< איוב 20 >

ויען צפר הנעמתי ויאמר 1
Ndipo Sofari Mnaamathi akajibu:
לכן שעפי ישיבוני ובעבור חושי בי 2
“Mawazo yanayonisumbua yananisukuma kujibu, kwa sababu nimehangaika sana.
מוסר כלמתי אשמע ורוח מבינתי יענני 3
Ninasikia makaripio ambayo yananivunjia heshima, nao ufahamu wangu unanisukuma kujibu.
הזאת ידעת מני-עד מני שים אדם עלי-ארץ 4
“Hakika unajua jinsi ilivyokuwa tangu zamani, tangu zamani mwanadamu alipowekwa duniani,
כי רננת רשעים מקרוב ושמחת חנף עדי-רגע 5
macheko ya mtu mwovu ni ya muda mfupi, nayo furaha ya wasiomcha Mungu hudumu kwa kitambo tu.
אם-יעלה לשמים שיאו וראשו לעב יגיע 6
Ingawa kujikweza kwake hufikia mbinguni na kichwa chake hugusa mawingu,
כגללו לנצח יאבד ראיו יאמרו איו 7
ataangamia milele kama mavi yake mwenyewe. Wale waliomwona watauliza, ‘Yuko wapi?’
כחלום יעוף ולא ימצאהו וידד כחזיון לילה 8
Kama ndoto hutoweka, wala hapatikani tena, amefukuziwa mbali kama maono ya usiku.
עין שזפתו ולא תוסיף ולא-עוד תשורנו מקומו 9
Jicho lililomwona halitamwona tena; mahali pake hapatamwona tena.
בניו ירצו דלים וידיו תשבנה אונו 10
Watoto wake watalipa yote baba yao aliyowadhulumu maskini, nayo mikono yake itarudisha mali yote aliyonyangʼanya watu.
עצמותיו מלאו עלומו ועמו על-עפר תשכב 11
Nguvu za ujana zilizoijaza mifupa yake, zitalala naye mavumbini.
אם-תמתיק בפיו רעה-- יכחידנה תחת לשנו 12
“Ingawa uovu ni mtamu kinywani mwake naye huuficha chini ya ulimi wake,
יחמל עליה ולא יעזבנה וימנענה בתוך חכו 13
ingawa hawezi kukubali kuuachia uende, lakini huuweka kinywani mwake.
לחמו במעיו נהפך מרורת פתנים בקרבו 14
Hata hivyo chakula chake kitakuwa kichungu tumboni mwake, nacho kitakuwa sumu kali ya nyoka ndani yake.
חיל בלע ויקאנו מבטנו ירשנו אל 15
Atatema mali alizozimeza; Mungu atalifanya tumbo lake kuzitapika.
ראש-פתנים יינק תהרגהו לשון אפעה 16
Atanyonya sumu za majoka; meno ya nyoka mwenye sumu kali yatamuua.
אל-ירא בפלגות-- נהרי נחלי דבש וחמאה 17
Hatafurahia vijito, mito inayotiririsha asali na siagi.
משיב יגע ולא יבלע כחיל תמורתו ולא יעלס 18
Vile alivyovitaabikia atavirudisha bila kuvila; hatafurahia faida itokanayo na biashara yake.
כי-רצץ עזב דלים בית גזל ולא יבנהו 19
Kwa kuwa aliwaonea maskini na kuwaacha pasipo kitu; amenyangʼanya kwa nguvu nyumba asizozijenga.
כי לא-ידע שלו בבטנו בחמודו לא ימלט 20
“Hakika hatakuwa na raha katika kutamani kwake sana; hawezi kujiokoa mwenyewe kwa hazina zake.
אין-שריד לאכלו על-כן לא-יחיל טובו 21
Hakuna chochote kitakachosalia kwa ajili yake ili ale; kufanikiwa kwake hakutadumu.
במלאות שפקו יצר לו כל-יד עמל תבאנו 22
Katikati ya wingi wa ustawi wake, dhiki itampata; taabu itamjia kwa nguvu zote.
יהי למלא בטנו--ישלח-בו חרון אפו וימטר עלימו בלחומו 23
Atakapokuwa amelijaza tumbo lake, Mungu ataionyesha ghadhabu kali dhidi yake, na kumnyeshea mapigo juu yake.
יברח מנשק ברזל תחלפהו קשת נחושה 24
Ijapokuwa aikimbia silaha ya chuma, mshale wa shaba utamchoma.
שלף ויצא מגוה וברק ממררתו יהלך עליו אמים 25
Atauchomoa katika mgongo wake, ncha ingʼaayo kutoka ini lake. Vitisho vitakuja juu yake;
כל-חשך טמון לצפוניו תאכלהו אש לא-נפח ירע שריד באהלו 26
giza nene linavizia hazina zake. Moto usiopepewa na mtu utamteketeza, na kuangamiza yaliyosalia nyumbani mwake.
יגלו שמים עונו וארץ מתקוממה לו 27
Mbingu zitaweka wazi hatia yake, nayo nchi itainuka kinyume chake.
יגל יבול ביתו נגרות ביום אפו 28
Mafuriko yataichukua nyumba yake, maji yaendayo kasi katika siku ya ghadhabu ya Mungu.
זה חלק-אדם רשע--מאלהים ונחלת אמרו מאל 29
Hili ndilo fungu Mungu alilowagawia waovu, urithi uliowekwa kwa ajili yao na Mungu.”

< איוב 20 >