו | 15 |
Mwenye enzi ni nani, hata tumwabudu? Tutafaidika na nini tukimwabudu? Tutapata faida gani ikiwa tutamwomba?
הן לא בידם טובם עצת רשעים רחקה מני | 16 |
Tazama, je mafanikio yao hayamo katika mikono yao wenyewe? Sina cha kufanya na ushauri wa waovu.
כמה נר-רשעים ידעך-- ויבא עלימו אידם חבלים יחלק באפו | 17 |
Mara ngapi taa za waovu huzimwa, au kwamba majanga huja juu yao? Mara ngapi inatokea kwamba Mungu husambaza huzuni kwao kwa hasira?
יהיו כתבן לפני-רוח וכמץ גנבתו סופה | 18 |
Ni mara ngapi inatokea kwamba wanakuwa kama mabua mbele ya upepo au kama makapi yanayopeperushwa na dhoruba?
אלוה יצפן-לבניו אונו ישלם אליו וידע | 19 |
Mnasema, 'Mungu huweka hatia ya mtu kwa watoto wake kuilipa.' Na alipe yeye mwenyewe, ili kwamba aweze kujua hatia yake mwenyewe.
יראו עינו כידו ומחמת שדי ישתה | 20 |
Acha macho yake yaone uangamivu wake mwenyewe, na acha anywe gadhabu ya Mwenyezi.
כי מה-חפצו בביתו אחריו ומספר חדשיו חצצו | 21 |
Kwani anaangaliaje familia yake mbele yake idadi ya miezi yake inapokwisha.
הלאל ילמד-דעת והוא רמים ישפוט | 22 |
Je kuna mtu anaweza kumfundisha Mungu maarifa kwa kuwa yeye huwaukumu hata walio juu?
זה--ימות בעצם תמו כלו שלאנן ושליו | 23 |
Mtu mmoja ufa katika nguvu zake kamili, akiwa na utulivu kabisa na kwa amani.
עטיניו מלאו חלב ומח עצמותיו ישקה | 24 |
Mwili wake hauna uhitaji, na kiini cha mifupa yake ina unyevu na afya njema.
וזה--ימות בנפש מרה ולא-אכל בטובה | 25 |
Mtu mwingine ufa kwa uchungu wa nafsi, bila kujifurahisha kwa jambo lolote jema.
יחד על-עפר ישכבו ורמה תכסה עליהם | 26 |
Wanazikwa kaburini wote kwa pamoja, funza wanawafunika wote.
הן ידעתי מחשבותיכם ומזמות עלי תחמסו | 27 |
Tazama, nayajua mawazo yenu, na jinsi mnavyotaka kunikosesha.
כי תאמרו איה בית-נדיב ואיה אהל משכנות רשעים | 28 |
Kwa kuwa mwasema, 'Iko wapi sasa nyumba ya mwana wa mfalme? Liko wapi kao alipokaa mwovu?'
הלא שאלתם עוברי דרך ואתתם לא תנכרו | 29 |
Je hamjawauliza wasafiri? Hamfahamu wanavyoweza kusema,
כי ליום איד יחשך רע ליום עברות יובלו | 30 |
kwamba mwovu anaepushwa na siku ya shida, na kwamba anawekwa mbali na siku ya gadhabu?
מי-יגיד על-פניו דרכו והוא-עשה מי ישלם-לו | 31 |
Ni nani atakaye ituhumu siku ya mwovu mbele yake? Ni nani atakayemwadhibu kwa alichokifanya?
והוא לקברות יובל ועל-גדיש ישקוד | 32 |
Hata hivyo atapelekwa kaburini; watu wataliona kaburi lake.
מתקו-לו רגבי-נחל ואחריו כל-אדם ימשוך ולפניו אין מספר | 33 |
Udongo wa bondeni utakuwa mtamu kwake; watu wote watamfuata, hata kuwe na watu wengi mbele yake.
ואיך תנחמוני הבל ותשובתיכם נשאר-מעל | 34 |
Ni jinsi gani basi mtanifariji bila kufikiri, kwa kuwa majibu yenu hayana lolote ila uongo?”