< ישעה 24 >
הנה יהוה בוקק הארץ ובולקה ועוה פניה והפיץ ישביה | 1 |
Tazama, Bwana ataifanya dunia kuwa ukiwa na kuiharibu, naye atauharibu uso wake na kutawanya wakaao ndani yake:
והיה כעם ככהן כעבד כאדניו כשפחה כגברתה כקונה כמוכר כמלוה כלוה כנשה כאשר נשא בו | 2 |
ndivyo itakavyokuwa kwa makuhani na kwa watu, kwa bwana na kwa mtumishi, kwa bibi na kwa mtumishi wake wa kike, kwa muuzaji na kwa mnunuzi, kwa mkopaji na kwa mkopeshaji, kwa mdaiwa na kwa mdai.
הבוק תבוק הארץ והבוז תבז כי יהוה דבר את הדבר הזה | 3 |
Dunia itaharibiwa kabisa na kutekwa nyara kabisa. Bwana amesema neno hili.
אבלה נבלה הארץ אמללה נבלה תבל אמללו מרום עם הארץ | 4 |
Dunia inakauka na kunyauka, dunia inanyongʼonyea na kunyauka, waliotukuzwa wa dunia wananyongʼonyea.
והארץ חנפה תחת ישביה כי עברו תורת חלפו חק הפרו ברית עולם | 5 |
Dunia imetiwa unajisi na watu wake; wameacha kutii sheria, wamevunja amri na kuvunja agano la milele.
על כן אלה אכלה ארץ ויאשמו ישבי בה על כן חרו ישבי ארץ ונשאר אנוש מזער | 6 |
Kwa hiyo laana inaiteketeza dunia, watu wake lazima waichukue hatia yao. Kwa hiyo wakazi wa dunia wameteketezwa, nao waliosalia ni wachache sana.
אבל תירוש אמללה גפן נאנחו כל שמחי לב | 7 |
Divai mpya inakauka na mzabibu unanyauka, watu wote wafurahishao wanalia kwa huzuni.
שבת משוש תפים חדל שאון עליזים שבת משוש כנור | 8 |
Furaha ya matoazi imekoma, kelele za wenye furaha zimekoma, shangwe za kinubi zimenyamaza.
בשיר לא ישתו יין ימר שכר לשתיו | 9 |
Hawanywi tena mvinyo pamoja na wimbo, kileo ni kichungu kwa wanywaji wake.
נשברה קרית תהו סגר כל בית מבוא | 10 |
Mji ulioharibiwa umekuwa ukiwa, mlango wa kila nyumba umefungwa.
צוחה על היין בחוצות ערבה כל שמחה גלה משוש הארץ | 11 |
Barabarani wanalilia kupata mvinyo, furaha yote imegeuka kuwa majonzi, furaha yote imefukuziwa mbali na dunia.
נשאר בעיר שמה ושאיה יכת שער | 12 |
Mji umeachwa katika uharibifu, lango lake limevunjwa vipande.
כי כה יהיה בקרב הארץ בתוך העמים כנקף זית כעוללת אם כלה בציר | 13 |
Ndivyo itakavyokuwa duniani na miongoni mwa mataifa, kama vile wakati mzeituni upigwavyo, au kama vile wakati masazo yabakiavyo baada ya zabibu kuvunwa.
המה ישאו קולם ירנו בגאון יהוה צהלו מים | 14 |
Wanainua sauti zao, wanapiga kelele kwa furaha, kutoka magharibi wanasifu kwa ukelele utukufu wa Bwana.
על כן בארים כבדו יהוה באיי הים שם יהוה אלהי ישראל | 15 |
Kwa hiyo upande wa mashariki mpeni Bwana utukufu, liadhimisheni jina la Bwana, Mungu wa Israeli, katika visiwa vya bahari.
מכנף הארץ זמרת שמענו צבי לצדיק ואמר רזי לי רזי לי אוי לי בגדים בגדו ובגד בוגדים בגדו | 16 |
Kutoka miisho ya dunia tunasikia uimbaji: “Utukufu kwa Yule Mwenye Haki.” Lakini nilisema, “Ninadhoofika, ninadhoofika! Ole wangu! Watenda hila wanasaliti! Kwa hila watenda hila wanasaliti!”
פחד ופחת ופח עליך יושב הארץ | 17 |
Hofu, shimo na mtego vinakungojea, ewe mtu ukaaye duniani.
והיה הנס מקול הפחד יפל אל הפחת והעולה מתוך הפחת ילכד בפח כי ארבות ממרום נפתחו וירעשו מוסדי ארץ | 18 |
Kila akimbiaye asikiapo sauti ya hofu atatumbukia shimoni, naye yeyote apandaye kutoka shimoni, atanaswa kwenye mtego. Malango ya gharika ya mbinguni yamefunguliwa, misingi ya dunia inatikisika.
רעה התרעעה הארץ פור התפוררה ארץ מוט התמוטטה ארץ | 19 |
Dunia imepasuka, dunia imechanika, dunia imetikiswa kabisa.
נוע תנוע ארץ כשכור והתנודדה כמלונה וכבד עליה פשעה ונפלה ולא תסיף קום | 20 |
Dunia inapepesuka kama mlevi, inayumbayumba kama kibanda kwenye upepo; imelemewa sana na mzigo wa hatia ya uasi wake na ikianguka kamwe haitainuka tena.
והיה ביום ההוא יפקד יהוה על צבא המרום במרום ועל מלכי האדמה על האדמה | 21 |
Katika siku ile Bwana ataadhibu nguvu zilizoko mbinguni juu, na wafalme walioko duniani chini.
ואספו אספה אסיר על בור וסגרו על מסגר ומרב ימים יפקדו | 22 |
Watakusanywa pamoja kama wafungwa waliofungwa gerezani, watafungiwa gerezani na kuadhibiwa baada ya siku nyingi.
וחפרה הלבנה ובושה החמה כי מלך יהוה צבאות בהר ציון ובירושלם ונגד זקניו כבוד | 23 |
Mwezi utatiwa haya, nalo jua litaaibishwa; kwa maana Bwana Mwenye Nguvu Zote atawala juu ya Mlima Sayuni na katika Yerusalemu, tena mbele ya wazee wake kwa utukufu.