< איוב 12 >
אמנם כי אתם-עם ועמכם תמות חכמה | 2 |
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
גם-לי לבב כמוכם--לא-נפל אנכי מכם ואת-מי-אין כמו-אלה | 3 |
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
שחק לרעהו אהיה--קרא לאלוה ויענהו שחוק צדיק תמים | 4 |
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
לפיד בוז לעשתות שאנן-- נכון למועדי רגל | 5 |
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
ישליו אהלים לשדדים ובטחות למרגיזי אל-- לאשר הביא אלוה בידו | 6 |
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
ואולם--שאל-נא בהמות ותרך ועוף השמים ויגד-לך | 7 |
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
או שיח לארץ ותרך ויספרו לך דגי הים | 8 |
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
מי לא-ידע בכל-אלה כי יד-יהוה עשתה זאת | 9 |
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
אשר בידו נפש כל-חי ורוח כל-בשר-איש | 10 |
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
הלא-אזן מלין תבחן וחך אכל יטעם-לו | 11 |
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
בישישים חכמה וארך ימים תבונה | 12 |
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
עמו חכמה וגבורה לו עצה ותבונה | 13 |
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
הן יהרוס ולא יבנה יסגר על-איש ולא יפתח | 14 |
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
הן יעצר במים ויבשו וישלחם ויהפכו ארץ | 15 |
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
עמו עז ותושיה לו שגג ומשגה | 16 |
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
מוליך יועצים שולל ושפטים יהולל | 17 |
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
מוסר מלכים פתח ויאסר אזור במתניהם | 18 |
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
מוליך כהנים שולל ואתנים יסלף | 19 |
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
מסיר שפה לנאמנים וטעם זקנים יקח | 20 |
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
שופך בוז על-נדיבים ומזיח אפיקים רפה | 21 |
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
מגלה עמקות מני-חשך ויצא לאור צלמות | 22 |
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
משגיא לגוים ויאבדם שטח לגוים וינחם | 23 |
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
מסיר--לב ראשי עם-הארץ ויתעם בתהו לא-דרך | 24 |
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
ימששו-חשך ולא-אור ויתעם כשכור | 25 |
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.