< איוב 15 >
ויען אליפז התימני ויאמר | 1 |
Ndipo Elifazi Mtemani alijibu na kusema,
החכם יענה דעת-רוח וימלא קדים בטנו | 2 |
Mtu mwenye hekima anapaswa kujibu kwa maarifa yasiyofaa na kujijaza mwenyewe na upepo wa mashariki?
הוכח בדבר לא-יסכון ומלים לא-יועיל בם | 3 |
Anapaswa kuhojiana na mazungumzo yasiyo na faida au na hotuba ambazo kwa hizo yeye hawezi kufanya mema?
אף-אתה תפר יראה ותגרע שיחה לפני-אל | 4 |
Dhahiri, wewe wafifisha heshima ya Mungu; Wewe wazuia heshima kwa yeye,
כי יאלף עונך פיך ותבחר לשון ערומים | 5 |
kwa maana uovu wako hufundisha midomo yako; Wewe wachagua kuwa na ulimi wa mtu mwenye hila.
ירשיעך פיך ולא-אני ושפתיך יענו-בך | 6 |
Mdomo wako mwenyewe hukukukumu wewe, siyo wangu; hakika, midomo yako mwenyewe hushuhudia dhidi yako wewe.
הראישון אדם תולד ולפני גבעות חוללת | 7 |
Je, wewe ni mwanadamu wa kwanza ambaye aliyezaliwa? Wewe ulikuwepo kabla ya vilima kuwepo?
הבסוד אלוה תשמע ותגרע אליך חכמה | 8 |
Wewe Umewahi kusikia maarifa ya siri ya Mungu? Je, wewe wajihesabia mwenye hekima wewe mwenyewe?
מה-ידעת ולא נדע תבין ולא-עמנו הוא | 9 |
Ni kitu gani unachokifahamu wewe ambacho sisi hatukijui? Ni kitu gani unachokifahamu wewe ambacho hakiko katika sisi?
גם-שב גם-ישיש בנו-- כביר מאביך ימים | 10 |
Pamoja nasi wapo pia wenye mvi na watu wazee sana ambao ni wazee zaidi kuliko baba yako.
המעט ממך תנחומות אל ודבר לאט עמך | 11 |
Je, faraja ya Mungu ni ndogo sana kwako, maneno ambayo ni ya upole dhidi yako wewe?
מה-יקחך לבך ומה-ירזמון עיניך | 12 |
Kwa nini moyo wako wewe unakupeleka mbali? Kwa nini macho yako yananga'ra,
כי-תשיב אל-אל רוחך והצאת מפיך מלין | 13 |
ili ya kwamba kuirejesha roho yako kwa Mungu na kuyatoa maneno hayo kutoka katika mdomo wako?
מה-אנוש כי-יזכה וכי-יצדק ילוד אשה | 14 |
Je, mwanadamu yeye ni nini kwamba yeye anapaswa kuwa safi? Yeye mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke ni nini kwamba yeye anapaswa awe mwenye haki?
הן בקדשו לא יאמין ושמים לא-זכו בעיניו | 15 |
Tazama, Mungu haweki tumaini lake hata kwa mmoja wake aliye mtakatifu; Hakika, mbingu haziko safi machoni pake yeye;
אף כי-נתעב ונאלח איש-שתה כמים עולה | 16 |
jinsi gani asivyo safi ni mmoja aliye mbaya na mla rushwa, mtu ambaye hunywa uovu kama maji!
אחוך שמע-לי וזה-חזיתי ואספרה | 17 |
Mimi nitakuonyesha wewe; Nisikilize mimi; Mimi nitakutangazia wewe vitu ambavyo nimeviona,
אשר-חכמים יגידו ולא כחדו מאבותם | 18 |
vitu ambavyo watu wenye hekima wamepita chini yake kutoka kwa baba zao, vile vitu ambavyo mababu zao hawakuvificha.
להם לבדם נתנה הארץ ולא-עבר זר בתוכם | 19 |
Hawa walikuwa mababu zao, ambao kwao pekee nchi walipewa, na miongoni mwao hakuna mgeni aliyepita.
כל-ימי רשע הוא מתחולל ומספר שנים נצפנו לעריץ | 20 |
Mtu mwovu hupitia katika maumivu siku zake zote, idadi ya miaka iliyowekwa juu kwa mtesaji kuteseka.
קול-פחדים באזניו בשלום שודד יבואנו | 21 |
Sauti ya vitisho katika masikio yake; pindi yeye yuko katika kufanikiwa, mharibu atakuja juu yake yeye.
לא-יאמין שוב מני-חשך וצפו (וצפוי) הוא אלי-חרב | 22 |
Yeye hafikiri kwamba yeye atarudi kutoka katika giza; Upanga humngojea yeye.
נדד הוא ללחם איה ידע כי-נכון בידו יום-חשך | 23 |
Yeye huenda sehemu mbali mbali kwa ajili ya mkate, akisema, 'Kiko wapi? ' Yeye anatambua kuwa siku ya giza iko mkononi.
יבעתהו צר ומצוקה תתקפהו כמלך עתיד לכידור | 24 |
Dhiki na mateso makali humfanya aogope; wao hushinda dhidi yake yeye, kama mfalme tayari kwa vita.
כי-נטה אל-אל ידו ואל-שדי יתגבר | 25 |
Kwa sababu yeye ameunyosha mkono wake dhidi ya Mungu na ameishi kwa kiburi dhidi ya aliye mkuu,
ירוץ אליו בצואר בעבי גבי מגניו | 26 |
huyu mtu mwovu hukimbia kwa Mungu na shingo ngumu, kwa vifundo vikubwa vya ngao.
כי-כסה פניו בחלבו ויעש פימה עלי-כסל | 27 |
Hii ni kweli, hata ingawa yeye amefunika uso wake kwa mafuta yake na amekusanya mafuta juu ya viuno vyake,
וישכון ערים נכחדות--בתים לא-ישבו למו אשר התעתדו לגלים | 28 |
na ameishi katika miji yenye ukiwa; katika nyumba ambazo hakuna mwanadamu anayeishi humo sasa na ambazo zilikuwa tayari kuwa magofu.
לא-יעשר ולא-יקום חילו ולא-יטה לארץ מנלם | 29 |
Yeye hatakuwa tajiri; utajiri wake yeye hautadumu; hata kivuli chake hakitadumu katika nchi.
לא-יסור מני-חשך--ינקתו תיבש שלהבת ויסור ברוח פיו | 30 |
Yeye hatatoka nje ya giza; mwali wa moto utakausha matawi yake; katika pumzi ya kinywa cha Mungu yeye ataenda zake.
אל-יאמן בשו נתעה כי-שוא תהיה תמורתו | 31 |
Mwacheni yeye asitumaini katika vitu visivyofanya kazi, akijidanganya yeye mwenyewe; maana upuuzi utakuwa mshahara wake yeye.
בלא-יומו תמלא וכפתו לא רעננה | 32 |
Itatokea kabla ya wakati wake yeye atapaswa kufa; tawi lake halitakuwa kijani.
יחמס כגפן בסרו וישלך כזית נצתו | 33 |
Yeye atazipukutisha zabibu zake zisizovunwa kama mzabibu; yeye atayaondoa maua yake kama mti wa mzeituni.
כי-עדת חנף גלמוד ואש אכלה אהלי-שחד | 34 |
Kwa maana msaada wa watu wasiomcha Mungu utakuwa tasa; moto utateketeza hema za rushwa.
הרה עמל וילד און ובטנם תכין מרמה | 35 |
Wao wanabeba mimba yenye ubaya na kuzaa uovu; tumbo lao hutunga mimba ya udanganifu.